Nimemsikia Mhe. Bashe akihitimisha hotuba yake ya Bajeti ya Kilimo 2024/25 kwa kweli Mhe. Bashe yuko vizuri na imara katika kuongoza Wizara ya Kilimo.
Mhe. Bashe amezungumzia zao la ufuta, korosho, pamba, kahawa na mazao mchanganyiko. Kwa maelezo yale kama Serikali itifanyia kazi ushauri wake basi Tanzania tutafika mbali. Kilichonifurahisha ni jinsi watakaowezeshwa wakulima wa parachichi ambayo amesema watajengewa kiwanda na kujengewa stoo kubwa za kuhifadhia parachichi zao kabla hazijasafirishwa nje ya nchi. Pia amezungumza kuwarudisha Maafisa ugani madarasani kwa ajili ya refresher coutses ili waende na wakati.
Mhe. Bashe amezungumzia kujjenga kiwanda cha pamba ambacho kitazalisha nyuzi na siyo tulivyozoea kuuza marobota. Anataka tuuze final product na kupata fedha za kigeni nyingi. Mhe. Bashe pia amesema Wizara itanunua matrekta na kuanza vituo ambavyo hizo trekta zitawalimia wakulima kwa bei nafuu. Kwa kweli kama mipango hii itaenda kama alivyoshauri basi Tanzania tutafika mbali na mkulima mdogo atalima kwa tija.
Wito kwa Mhe. Rais. Ninakuomba sana usimbadilishe Mhe. Bashe Wizara na ninashauri aendelee kuwa Waziri wa Kilimo ili yote haya aliyoyashauri aendelee kuyasimamia. Katika Mawaziri wote ulio nao binafsi Mhe. Bashe ndiyo Waziri namba moja(ranking) na nakushauri umtumie sana. Wakulima wakifanikiwa ujue na wewe utapendwa na utafanikiwa.
Mhe. Bashe amezungumzia zao la ufuta, korosho, pamba, kahawa na mazao mchanganyiko. Kwa maelezo yale kama Serikali itifanyia kazi ushauri wake basi Tanzania tutafika mbali. Kilichonifurahisha ni jinsi watakaowezeshwa wakulima wa parachichi ambayo amesema watajengewa kiwanda na kujengewa stoo kubwa za kuhifadhia parachichi zao kabla hazijasafirishwa nje ya nchi. Pia amezungumza kuwarudisha Maafisa ugani madarasani kwa ajili ya refresher coutses ili waende na wakati.
Mhe. Bashe amezungumzia kujjenga kiwanda cha pamba ambacho kitazalisha nyuzi na siyo tulivyozoea kuuza marobota. Anataka tuuze final product na kupata fedha za kigeni nyingi. Mhe. Bashe pia amesema Wizara itanunua matrekta na kuanza vituo ambavyo hizo trekta zitawalimia wakulima kwa bei nafuu. Kwa kweli kama mipango hii itaenda kama alivyoshauri basi Tanzania tutafika mbali na mkulima mdogo atalima kwa tija.
Wito kwa Mhe. Rais. Ninakuomba sana usimbadilishe Mhe. Bashe Wizara na ninashauri aendelee kuwa Waziri wa Kilimo ili yote haya aliyoyashauri aendelee kuyasimamia. Katika Mawaziri wote ulio nao binafsi Mhe. Bashe ndiyo Waziri namba moja(ranking) na nakushauri umtumie sana. Wakulima wakifanikiwa ujue na wewe utapendwa na utafanikiwa.