Melki the Storyteller
JF-Expert Member
- May 3, 2022
- 5,701
- 9,779
Inauma saaana ndugu zangu. Licha ya kuwa pamoja naye katika masuala tofauti ya hapa na pale, nikimsapoti pale ninapoweza, akinisaidia kimawazo n.k Jana ndipo nilipatwa na ganzi ya mdomo baada ya kuufahamu ukweli. Licha ya kuufahamu ukweli mtupu, nimeshindwa namna ya kumkataa ama kumchana ukweli. Naumia moyo
Anaishi na dada yake lakini mara moja moja kwa wiki huwa anakuja kijana kuwaona ambaye wanadai kuwa ni kaka wa binti ninaempenda na mdogo wa binti ambaye ni dada wa binti nimpendaye
Siku ya jana ndipo nilipata ukweli kutoka kwa mashushu wanaolifahamu jiji na watu wake kwa ujumla kuwa huyo kijana ni mpenzi wa mpenzi wangu, lakini pia amewahi kumzagamua dada wa binti japo kwa usiri wa hali ya juu, si mnajua tena hakuna siri duniani?
Leo asubuhi nimemuomba simu binti ndipo kukutana na meseji za mshikaji akiwa ameseviwa kaka, mshkaji anadai mbona siku ya jana binti alimyeyusha? Ndipo binti kujitetea kuwa leo atakipeleka. Dakika chache baadae binti alikuja kuchukua simu yake kwa mshtuko mkubwa nisioneshe kama nimeona jambo lolote
Mida ya saa tatu wakati najiandaa kwenda kufungua kiduka changu, nalimshuhudia akiondoka huku akiwa kapendeza sana
Nimeshindwa kwenda kwenye biashara yangu. Mpaka sasa hivi hajarudi, sijui atalala uko uko jamani. Dah!
Anaishi na dada yake lakini mara moja moja kwa wiki huwa anakuja kijana kuwaona ambaye wanadai kuwa ni kaka wa binti ninaempenda na mdogo wa binti ambaye ni dada wa binti nimpendaye
Siku ya jana ndipo nilipata ukweli kutoka kwa mashushu wanaolifahamu jiji na watu wake kwa ujumla kuwa huyo kijana ni mpenzi wa mpenzi wangu, lakini pia amewahi kumzagamua dada wa binti japo kwa usiri wa hali ya juu, si mnajua tena hakuna siri duniani?
Leo asubuhi nimemuomba simu binti ndipo kukutana na meseji za mshikaji akiwa ameseviwa kaka, mshkaji anadai mbona siku ya jana binti alimyeyusha? Ndipo binti kujitetea kuwa leo atakipeleka. Dakika chache baadae binti alikuja kuchukua simu yake kwa mshtuko mkubwa nisioneshe kama nimeona jambo lolote
Mida ya saa tatu wakati najiandaa kwenda kufungua kiduka changu, nalimshuhudia akiondoka huku akiwa kapendeza sana
Nimeshindwa kwenda kwenye biashara yangu. Mpaka sasa hivi hajarudi, sijui atalala uko uko jamani. Dah!