Binti wa zamani
Platinum Member
- Nov 19, 2011
- 11,763
- 27,149
Huyu jirani yetu ni baba ni mtu mzima, tumepakana naye, na mara nyingi mida ya jioni anapenda kukaa kibarazani kwake juu ghorofani, na tushamzoea hivyo.
Usiku wa leo niko narudishia mapazia, ghafla namuona na binoculars (zile za kuonea mbali) ameelekeza huku kwangu anatuangalia na baada ya kuniona wala hajashtuka ameendelea tu kuangalia.
Sasa sijaelewa alikua anafanya vile kwa lengo gani, tumeongea na mtoto wake kwa simu ili amuulize maana niko mwenyewe na vijana wadogo tu na sikutaka kwenda hapo kwake usiku.
Usiku wa leo niko narudishia mapazia, ghafla namuona na binoculars (zile za kuonea mbali) ameelekeza huku kwangu anatuangalia na baada ya kuniona wala hajashtuka ameendelea tu kuangalia.
Sasa sijaelewa alikua anafanya vile kwa lengo gani, tumeongea na mtoto wake kwa simu ili amuulize maana niko mwenyewe na vijana wadogo tu na sikutaka kwenda hapo kwake usiku.
- Ingekua wewe kwenye hii situation ungefanyaje?
- Na vipi ushawahi kua na jirani ambaye ni kipengele? ilikuwaje ?