Nimekutana na Jini?

Nimekutana na Jini?

u
My dear polee na wala usiwe na hofu siwezi kukudhuru, nilitaka kukupa sapraiz tu kuwa nipo na

nakuona kila
utakapokwenda[/

QUOTE]
hahaha sasa utamuua mazima
 
Wewe ni muumini mzuri tu wa mambo hayo ila wewe mwenyewe ndiyo hujijui, asiamini hawezi linganisha tukio la paka na kuwa binadamu uliemuona mbele ya safari. Kumbuka umeeleza ulikua kasi kwenye gari, iweje uweze kumsoma mtu usoni mpaka macho yagongane, wakati ulikuwa unaendesha kasi.
 
Wewe ni muumini mzuri tu wa mambo hayo ila wewe mwenyewe ndiyo hujijui, asiamini hawezi linganisha tukio la paka na kuwa binadamu uliemuona mbele ya safari. Kumbuka umeeleza ulikua kasi kwenye gari, iweje uweze kumsoma mtu usoni mpaka macho yagongane, wakati ulikuwa unaendesha kasi.
Haya mjuaji, ni hivi alipotokea paka nilipunguza mwendo wakati namkwepa. Halafu huyo mwanamke nilimuona mita kumi mbele au ndio mbele ya safari hio?
 
We unakunywa konyagi unachanganya na safari then una drive kwanin usione jini kwa barabara.
 
Wewe ni muumini mzuri tu wa mambo hayo ila wewe mwenyewe ndiyo hujijui, asiamini hawezi linganisha tukio la paka na kuwa binadamu uliemuona mbele ya safari. Kumbuka umeeleza ulikua kasi kwenye gari, iweje uweze kumsoma mtu usoni mpaka macho yagongane, wakati ulikuwa unaendesha kasi.

MKUU hata mimi nimejiuliza swali hilo! Reading between the lines nafikiri stori hii inebuniwa/tungwa I might be wrong though.
 
pole ushauri wangu jitahidi usiwe unakimbiza gari wakati umelewa
sio vizuri bado tunakuhitaji
 
Haya mjuaji, ni hivi alipotokea paka nilipunguza mwendo wakati namkwepa. Halafu huyo mwanamke nilimuona mita kumi mbele au ndio mbele ya safari hio?
Wewe umekereka maelezo yangu tu.
 
Ha ha haaaa.. Unaijua nauli ya kutoka dar hadi katavi? Half Katavi ni mlisha mifugo nyumbani kwa Pinda kule Mpanda so ticket ya ndege kwa duu kama wewe haezi gharamikia. Unless ujitolee kwa kila kitu
Tuachane na huyo bwana ana stress za maisha tuu..... ila wajua Katavi mie nakuzimikia ile mbayaa hasa hayo masikio yako yananikonga moyo sijuwi nifanyaje
 
Kuna rafiki yangu aliwai kunisimulia kukutana na kitu kinachofanana sana na hicho na sikuwa na sababu ya kutokumuamini, kwa jinsi ninavyomfahamu.

Mimi siku niliyokanyaga paka tu nilijisikia vibaya sana hata kula sikuweza usiku ule. Huyo paka alijichanganya mwenyewe katikati ya tairi la mbele na la nyuma. Thread ya jamaa imenikumbusha exactly yule paka alivyokuwa akitaka kucross barabara...
R.I.P paka
 
Ndugu zangu mimi sio muumini wa haya mambo, sijui majini wanga siamini kama yapo. Ila leo kuna kitu kimenitokea kinaweza kubadili maoni yangu juu ya hivi viumbe.

Kama mjuavyo mwisho wa wiki huu unapilika nyingi za usiku na mimi leo nilikuwa kwenye misele ya usiku. Sasa wakati narudi mida ya saa kumi na robo hivi alfajiri hii nimeona vitu naona si vya kawaida.

Wakati narudi nyumbani niko peke yangu kwenye gari na barabarani ghafla akatokea paka mweupe anakatiza barabara . Kwa kawaida usiku huwa nakimbiza gari kidogo na ninaendesha katikati ya barabara, basi yule paka katokea upande wa kushoto anakatiza kueleke kulia.

Kwa instict za udereva nikanyunyiza breki kidooogo, nikahamia kushoto alipotoka nikamkwepa bila kashkashi. Kuangalia nyuma kwa kutumia vioo sikumuona yule paka! Kwenda mbele kama mita kumi nikamuona mwanamke wa kizungu 'blonde' kavaa gauni jeusi refu limefunika hadi viatu kasimama upande wa kulia wa barabara!

Nikamwangalia na yeye akaniangalia wakati napta macho yalipogongana mwili wote ukanisisimka! Kwa mazingira yale niliomkuta na muda huu si kawaida kukuta mwanamke kasimama peke yake awe wa kizungu au mswahili, ndugu zanguni huyu ni jini? Nimeandika hii habari kabla sijalala mkiona nipo kimya sana mjue ni athari za huyo 'jini'.

cc: mshana jr
ilikuwa maeneo gani mkuu?
 
Bado sijaweza kuamini katika haya mambo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom