Nimekutana na Jini?

Nimekutana na Jini?

Huyo alikuwa subian mkuu, ilikuwa kidogo tu aje makata eneo lao la promise hapo ndo ungeisoma... Bahati yako maana ana wivu hapo gari lingezima na kutiwa nguvuni...... Tehetehe!!!
 
Umenikumbusha kuna siku nimetoka bar saa tisa usiku na nilikuwa sijalewa kivile, ile nakaribia nyumbani nikaona watu ambao naweza kusema sio wa kawaida kutokana mwonekano wao.
Na ili nifike nyumbani iliuwa ni lazima nipite pale walipo. Sasa kutokana na pombe zangu na kujiamini nikaendelea kuwasogelea na nilipowakaribia nikawaambia kabisa sasa mi napita hapo hapo kati kati yenu ili mjue mi ni nani, na wenyewe wakasogea pembeni wawili upande wa kushoto na wawili upande wa kulia, nikapita.
Baada ya kupita nikawa najihisi tofauti, kama niko ndotoni hivi! Nikageuka ili niwatukane sikuwaona, nikasema ngoja nitukane hivyo hivyo hata kama siwaoni, sikuweza (ulimi uling'ang'ania juu)
Nikaendelea na safari, ikaanza kunyesha mvua na cha ajabu ile njia nimeizoea lakini nilitafuta njia ya kuchepukia nyumbani sikuiona, nilikuwa nazunguka maeneo yale yale hadi asubuhi saa kumi na mbili kasoro ndio nikafanikiwa.
Ile nafika nyumbani wanashangaa eti kwanini nimeloana, Kumbe ile mvua ilininyeshea mm tu!
 
Hahahaah kama unayazimikia haya masikio hakuna namna zaidi ya kufanya uumbaji upate kababy kenye masikio kama haya...!!!
Mimi nina masikio kama hayo kabisa. Tufanye mchakato
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom