Nimekumbuka zamani!!

Hi thread nimeipenda sana,
Kweli name imenikumbusha mbali sana….nakumbuka tukiwa shule ya msingi kabla ya kuingia darasani lazima tukimbie mchakamchaka…nakumbuka somo la sayansi kimu….mihogo ya kukaanga ilikuwa juu sana wakati wa mapumziko na bakora ukichelewa namba…
Nakumbuka tukiwa wadogo bado siku za sikukuu ilikuwa ndio swaga kwenda kutembea mjini maeneo ya feli na pale chini pembeni ya bahari siku hizi kumewekwa fensi….
Nakumbuka enzi tukiwa tunakwenda sinema kwenye theatres kama vile "Avalon,Empire,Empress,Odeon,New Chox na kule msasani Drive Inn" na sinema za kihindi kina Mithun na wengine…
Nakumbuka tulikuwa tunakwenda kuruka ukuta ili kuona mpira uwanja wa Taifa (ule wa zamani)…
Nakumbuka Corn Ice Cream za Bakhressa zilivyokuwa juu enzi hizo….

Mchakamchaka ....Chinjaaaa
Mchaka mchaka ...Chinjaaaaa
Nimesahau mwendelezo...alafu kulikua na mwingine unasema tungeweza tungemrudisha SOKOINE duniani!!!
Ehhh bila kusahau ngonjera na mashairi,.....
 
attachment.php

Swagga la STD 4 pepa imeisha....pilau imeliwa na soda
zimenywewa kilichobaki ni kupozz kwa picha....waone hao
wanaovizi kwa nyuma na wao waonekane!!!!

attachment.php

Ubarikio....yani hapo mawazo ni wapi waanzie kula ubweche!!!

Dah utoto raha...imebidi nitafute ukumbusho kidogo!!!!
 

Attachments

  • scan0008 - Copy.jpg
    scan0008 - Copy.jpg
    53.3 KB · Views: 124
  • scan0003 - Copy.jpg
    scan0003 - Copy.jpg
    38.2 KB · Views: 122
ha ha aha nimecheka sana
mimi bana nilikuwa napenda shule uspime!saa kumi na mbili kamili nipo shuleni na hapakuwa mbali na home like 5minutes tuuu, nikifika shule hamna hata mtu nakuta walinzi tuuu, basi next to shule kulikuwa na kanisa soo watu walikuwa wanapita hapo kwenda morning mass kuna mwalimu alikuwa kila siku akipita ananinkuta siku moja akaja home kumweleza mama niwe nachelewa kidogo kwenda shule coz it was not safe kuwa shule muda huo!!!

pia nakumbuka nikiwa std one tukaambiwa inabidi tuweke lable kwenye mashati basi nilivyorudi home mwenyewe nikawa natangaza kuwa kesho tumeambiwiwa tutawekewa 'table' kwenye mashati mama yangu alicheka sana but akaniambia sio table ni lable nilikuja kuelewa baadae sana....

nakumbuka pia mimi nilikuwa monitress and prefect at the same time daaa nilikuwa nakula stiki uspime nisipoandika majina darasani ya wapiga kelele napigwa as moniter and as prefect

nikiwa darasa la nne nikamsema msichana mmoja kuwa anamchumba huyo dada akakasirika akatangaza ngumi bwana weee karibia nijikojolee maana nilikuwa sijawahi kupigana halafu nilikuwa kimbaumbau huyo dada bonge la mtu.ila kwa sababu ya ushabiki nikaenda kwenye ngumi nilichoponea ni kuwa mi nilikuwa narusha ngumi usoni mwisho wa siku yule dada katoka manundu nikatangazwa mshindi ila niliapa sitakuja kupigana tena maana yale manundu ningayapata mimi najua home pasingetosha kwa kichapo
 
nikiwa darasa la nne nikamsema msichana mmoja kuwa anamchumba huyo dada akakasirika akatangaza ngumi bwana weee karibia nijikojolee maana nilikuwa sijawahi kupigana halafu nilikuwa kimbaumbau huyo dada bonge la mtu.ila kwa sababu ya ushabiki nikaenda kwenye ngumi nilichoponea ni kuwa mi nilikuwa narusha ngumi usoni mwisho wa siku yule dada katoka manundu nikatangazwa mshindi ila niliapa sitakuja kupigana tena maana yale manundu ningayapata mimi najua home pasingetosha kwa kichapo

Hahahahahhaha....umenikumbusha...mimi kuna msichana mmoja alikua mkubwa kuliko wote darasani....wakati wengine wote bado tumekaa kitoto toto ye alikua ameshaota maziwa ...hips kule....miguu imechanua!!Alafu alikua sketi anakunja kiunoni ili iwe fupi na shati anafungua vifungo vya juu ili maziwa yaonekane!!!Basi wavulana walikua wanapenda kweli kumchezea na mwenye alikua anachekelea sana!!Sasa bwana siku moja tunatoka shule mtoto mmoja akaniambia kwamba kasikia yule msichana ana mtoto ambae tunajua ni mdogo wake ila tu wanajaribu kuficha na ana bwana mzee!!
Sinikamwadhithia rafiki yangu bwana.....muda ukapita....siku moja sijui aliniomba kitu gani nikamnyima si akaenda kunichongea bwana!!
Heeee mbona nilikoma...nikafatwa ni kigenge...umesemaje??sijui nini na nini....yule msichana akawa anatishia kunishtakia kwa mwl hapo kiroho kinanidunda na yule aliyenipaga umbea alishahama ....ahh nikajifanya ngangari nikwamwambia nenda tuone ntafanywa nini!Mwenyewe akaamua kupotezea tu kwasababu mwl mkuu ..mkuu msaidizi na mwingine mmoja walikua ndugu zangu kwa hiyo akaona watanipendelea tu......ila najua kingefika ningesemwa sana niache umbea!!!Tangu siku hiyo maneno ya she said he said na mimi hatufuatani kabisaaa!!!
 
Hahahaha!Umenifanya nicheke kama mwehu!Eti sita kali au nne moto!

Ndugu, ila na mi kwa utundu nilizidi, nilikua napenda kucheza gwaride hahaa ndo kiongozi, na utamaduni ha haaa kweli tunatoka mbali.
 
nina kovu mkono wangu wa kulia.mwalimu wa hesabu alinijeruhi wakati akinilazimisha kunipa adhabu kwa kutofanya zoezi la siku iliyopita.mi nikawa nakataa coz mwalimu mwenzie alinituma siku hiyo so sikuweza kukusanya kwa wakati,so tukiwa tunagombania fimbo akanizidi na kunichapa nikaumia vibaya kiwiko cha mkono wa kulia.baada ya kupona mwezi mmoja baadae mwalimu alishambuliwa vibaya kwa baruti(kupitia bastola ya mbao ya kuchonga) na mpaka leo nae ana kovu zito juu ya jicho lake la kushoto!mungu nisamehe,lakini ulikua utoto tu bana,afu nae alinionea!wakati wa Issevya Primary School,tabora!
 
Nimesoma posts zote, zimenifurahisha sana, yaani jinsi mnavyokumbukia utoto wenu (enzi za utoto) shuleni, nyumbani n.k.
Mimi nina mengi sana ninayoyakumbuka........nilikuwa na wadogo zangu, tulikuwa tunapenda sana mpira wa miguu, kwa vile tuliishi jirani kabisa na uwanja wa kumbukumbu ya Karume, pale ilala, tulikupenda sana kwenda kuangalia mecchi pale. Baba na Mama hawakupenda kabisaaaa kusikia habari za mpira, hivyo hatukupewa hata SENTI TANO za kiingilio. Matokeo yake tulikuwa tunaruka ukuta, nakumbuka tulikimbizana sana na polisi wenye farasi na mabomu ya machozi yalitutesa sana, maana si sisi tu tuliokuwa tunaruka ukuta. Tukirudi nyumbani sasa..... si unajua kuparamia ukuta ni lazima uchubuke, bakora za baba na makofi ya mama, utakoma.....cha ajabu hatukuacha kwenda mpirani hata siku moja, si ajabu leo hii kukosa mechi pale uhuru stadium au national stadium ni nadra sana (ila siparamii ukuta siku hizi si ulikuwa utoto tu, nimekua nimeacha)

Ila naomba kuwauliza wanaJF wenzangu, malezi au maisha tuliyokuwa nayo wakati ule na hivi sasa tumekuwa wakubwa tuna familia na watoto wetu, Je yamekusaidia? Yaani kwa mfano baba yetu alisisitiza sana elimu na akapigania hadi watoto wake wote (tuko saba), walipata elimu hadi ya vyuo vikuu, alitulea vizuri kiasi kwamba najivunia malezi yake. Pia baba yetu alikuwa mkali sana, kiasi kwamba hata kwa mtoto wa kiume kama mimi nikirudi nyumbani saa 2 usiku naulizwa nilikuwa wapi, nikishindwa kujibu ni kichapo tu! Hii iliendelea hadi nilipoanza kazi nikiwa naishi kwa wazazi (kula kulala). Kwa kweli sijutii malezi yale maana naishi vizuri na watu kila ninapokuwa. Huwa naukumbuka kwa furaha wimbo wa DDC Mlimani Park:
"NAWASHUKURU WAZAZI WANGU WAKATI WOWOTE,
USHAURI WAO UMENILETEA MAFANIKIO MEMA,
SASA NAISHI NA WATU VIZURI......................."
 
Back
Top Bottom