Nimekumbuka zamani!!

Dr Lizzy

Platinum Member
May 25, 2009
30,820
59,406
Nimejikuta nakumbuka enzi zangu za utoto..utundu...ukorofi na uchokozi kwa sana nikaona nishee na kakaz pamoja na dadaz zangu wa JeiEff....bila kukosa zenu!!!

Nakumbuka darasa la tano rafiki yangu L alianza kuandikiana barua za kimapenzi na mvulana mpya shuleni...tena alikua mkubwa kuliko sisi.Tulikua tuna kundi letu sasa ghafla mwenzetu akapunguza kusoma na sisi...kucheza na sisi....kila saa anajifanya kuna kitu anatakiwa kufanya!Siku moja tukiwa darasani tunamsubiria mwl. wa eng. aje mwenzetu akawa kainama kwenye daftari yuko bize kweli....si tulikua dawati la mbele na yeye la pili kwahiyo tukageuka kumuuliza anasoma nini akakataa kutwambia!Tukapanga wawili wabaki pale kumsumbua alafu mimi nimzunguke ili nimnyang'anye lile daftari!Ikawa vuta nikuvute nikatoka na kipande cha karatasi na yeye akabaki na kipande....tukakimbia nje kuongalia tunaona mambo ya nakupenda...sijui nini na nini tukabaki tunacheka!Bahati mbaya mwl akatukuta pale nje akaitaka ile karatasi kwahiyo besti yetu akawa in trouble.Akamaind seme baadae akaja kutuambia asante!!!

Nakumbuka tulikua tunapikiwa uji wa sukari na chumvi ...tunaweka malimao au kupindi cha maembe tunachukua mabichi tunayakataka alafu tunaweka kwenye uji!Makande na ugali wa maharage vilikua vinasindikizwa na maparachichi!!Siku za sherehe wali wa maharage...pilau au ndizi nyama!!

Nakumbuka niliwahi kulipiza kisasi kwa kumsingizia mshkaji mmoja hivi kanipiga baada ya kunichokozoga mpaka nikaogopa kwenda shule kwa siku kadhaa...nikajificha chaka..lolzz....then nilivyorudi mi ndo niliadhibiwa yeye hata hakuguswa!!Basi alicharazwa na adhabu ya kuotesha na kunyeshea maua akapewa!!!

Nakumbuka kuna kipindi iliazuka kwamba baadhi ya wanafunzi wana majini....sijui kama ilikua kweli au walikua wanajifanya tu ila walikua wanazimia....wanaongea mambo ya ajabu ajabu..bila kusahau wakawa wakorofi kweli maana wakiona fimbo tu wanazimia kwahiyo wakawa hawachapwi.

Nakumbuka wavulana walikua wanatuchungulia na vioo tukiwa mstarini....waliotangulia kukua wakawa wanashikwa maziwa...wengine wanachekelea wengine wanamaind.

Nakumbuka tulikua tunashika namba saa 1...usafi mpaka saa 2....break saa 4..lunch saa 6 mpaka 7....alafu class tena mpaka saa 9 alafu tunamalizia kwa usafi.

Nakumbuka tulikua tunatumwa kuni....watu wanakuja na vifagio vyao.

Nakumbuka kuna mtoto mmoja mkorofi kweli alikua anaitwa Gody alirushaga baruti wakati wa mapumziko chuma ikamdondokea mwenzake kichwani akapasuka kidogo.Akakimbia hakuwahi kuja tena shule..mama yake alikua mwalimu wa shule nyingine kwahiyo akampeleka mtoto wake huko.Huko nako akaendelea na uchokozi kama kawa....siku moja wakiwa wanatoka shule akawa anamtoboa toboa msichana mmoja na penseli...yule msichana akampokonya ile penseli akajikuta amemtoboa jicho!Gody akawa chongo kwa uchokozi wake.

Nakumbuka kipindi cha majini mvulana mmoja alichaniwaga kaptula yake na mmoja wa wasichana akiwa amepandisha yake.Hahahaha....mshkaji alibaki wazi nyuma ikabidi aazimwe sweta ajifunike alafu akaruhusiwa kwenda nyumbani.

Nakumbuka nilikua tukitoka shule naingia tuition mpaka saa 12 ndo niende nyumbani.

Nakumbuka siku moja nilipitia kwa rafiki yangu kuangalia tv ....nilivyorudi nyumbani nikasema nilikua nimetumwa na mwl.Ile nimeingia ndani kubadilisha nguo rafiki yangu huyo kaniletea begi langu nlikua nimesahau kwao.....akaulizwa na wewe ulikua umetumwa akajibu hapana,...sasa begi la Lizzy umelipata wapi...akajibu tulikua kwetu tunaangalia tv akasahau.

Nakumbuka kuna rafiki yangu baba yake alijinyonga!Nampitia asubuhi tuongozane nakuta kwao kumejaa watu.....kumbe baba wa watu kajinyonga...tena kisa mapenzi!!

Nakumbuka nilimvunja kaka yangu jino mpaka sasa hivi yuko kama ana mwanya!!!LOLZZZ!

Nakumbuka siku ya mtihani wa darasa la nne mvua ilinyesha radi ikachana mti uliokuwepo nyuma ya darasa letu kwanzia juu mpaka chini!!Bila kusahau picha zetu za kushikilia makompasi.....swagga za enzi hizo.

Ahhhh so many memories..nyingine ngoja niwawekee wajukuu zangu!!!!
 
Nice one, nakumbuka tulikuwa tunacheza sheki rede na kuruka kamba ahhh siku hizi wanafunzi wamebadilika kweli!
 
Nakumbuka nilikuwa nawachokoza sana wasichana nao kwa hasira zao walikuwa wananichania mashati yangu kwa sana tu, nyumbani ni viboko lakini sikukoma, ilibidi wazazi waninunulie fulana nyeupe ili isichanike kiurahisi, na kwa vile nikuwa mtoto wa mwalimu haikuwa shida mimi kuvaa fulana.
 
Ngoja nikalale nikiamka,nitakuwa nakumbuka namimi.........:laugh::laugh:
 
nakumbuka nilipokuwa drs la 5 nilimtorosha msichana mtoto wa mwl mkuu nikampeleka kwene kijimlima cha karibu na shule afu 70% ya wanafunzi wote wakajua wakaanza kuimba "mlimani mlimani mlimani mlimani..."
 
nakumbuka nilipokuwa drs la 5 nilimtorosha msichana mtoto wa mwl mkuu nikampeleka kwene kijimlima cha karibu na shule afu 70% ya wanafunzi wote wakajua wakaanza kuimba "mlimani mlimani mlimani mlimani..."

mkubwa umetisha :car:
 
Tuliosoma shule za kata tuna mengi ya kukumbuka.
Nakumbuka kuna mwanafunzi eti alimkuta mbuzi anasoma gazeti chooni.
Nakumbuka tulipokuwa tunalazimishwa kununua mifagio ya chelewa kama adhabu kwa kuchelewa kuwahi namba.
Nakumbuka nilipokuwa monitress nilikuwa na kibarua kizito cha kuandika majina ya wapiga kelele. Nisipoandika nachapwa mimi, nikiwaandika wakati wa kutoka wananivizia wanipige.
Sitosahau tulipompiga mwalimu na yai viza maana alikuwa mnoko sana.
Yote kwa yote nakumbuka nilikuwa nakaa nyumba ya pili kutoka shule hivyo nilikuwa sipewi hata sh kumi ya kwenda nayo shule.
Jamani mambo ya shule ya msingi....mmmh
 
hahaha...very funny, ulikuwa hauendi shulen na mahindi yaliyokaangwa, yakachemshwa then ukayaweka sukari? halaf marafiki wanakuwa wengi maana umekuja na mahindi.maembe je?

Nimejikuta nakumbuka enzi zangu za utoto..utundu...ukorofi na uchokozi kwa sana nikaona nishee na kakaz pamoja na dadaz zangu wa JeiEff....bila kukosa zenu!!!

Nakumbuka darasa la tano rafiki yangu L alianza kuandikiana barua za kimapenzi na mvulana mpya shuleni...tena alikua mkubwa kuliko sisi.Tulikua tuna kundi letu sasa ghafla mwenzetu akapunguza kusoma na sisi...kucheza na sisi....kila saa anajifanya kuna kitu anatakiwa kufanya!Siku moja tukiwa darasani tunamsubiria mwl. wa eng. aje mwenzetu akawa kainama kwenye daftari yuko bize kweli....si tulikua dawati la mbele na yeye la pili kwahiyo tukageuka kumuuliza anasoma nini akakataa kutwambia!Tukapanga wawili wabaki pale kumsumbua alafu mimi nimzunguke ili nimnyang'anye lile daftari!Ikawa vuta nikuvute nikatoka na kipande cha karatasi na yeye akabaki na kipande....tukakimbia nje kuongalia tunaona mambo ya nakupenda...sijui nini na nini tukabaki tunacheka!Bahati mbaya mwl akatukuta pale nje akaitaka ile karatasi kwahiyo besti yetu akawa in trouble.Akamaind seme baadae akaja kutuambia asante!!!

Nakumbuka tulikua tunapikiwa uji wa sukari na chumvi ...tunaweka malimao au kupindi cha maembe tunachukua mabichi tunayakataka alafu tunaweka kwenye uji!Makande na ugali wa maharage vilikua vinasindikizwa na maparachichi!!Siku za sherehe wali wa maharage...pilau au ndizi nyama!!

Nakumbuka niliwahi kulipiza kisasi kwa kumsingizia mshkaji mmoja hivi kanipiga baada ya kunichokozoga mpaka nikaogopa kwenda shule kwa siku kadhaa...nikajificha chaka..lolzz....then nilivyorudi mi ndo niliadhibiwa yeye hata hakuguswa!!Basi alicharazwa na adhabu ya kuotesha na kunyeshea maua akapewa!!!

Nakumbuka kuna kipindi iliazuka kwamba baadhi ya wanafunzi wana majini....sijui kama ilikua kweli au walikua wanajifanya tu ila walikua wanazimia....wanaongea mambo ya ajabu ajabu..bila kusahau wakawa wakorofi kweli maana wakiona fimbo tu wanazimia kwahiyo wakawa hawachapwi.

Nakumbuka wavulana walikua wanatuchungulia na vioo tukiwa mstarini....waliotangulia kukua wakawa wanashikwa maziwa...wengine wanachekelea wengine wanamaind.

Nakumbuka tulikua tunashika namba saa 1...usafi mpaka saa 2....break saa 4..lunch saa 6 mpaka 7....alafu class tena mpaka saa 9 alafu tunamalizia kwa usafi.

Nakumbuka tulikua tunatumwa kuni....watu wanakuja na vifagio vyao.

Nakumbuka kuna mtoto mmoja mkorofi kweli alikua anaitwa Gody alirushaga baruti wakati wa mapumziko chuma ikamdondokea mwenzake kichwani akapasuka kidogo.Akakimbia hakuwahi kuja tena shule..mama yake alikua mwalimu wa shule nyingine kwahiyo akampeleka mtoto wake huko.Huko nako akaendelea na uchokozi kama kawa....siku moja wakiwa wanatoka shule akawa anamtoboa toboa msichana mmoja na penseli...yule msichana akampokonya ile penseli akajikuta amemtoboa jicho!Gody akawa chongo kwa uchokozi wake.

Nakumbuka kipindi cha majini mvulana mmoja alichaniwaga kaptula yake na mmoja wa wasichana akiwa amepandisha yake.Hahahaha....mshkaji alibaki wazi nyuma ikabidi aazimwe sweta ajifunike alafu akaruhusiwa kwenda nyumbani.

Nakumbuka nilikua tukitoka shule naingia tuition mpaka saa 12 ndo niende nyumbani.

Nakumbuka siku moja nilipitia kwa rafiki yangu kuangalia tv ....nilivyorudi nyumbani nikasema nilikua nimetumwa na mwl.Ile nimeingia ndani kubadilisha nguo rafiki yangu huyo kaniletea begi langu nlikua nimesahau kwao.....akaulizwa na wewe ulikua umetumwa akajibu hapana,...sasa begi la Lizzy umelipata wapi...akajibu tulikua kwetu tunaangalia tv akasahau.

Nakumbuka kuna rafiki yangu baba yake alijinyonga!Nampitia asubuhi tuongozane nakuta kwao kumejaa watu.....kumbe baba wa watu kajinyonga...tena kisa mapenzi!!

Nakumbuka nilimvunja kaka yangu jino mpaka sasa hivi yuko kama ana mwanya!!!LOLZZZ!

Nakumbuka siku ya mtihani wa darasa la nne mvua ilinyesha radi ikachana mti uliokuwepo nyuma ya darasa letu kwanzia juu mpaka chini!!Bila kusahau picha zetu za kushikilia makompasi.....swagga za enzi hizo.

Ahhhh so many memories..nyingine ngoja niwawekee wajukuu zangu!!!!
 
Nakumbuka luxuries za kipindi kile sasa ni vitu vya kawaida....., vitu kama movies, pass time ilikuwa ni kupigiana hadithi na kulikuwa kuna watu walikuwa expert wa kudanganya (Nakumbuka kuna Jamaa mmoja alikuwa anatudanganya balaa..., aliwahi kusema kwamba kwao wana wafanyakazi wazungu, na kila alipokuwa anakuja jumatatu alikuwa anatupa hadithi ya movies kama tatu alizoziangalia)

pia ilibidi tuwe wabunifu kutengeneza toys zetu wenyewe.., mfano gari la wire na matairi ya ndala (malapa)...., mpira wa kusukasuka...., lakini nadhani with all that tuli-enjoy zaidi kuliko watoto wa sasa, we really appreciated things

Nakumbuka kipindi fulani nilipata comics za Tintin karibia shule nzima walikuwa marafiki zangu....:)
 
wewe bado hujaamka tuu:horn:
kweli memories ni nzuri sn unaona heri ungerudia tena halafu uchukue video uje onyesha wajukuu zako,
nakumbuka nilipokuwa std 4 nilijiwa na wadada wawili mmoja kamshika mwenzie mgongni wakanipa kibarua kimekunjwa kama pembe 4 nikawaambia chanini? wao walikuwa wakubwa kidogo kuliko mimi, wakawa wanacheka, nikakirusha kwenye majani, nikaondoka, nilipokuwa kidogo mh! nikawa mwenyeji wa mtaa, lkn ninachoshukuru sikuwa mjinga darasani kwani toka nilipoingia std 1 hadi std saba namba yangu 1 tu nikapata zawadi kibao nikashukuru nikaenda sec, nikafurahi sn,
nakumbuka kulikuwa na mwl mmoja alikuwaanapiga sn wanafunzi kutumia kushoto kwahiyo akawa anaitwa mwl, mashoto, alikuwa anapigwa na wanafunzi wa madarasa ya juu, wakati sis ni std 2&3 tunaona mwalimu akivurumishwa darasani na minjemba ya std 6/7 wakikataa kupigwa
Yaaaaaani nimengi sn sn natamini ningekuwa mtoto leo nirudie video yangu we acha tu.
 
Nice one, nakumbuka tulikuwa tunacheza sheki rede na kuruka kamba ahhh siku hizi wanafunzi wamebadilika kweli!

Yani kulikuaga na msimu wa kila mchezo.....
kuna rede...kuruka kamba....kuna mwingine nimesahau jina ilikua tunachora pembe nne...kila pembe ina duara na mistari inayounganisha zile duara...alafu kati kati nako kuna duara kubwaaa!!!Mtu unatakiwa ukimbie kuzunguka duara ukilengwa na mpira unaingia kati...wakikulenga tena unatoka!!Ukiudaka unaurusha mbali alafu unakimbia kadri ya uwezo wako!!!
Kipindi cha kufuma vitambaa usipokua na silver na uzi wako unajiona sio kabisa....wengine walikua wanachonga vijiti au wanatumia njiti ya kiberiti!!


Kipindi cha stadi za kazi tulijifunzaga kupika mandazi na pilau!!
 
Tuliosoma shule za kata tuna mengi ya kukumbuka.
Nakumbuka kuna mwanafunzi eti alimkuta mbuzi anasoma gazeti chooni.
Nakumbuka tulipokuwa tunalazimishwa kununua mifagio ya chelewa kama adhabu kwa kuchelewa kuwahi namba.
Nakumbuka nilipokuwa monitress nilikuwa na kibarua kizito cha kuandika majina ya wapiga kelele. Nisipoandika nachapwa mimi, nikiwaandika wakati wa kutoka wananivizia wanipige.
Sitosahau tulipompiga mwalimu na yai viza maana alikuwa mnoko sana.
Yote kwa yote nakumbuka nilikuwa nakaa nyumba ya pili kutoka shule hivyo nilikuwa sipewi hata sh kumi ya kwenda nayo shule.
Jamani mambo ya shule ya msingi....mmmh

Hahahhahahah!!!Alafu kabla hujaanza kuandika unawaambia marafiki zako kabisa...nyamazeni naanza kuandika wasumbufu!!Maana wakisumbua alafu usipowaandika wale wanaoandikwa lazima waseme....mwl. hata fulani na fulani walikua wanaongea ila hawajaandikwa!!!
Alafu ukiwa kiranja wa darasa lako mwenyewe unashindwa kuwapangia kazi kwasababu wengi wanakua ni marafiki...mi nlikua navizia wale watoto wengine wanaochelewa sana nawaambia wafagie au nimwambie mwl. walivyochelewa!Lolzzz

Siku ya kufunga shule ndo ilikuaga wavulana wanajificha vichakani....wengine juu ya mti kumvizia ticha mnoko!!!

Mvua ikinyesha kuna watu walikua wanaacha wanyeshewe makusudi ili wasikae darasani....mwl. akimuona mtu maji yanamtiririka anamwambia aende jikoni akakaushe nguo zake!!!
 
Back
Top Bottom