Muuza Viat
JF-Expert Member
- Dec 23, 2022
- 2,865
- 7,473
Mimi hapa muuza viatu nilikua mbishi kwa kuukataa ukwel mchungu kuwa nimefilisika hatimaye nimekubali kuwa nimefirisika biashara zangu zote zimekufa.
Mwaka 2022 soko liliungua kinomanoma na mimi nikiwa miongoni mwa waathirika kutokana na presha kwamba labda tunaweza tukazuiwa kurudi kufanya shughuli zetu ndani ya soko. Tukalazimika kutumia nguvu kubwa kuhakikisha tunarudi na kujenga mabanda kwa haraka kama zali tulifanikiwa lkn kwa upande wangu biashara hazikwenda vizur na kupelekea biashara kusinyaa mdogomdogo. Baada ya kula faida nililazimishwa kula mtaji huku nikijifariji ipo siku mambo yatakua sawa huku nikiendelea kuchukua hatua mbalimbali kama kumwaga sana maji ya upako, kuwaleta wanamaombi na kuendelea kutoa fungu la kumi ingawaje biashara haizalishi faida.
Baada ya kupambana zaidi ya mwaka unusu niliona hapa nalazimika kutia busta labda itakaa sawa. Nilienda bank nikakopa milioni 30 na nikailipia fungu la kumi na mimi mwenyew nilikua sijajinunulia mahitaj kitambo nikajipendelea, nafika home wife ananishangaa mbona yeye sijamkumbuka nae nikampa. Nageuka pembeni nawaona watoto nao wananiangalia hawaongei kitu nao nikawapa nakuja kuangalia salio nimebakiwa na m18 duu! Nikajipa moyo kwa vile ina upako hakuna kitakachoharibika mzee mzima nikaingia mtumbani.
Nilikomaa mpaka Feb mwaka huu kausha damu wa mule sokoni wote walikua wananijua wote niliwakopa na nikashindwa kuwalipa kwa sababu biashara ilishajifia, angalau ule mkopo wa bank ulilipwa kwa pesa ya kodi ya kibanda na kausha damu walishindwa kukitaifisha hiki kibanda kwa sababu wife alishashtukia anguko langu kitambo akabadili jina la umiliki ktk vitu vyangu vingi tu kwa sabab niliwahi kuuza daladala tatu zilikuwa zinapiga ruti ya tandika mwanagati bila kumshirikisha.
Nimekubal nimefirisika kwa sasa natuliza ubongo nadhan mwakan nitaanza tena harakati
Mwaka 2022 soko liliungua kinomanoma na mimi nikiwa miongoni mwa waathirika kutokana na presha kwamba labda tunaweza tukazuiwa kurudi kufanya shughuli zetu ndani ya soko. Tukalazimika kutumia nguvu kubwa kuhakikisha tunarudi na kujenga mabanda kwa haraka kama zali tulifanikiwa lkn kwa upande wangu biashara hazikwenda vizur na kupelekea biashara kusinyaa mdogomdogo. Baada ya kula faida nililazimishwa kula mtaji huku nikijifariji ipo siku mambo yatakua sawa huku nikiendelea kuchukua hatua mbalimbali kama kumwaga sana maji ya upako, kuwaleta wanamaombi na kuendelea kutoa fungu la kumi ingawaje biashara haizalishi faida.
Baada ya kupambana zaidi ya mwaka unusu niliona hapa nalazimika kutia busta labda itakaa sawa. Nilienda bank nikakopa milioni 30 na nikailipia fungu la kumi na mimi mwenyew nilikua sijajinunulia mahitaj kitambo nikajipendelea, nafika home wife ananishangaa mbona yeye sijamkumbuka nae nikampa. Nageuka pembeni nawaona watoto nao wananiangalia hawaongei kitu nao nikawapa nakuja kuangalia salio nimebakiwa na m18 duu! Nikajipa moyo kwa vile ina upako hakuna kitakachoharibika mzee mzima nikaingia mtumbani.
Nilikomaa mpaka Feb mwaka huu kausha damu wa mule sokoni wote walikua wananijua wote niliwakopa na nikashindwa kuwalipa kwa sababu biashara ilishajifia, angalau ule mkopo wa bank ulilipwa kwa pesa ya kodi ya kibanda na kausha damu walishindwa kukitaifisha hiki kibanda kwa sababu wife alishashtukia anguko langu kitambo akabadili jina la umiliki ktk vitu vyangu vingi tu kwa sabab niliwahi kuuza daladala tatu zilikuwa zinapiga ruti ya tandika mwanagati bila kumshirikisha.
Nimekubal nimefirisika kwa sasa natuliza ubongo nadhan mwakan nitaanza tena harakati