Nimekua hasira za karibu kwa wanawake

Nimekua hasira za karibu kwa wanawake

God'sBeliever

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2015
Posts
5,788
Reaction score
3,068
Habari za sasa wanaJF
Bila kupoteza swala la hasira limekua ishu sana kwangu.
Nimevunja urafik mara kibao pale mschana anaponiambia habar za kijinga mfano kuniomba vocha, kutonipigia au kujibu msg yangu kwa wakat, kutokufika, kunipiga kalenda za mbali, kunitizama sana hasa napokua bize na mambo yangu.

Juzi ilikua nimfumue dada mmoja makofi baada ya kunitizama sana ila nilishindwa sababu kulikua na ulinzi wa jeshi.

Mimi napenda nikimwambia kitu mschana akifanye hapo hapo akileta za kuleta kwaheri.
Kuna mmoja ilikua niishi nae nikaona ana mambo ya kitoto nikampiga chini saivi nimeona bora kukaa pekee yangu tuu kuliko kuwa na mahusiano.

Nawaza ntakapooa sijui ndoa itakuaje kama hali hii itaendelea.

Naombeni ushauri plz.
 
Kwanza Huna uvumilivu, pili ukitaka hasira ziishe tafuta anayekufaa funga ndoa kabsa.
 
Hizo ni Tabia za kike ndugu yangu ,Jirekebishe haraka ili uweze kuoa.Wanawake wawili hawawezi kukaliana pamoja pakawa salama .Hope huko kwenye MP so unaweza change
 
***** mleta uzi ni askari uache akili za depo na mahovyo hovyo ya depo mapenzi ni unyenyekevu.Tambua kuwa huyo mpenzi wako sio askari yeye ni raia wewe ndio askari ishi na raia kama raia
 
Habari za sasa wanaJF
Bila kupoteza swala la hasira limekua ishu sana kwangu.
Nimevunja urafik mara kibao pale mschana anaponiambia habar za kijinga mfano kuniomba vocha, kutonipigia au kujibu msg yangu kwa wakat, kutokufika, kunipiga kalenda za mbali, kunitizama sana hasa napokua bize na mambo yangu.

Juzi ilikua nimfumue dada mmoja makofi baada ya kunitizama sana ila nilishindwa sababu kulikua na ulinzi wa jeshi.

Mimi napenda nikimwambia kitu mschana akifanye hapo hapo akileta za kuleta kwaheri.
Kuna mmoja ilikua niishi nae nikaona ana mambo ya kitoto nikampiga chini saivi nimeona bora kukaa pekee yangu tuu kuliko kuwa na mahusiano.

Nawaza ntakapooa sijui ndoa itakuaje kama hali hii itaendelea.

Naombeni ushauri plz.


Huenda ukishaoa pengine hutakaa wiki bila kufungwa maisha jela au kuuliwa na huyo mkeo mtarajiwa kwani hakuna mtu anayependa mwanamme asiyejitambua.
 
Umesema umeamua kukaa peke yako...

Suala la kuoa tena vp


Acha siasa kwenye mahusiano at... Be straight forward aseee
 
wewe ni mura wa kutoka rorya au kiagata?


Kwa hali hio ndugu yangu ukifika 2020 basi uchawi upo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom