Nimekosa mke wa kuoa mpaka leo hii

Nimekosa mke wa kuoa mpaka leo hii

Tatizo lingine linaweza kuwa jinsi unavyojiweka. Perfect wapo ila sio 100 perc. kama utajiweka vizuri basi vizuri vitakuwa vyako. Ila kama unajiweka vibaya vibaya vitakuangukia tu!
 
Usiwe desperate kuingia kwenye mahusiano let alone kukimbilia kuoa.
Inawezekana umeweka vigezo vya juu sana kwa huyo mwenzi unayemtaka au Inawezekana pia una vigezo vya kawaida tu, ila hujampata wa kwako sahihi. Ni kawaida sana, wala usijione kuwa una mkosi, relax kila kitu kitakuwa mwaaaaaah kwa wakati wake

Lingine umesema "Nimejaribu so many girls lakini hawajafanania. ...". Ukiwa desperate sana utajikuta kila siku una mahusiano mapya afu ukikaa naye after few days/months unagundua kuwa huyo sio mtu sahihi kwako na hii pia inachangiwa na wewe kuingia kwenye mahusiano with so much expectations. Na usiwe Unaingia kwenye mahusiano na negativities, utashindwa kuona positive side ya huyo mtu wako as wewe upo busy kuangalia flaws zake. Kila mtu ana mazuri na mapungufu yake, so angalia kama unaweza kuyahimili mapungufu ya mwenzi wako. Kwa muda huu wewe relax tu kwanza, kaa tu single kwa muda na wala usiwaze sana kuhusu mahusiano. Kila kitu kitakuwa poa tu, let things happen naturally, usiforce mahusiano
 
daaah nimecheka sana jamani ila hata mimi role model ni regina.

Umeona eeh, kupata combo ya looks, brains na class ni kugundua mgodi wa almasi. Sugua goti sana Mungu anaweza akakujibu. Otherwise kina Wema sepetu ni ndo wako available
 
Kwani we wahitaji mwenye sifa zipi na hao unaowapata wana sifa zipi?
 
okey sijajua unafanya kazi gani but all in all kama umeamua kuoa ni kheri inabidi ujiandae vizuri. Kabla hujaona hakikisha una
1 nyumba ya kuishi
2 kazi ya kipato
3 akiba
4 heshima na busara
5 elimu
ukishakua navyo ivyo hiyo ni hatua ya kwanza
unatakiwa uwe na mpole kama njiwa utapata yule akupendaye
nb:tabia yako yaweza kukusababishia upate pasua kichwa badili tabia kua kama baba

Namba 1. Sina
2. Kazi ya kipato cha kawaida tu
3.Unazungumzia akiba ipi labda? sijaelewa.
4. ndio nna heshima sana tu.
5. elimu ya kawaida tu ya kupatia mkate wa kila siku.
Ungeongeza 6. Mkokoteni nnao wa kunizungusha kwenye mizunguko yangu.
Hebu nieleze njia gani nitumie nimpate yule ninae match naye?
 
fanya maombi, mwombe mungu utapata wako wa maisha. Usi force kama wadau walivyokushauri, endelea kutafuta na kufanya maombi you will get one.
 
Itakuwa huna nyota ya kuoa......

Endelea kuwa single tu


Maana hakuna binadamu asiyekuwa na mapungufu
 
Ukimchunguza bata......ukipenda au ukimtaka mtu lazima ukubaliane na mapungufu yake, simaanishi mapungufu kama uchangu...lah kuna vitabia vidogo dogo you can learn to live with it.

cc ankol
 
Last edited by a moderator:
Tatizo lingine linaweza kuwa jinsi unavyojiweka. Perfect wapo ila sio 100 perc. kama utajiweka vizuri basi vizuri vitakuwa vyako. Ila kama unajiweka vibaya vibaya vitakuangukia tu!


kama hajakuelewa basi atakuwa na kichwa kigumu.
 
Mchagua nazi hupata koroma. Hao wife material usifikiri wanadondoshwa toka mawinguni. Watu wanavumiliana mpk unawaona hivyo walivyo. Wewe pia wakikuchambua utabaki makapi tu. Uvunilivu tu
 
Back
Top Bottom