Magwangala
JF-Expert Member
- Oct 4, 2011
- 2,981
- 2,359
nadhani tuko wengi sana ingawa sijui TUKO WANGAPI
Wengi sana,mie mmoja wao
nadhani tuko wengi sana ingawa sijui TUKO WANGAPI
Mkuu Amavubi! Miaka yote uwiano haujawahi kuwepo.... Mwaka huu WAKIWA mlikuwa na nafasi kubwa ya kupunguza gap kama sio kuwa na majority bungeni. Ghafla mahaba yaliwaingia mkapoteza DIRA na MVUTO kwa Watanzania wa kawaida ambao ndio wengi. Na hili ni Jeraha zito ambalo matibabu yake ni ya muda mrefu.... Mlikuwa mkionekana kama chama Mbadala cha Kutengeneza Serikali Mbadala mkijigeuza kuwa MAJINUNI waliojitoa FAHAMU baada ya kuzungumza sense na sera zenu zinasimamia nini...Mkaja habari kuwa nyinyi ni majemedari kama MAMVI sio rais BORA hata MCHAGUE JIWE.... Kwenu the most important thing ilikuwa ni MAMVI awe raisi hamkujali Madiwani wa wabunge.... Look here my friends CCM wamenyakua kata 1022 za UDIWANI VS 200+ za CHADEMA........ Wabunge CCM 180+ VS CHADEMA 35 ...... Kweli mlikuwa mnataka Uwiano...Kibaya zaidi Chama chako kiliamua kugeuka mila na desturi za kuamini na kufanyia kazi tafiti za kisayansi na kuanza kuruhusu WAPIGA RAMLI wakubwa kama MZEE WA MISUKULE, na Kile KIBABU MLIKOKITOA CCM wawe majemedari wakuu na kuwapa DIRA..... POLE SANA.... JIPANGENI UPYA !!!
Ni kweli Putin V,kwa jinsi Chadema ilivyokuwa ikiendesha mambo yake kwa kushikilia Sera ya kuupinga ufisadi kwa nguvu zote,viongozi wakweli ambao hata ukiwaona usoni unajua huyu anazungumzia vitu vyenye logic,mvuto ushawishi na hamasa kubwa,uwezo wa kujenga hoja kuichambua na kuifafanua kwa kina,hakika ni chama ambacho kilikuwa kikifuatiliwa na watu wa rika karibu zote.Walikuwepo viongozi ambao hata serikali ilikuwa ikifuatilia kauli zao kimya kimya,watu waliaminishwa kuwa fulani,fulani na fulani ni wahalifu wa Ufisadi Mkubwa kabisa nchini tena kwa kutamkwa hadharani bila kumumunya maneno na kwamba anayeona kachafuliwa aende mahakamani akalalamike.Waliotajwa hakuna hata mmoja aliyejitokeza kwenda mahakamani kuomba asafishwe,jambo ambalo liliwapa Imani kubwa wananchi kwa viongozi hao wa Chadema,wakati chama tawala kikimtafuta na kumtangaza mgombea wao Chadema walikuwa wamejifungia vyumbani huku wakisikiliza nani Anakatwa huku wakiwa na matumaini tele juu ya huyo waliyemchafua kwa miaka tele,na kusahau kujiimarisha kimtandao hadi ngazi ya chini kabisa waliko wapiga kura wengi,gea zimebadilishwa Angani na Falsafa sahihi za Ufisadi ukawa ni Msamiati usiokuwemo tena ktk Misahafu ya Chadema na akili yote ikawa ni Kukamata Dola mengine baadaye,poleni kwa yote,Kampeni Uchaguzi umepita na Kiongozi Mkuu wa nchi ameshachaguliwa na kuapishwa,mengine yote baada ya hapo hayana Tija kwa mama yetu Tanzania zaidi ya kufanya kazi kwa bidii tena kwa Kukimbia mchaka mchaka maana tumechelewa mno wenzetu wako mbali.
Bado siamini kama ni mimi ambaye nilikua karibu ya kuugua ninapokosa kipindi cha Bunge pindipo nina fursa hamu imekwisha kabisa naona mauzauza tu na nimekata tamaa sana nahitaji kuhuishwa upya.
nadhani tuko wengi sana ingawa sijui TUKO WANGAPI
teh teh teh teh asante kwa kuniongezea sikuuwepo wa nepi ndio umenifanya nisitake kufatilia bunge hili