Bwaga ya moyoni
Senior Member
- Aug 21, 2012
- 147
- 76
Inamaana umekosa Mwislam mwenzako ukafunge naye ndoa huko msikitini? Kwa mwenye imani ya kweli hicho unachokitaka ni kitu kigumu sana na kimsingi, hakuna mtu serious kiimani (awe mzazi au yeye mwenyewe) binti atakayekubali kiukweli. Tazama upande wa pili utaona kuwa kwa misingi ya dini ya kiislam, ndoa kati ya mwislam na asiye mwislam iliyofunga bomani ni uzinzi. Sasa rudi ujiulize, je, hiyo ndoa yenu itafungwa wapi? Je, kama huyo binti atakubari ndoa yake ikafungwe msikitini, atakuwa ameiamini imani yake mpaka akaamua kuwa sehemu ya hiyo imani kweli au atakuwa amependa ndoa tu na akaendelea kukupigia kwaya ndani mpaka wewe mwenyewe na ndugu zako wote wataanza kuchukia muda si mrefu? Msingi wa ndoa ni imani. Yeye amekulia ktk mazingira yakuamini kuwa ndoa ni mke mmoja na mume mmoja, je, ikija baadaye mapenzi yakapungua kati yenu na ukataka kuoa mke wa pili, je yeye atakuwa tayari? Dont be blinded na mapenzi ya leo. Fikiria hata baada ya miaka kumi mkiwa pamoja.
Waungwana nisaidieni, nimekataliwa kuoa kisa mimi mwislam, wakwe wanasema sifa zooote ninazo ila dini yangu eti sisi wengi wetu ni magaidi, bibie yeye yuko radhi tufunge ndoa bila ridhaa ya wazazi ila mimi naona haiwezekani hususan kwa tuhuma hii ya kidini, sasa wanajamii mnanishauri nini na upande wa dini je inaswihi ndoa ya ilofungwa bila ridhaa ya wazazi,, habari hii si ya kubuni hivyo naomba muelewe hivyo