Nimekata tamaa ya maisha

Lakini madam hii mimba ya miezi 8 ni toka mwaka jana August inakuwaje inabaki hivyo hujazaa? Kuna uzi wako uliweka August ukasema una mimba ya miezi 8
Labda mimba imejirudia emu tuone huo uzi
 
Nimepitia nyuzi zake za nyuma, tatizo linaanzia kwake sio kwa mumewe.
Pesa na shughuli ya kufanya sidhani kama ni shida kwake ila mbongo kidogo ina hitilafu.
Sawa sawa mkuu. Nimeona. Tatizo lipo
 
Lakini madam hii mimba ya miezi 8 ni toka mwaka jana October inakuwaje inabaki hivyo hujazaa? Kuna uzi wako uliweka August ukasema una mimba ya miezi 8
Ata ingekuwa wewe ungeendelea kukua huko tumboni uzaliwe kama muhusika mwenyewe anataka kujidedisha?
 
pole sana, na hiyo hali uliyonayo sasa ndio tafran zinazidi mara 4!
jikaze ,omba sana Mungu akupe uvumilivu.. ..yatapita tu.. ..kuna wengine tu naishi motoni kabisa lkn bado hiyo si sababu ya kujiakatia tamaa na kujidhuru.. .. ukaacha watoto wanateseka ...
Kama una ndugu wa karibu nenda ukajihifadhi kwa mda au kamshtaki huyo dhalim...
 
Kuna member anaitwa Mpauko
Huyu anaweza kujiua kweli kama yule member mpauko.
 
Unataka kujiondoa,we si ulichukua cheti na ukala kiapo na wali ukala na ukaahidi utavumilia mpaka kifo kiwatenganishe,sasa nini tena unataka kukatisha safari yako ya maisha kabla mwenyewe mtoa uhai hajakuruhusu...?
 
Mazingira uliyopo na watu wanaokuzunguka ndo ninavyokufanya uone kama dunia imekulemea peke ako. Watu wengi wanapitia hali yako, jaribu kuvumilia na kubadilisha pattern za siku yako na utaondoka kwenye hilo wingu jeusi soon...nakusubiri baada ya wiki mbili utakavyosaidia wengine wanaopitia unayopitia...see you soon here
 

Mume yupo wapi? Anatesa Tabia au Hana uwezo wa kulea watoto? Funguka,
 
Kujiua sio solution.

Kujiua nikuongeza matatizo zaidi kwa wanao.

Bora ubaki hai upambane mpaka tone la mwisho.

Shida zitapita.
 
Yani kinachokutesa ni huna hela? Au msiba, magonjwa, ndoa, watoto na mimba?
Kama ni hela basi unahaki ya kulalamika na kuonewa huruma ila hayo mengine ndo maisha sasa usiyafikirie sana ikiwa utapata solution ya kiuchumi.

#PUSH HARDER
 
Becky hujambo? Sijakuona mda my favourite lady.
Ushauri mzuri!
 
Usikate tamaa,hebu nyoosha maelezo nyumbani hapo ni kwa nani? umeolewa au vipi,tupe maelezo ya kutosha ili watu wakusaidie
 
Mimi mwenyewe nakata tamaa aisee, Mungu anajua
 

Kumbe yeye mwenyewe ndiyo shida. Hapo lazima mwanaume akimbie tu.
 
Pole mama K, ni majira tu yatapita......utajifungua, utapakata mwanao mzuri....atatabasamu na utafurahi.
Utasahau yote niamini....njoo pm please.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…