Nimejaa hofu kwa nilichokishuhudia kwa mpenzi wangu

Umenivunja mbavu, kafungwa mpaka mapumbu, huyu kaja kuomba ushauri huku, amefungwa kweli, mi ningechoma halafu nikaa kimya tu kiaiana
Najua sijafungwa wala nini,na hapa nilikuja sio kuomba ushauri wa nini cha kufanya,la hasha,nilikuja ili nisaidiwe kupata tafsiri ya maandishi hayo hapo juu,kwani lugha iliyoandikwa siielewi hata kidogo,kwa hiyo ukirudia kusoma maelezo yangu itakuwa vizuri zaidi ili utoe mchango wako wa kutafsiri hiyo lugha!!!
 
Najua sijafungwa wala nini,na hapa nilikuja sio kuomba ushauri wa nini cha kufanya,la hasha,nilikuja ili nisaidiwe kupata tafsiri ya maandishi hayo hapo juu,kwani lugha iliyoandikwa siielewi hata kidogo,kwa hiyo ukirudia kusoma maelezo yangu itakuwa vizuri zaidi ili utoe mchango wako wa kutafsiri hiyo lugha!!!

Huna haja ya kujua hiyo tafsiri, na mtu aliyefungwa hajui kama kafungwa, wewe choma huo ujinga full stop... kama wataka kujua tafsiri piga picha wacha kwenye simu, ila hayo yachome
 
Ukijaa hofu atakushinda, omba Mungu kwa imani yako, hatakufanya chochote. Then achana nae, inawezekana unampenda kwa sababu ya nguvu flani
 
Najua sijafungwa wala nini,na hapa nilikuja sio kuomba ushauri wa nini cha kufanya,la hasha,nilikuja ili nisaidiwe kupata tafsiri ya maandishi hayo hapo juu,kwani lugha iliyoandikwa siielewi hata kidogo,kwa hiyo ukirudia kusoma maelezo yangu itakuwa vizuri zaidi ili utoe mchango wako wa kutafsiri hiyo lugha!!!
usipanic mkuu.kufungwa huko unadhani utapaona kwa macho? unajua huko alikoenda kabla ya kuja na huo uchafu alifanya kafara gani? yaani unatakiwa ukae nae ukute hata umefukiwa makaburini.mwnamke mshirikina nionavo mimi hafai kabisa maana ni muharibifu.
 
Huna haja ya kujua hiyo tafsiri, na mtu aliyefungwa hajui kama kafungwa, wewe choma huo ujinga full stop... kama wataka kujua tafsiri piga picha wacha kwenye simu, ila hayo yachome
naona kapanic anadhani kufungwa hadi afungwe minyororo aione.ngoja kafara lianze kujibu ndo atajua kama kafungwa au vipi.
 
Ameamua kulinda kitu chake, sio kila jini ni baya kwa maisha ya wanadamu mengine ni neema,
 
Hahahaaa!!!sasa si ni jambo la kuzungumza tu,halihitaji njia nyeusi kama hizi,matokeo yake ndo kila kitu kimeharibika,analazimika kuanza mahusiano upya na mtu mpya,wakati huo huo amenirudiaha nyuma hatua nyingi sana katika swala zima la mahusiano,kwa sababu;
1.Nalazimika kutafuta mwanamke mwingine kwa ajili ya kutengeneza maisha.

2.Hata huyo ntakaye kuwa naye,anaweza kujikuta ktk wakati mgumu kwa sababu imani yangu itakuwa ndogo sana kwake,kutokana na jambo hili,(nilimuamini sana,hivyo moyo wangu utakuwa mzito sana kuamini mwanamke kwa namna yoyote)
Chief mara nyingi watu tunaofanya nao maisha kuna vitu wanavikosa kutokana na maumivu tuliyopata katika hatua za awali za mauhusiano,hui sio kwako huenda hata huyo utaempata nae kuna vitu atakuwa kapitia.Hivyo kumfanya kwako awe nusu nusu lakini kusahau kupo wote mtajiona ni wapya!
 
Mkuu msaada wangu hapo ni kujikausha.. Then unakurupuka kama umepanda mashetani vile..! Unasema sema maneno ya ajabu ajabu yasioeleweka.. Then unamgeukia huyo demu! Unampiga mikwara ya kutisha ukijifanya mashetani yako yamestukia uchawi wake..! Then shetani anasema atoe vitu vyote kwenye mkoba..!
Akitoa na madude yake unamkazia kuwa leo umemsamehe ila akirudia tena kutaka kumchezea kiti ATAKIONA CHA MTEMA KUNI!
Nakwambia harudii tena huyo!
Umetisha mkuu. Huo ushauri wako ni wa level za PhD.
 
naona kapanic anadhani kufungwa hadi afungwe minyororo aione.ngoja kafara lianze kujibu ndo atajua kama kafungwa au vipi.
Miss natafuta hapo sasa unaninyong'onyeza bhana,unataka kuniambia ndo tayari nshawekwa kwenye chupa kama Dr.ken??
Hakika sikubali,na katu Mungu wangu hawezi kuruhusu hilo litokee kwa mtoto aliyeniumba kwa mfano wake!!!hakika naamini ktk maandiko,tumepewa mamlaka ya kukanyaga nge na nyoka nao hawatatudhuru!!!
 
Miss natafuta hapo sasa unaninyong'onyeza bhana,unataka kuniambia ndo tayari nshawekwa kwenye chupa kama Dr.ken??
Hakika sikubali,na katu Mungu wangu hawezi kuruhusu hilo litokee kwa mtoto aliyeniumba kwa mfano wake!!!hakika naamini ktk maandiko,tumepewa mamlaka ya kukanyaga nge na nyoka nao hawatatudhuru!!!
kwa vile umeona halitakupata tena .assume usingeona .kwani wanaologwa Mungu hawaoni mkuu? Mungu si wetu sote? hawajaumbwa kwa mfano wake.huyo dada sio mtu mzuri inaonesha akija kupata tu dhoruba kidogo atakuendea kwa mganga ndo maisha yake hayo .muache tu kwa amani usije kulogwa tena mazima
 
kwa vile umeona halitakupata tena .assume usingeona .kwani wanaologwa Mungu hawaoni mkuu? Mungu si wetu sote? hawajaumbwa kwa mfano wake.huyo dada sio mtu mzuri inaonesha akija kupata tu dhoruba kidogo atakuendea kwa mganga ndo maisha yake hayo .muache tu kwa amani usije kulogwa tena mazima
Hapo umenena vema,hasa ushauri wako hapo mwisho,nimeupenda!!!maana umeona mbali!!nitaufanyia kazi ushauri wako,kikamilifu!!!
 
Lugha ya Kichawwi siyo Lugha sawa na Kibinandamu.. Ndiyo Mana unakuta Mtu wako Uchi Mahospitalini lakini hakuna anayejua kama kuna watu waliopo Uchi mahopitalini wanatembea mpaka uwe na macho ambayo yapo kati Dunia yao. Hakuna Lugha ya Kiganga ambayo inaweza tafsiriwa na kila Mtu kama ingekuwa hivyo basi wote wangekuwa ni waganga.
Hivi kuna watu hadi leo mnaamini hizo story za shigongo!
Eti watu wapo uchi mahospitalini hatuwaoni duh..

Waganga ni matapeli tu kama matapeli wengine, walikuepo kina manyau nyau wakadanganya watu wanatoa majini/uchawi wanakunywa dam sijui za paka leo hii katulia zake anabadili magari tu na mijengo ya maana
 
Back
Top Bottom