Nilikuwa Dar Es Salaam kwa muda wa week moja, nilikaa Atriums Hotel na nikaibiwa night ya nne, niliibiwa chumbani usiku wa saa 3 wakati nikiwa restaurant nakula hapo hapo hotelini... Niliibiwa digital camera 2, na simu aina ya HTC, na pesa taslim usd 2300.., mbaya zaidi mmiliki wa hotel anaitwa Erik Shingongo alifika hapo hotelin baada ya kupigiwa sim na meneja wake ndugu Sunday nilieripoti wizi huo muda huo huo. Shigongo aliniambia kuwa anawajua wezi nimpe muda wa saa 3 atarudisha vitu vyangu, baada ya masaa 3 kupita alikuja tena akiwa na maaskari 3 toka kituo cha polis kijitonyama na wakanitaka kutoa maelezo., na wakati huo, ikiwa saa 7 usiku shigongo aliniambia kuwa tayari kesha washika wezi wanne ambao ni wafanyakazi wa hotelini hapo HIVYO nitulie nitapata mali zangu.Nimesubiri bila mafanikio, nikapewa maelekezo ya kumwona RCO wa osterbay, kamanda Wambura ambae alitoa maagizo ya kuwepo mkutano kati yangu na shigongo na meneja wake bwana sunday, mkutano ufanyike ofisin kwa rco ili tuweze kukubaliana namna ya kurudisha vitu nilivyoibiwa. Shigongo hakutokea, meneja wake alifika na akiwa amepewa na maagizo na Shigongo kuwa msimamo wa hotel ni kutolipa au kutoa fidia ya aina yeyote, kuwa wao kama hotel wanaona ilikuwa ni kosa langu kwenda hotelin ATRIUMS. na pia alisema hakuna wa kumfanya lolote Tanzania hii hata nikiripoti kwa RPC, RCO akaridhia na akaniambia hana la kufanya na sheria haimpi nafasi ya kumbana shigongo.
hiyo ndo ilikuwa final na kesi ikafungwa, Tanzania ya watanzania raia hana haki, hadi polis wanaubariki wizi na kuutetea, pale ATRIUMS ni kichaka cha kufuga wezi, mwizi namba moja akiwa Erik Shigongo. namba 2 meneja wake na namba 3 team yake ya wafanyakazi, Kuweni makini msiumie kama mimi.