gwa myetu
JF-Expert Member
- Aug 18, 2014
- 4,473
- 4,671
kwa huruma kama hii itabidi hata majambazi, wabakaji na waovu wengine kwenye jamii tuwahurumie na tusiwachukulie hatua stahiki.
Mi naamini mashoga wengi wamejitakia na hata kama mtu kazaliwa hivyo au kaharibiwa, ya nini kuikubali hali na kujitangaza kwenye jamii na kujivika mavazi ya kike?
Ni kwavile jamii imewapa suport na kuvifanya hivi vitendo viovu ni vya kawaida ndomana wamepata ujasiri huo.
Tungewatenga wangebadilika, mtu ambae angejihisi anatabia hizo angetumia kila namna kama madawa, maombi na njia nyinginezo ili awe kawaida.
Na hata kama ingeshindikana kurudi katika hali ya kawaida, asinge thubutu kujitangaza na kujifakharisha mitaani.
Unapoiona dhambi ni ya kawaida unakuwa umejihalalishia kuendelea kuifanya na unawavutia watu wengine.
NB: suala la kumvusha mtoto wa kiume sio tatizo kama wewe mwenyewe utakuwa mchamungu na ukamlea mwanao ktk mazingira hayo.
Kama wazazi ni wachamungu na mnajitambua ni rahisi sana watoto kuiga na kuwa ktk maadili mazuri.
Hivi hujawahi sikia watoto wanaolawitiwa kanisani au madrasa kimyakimya ukishtuka ameshakuwa shoga? Hakuna sehemu salama