Nimegundua utajiri upo shambani

Nimegundua utajiri upo shambani

Embu ingia kwanza shambani halafu ndipo Uje na thiredi ingine.
Huku kijiji cha matobole debe la mahindi ni buku 2 tuu
 
Umechunguza ukajua hawa mama ntilie wanaingisza shingapi kibindoni?
Unajua faiada ya mchoma mahindi pale stend, chuoni au shuleni?
Umejiuliza wale wanaoza mandazi, keki, bagia, sambusa, chapatti n.k shuleni wanaingiza shingapi?
Mkuu fanya deep analysis ndipo uje utoe kauli hapa?
Watu tumejiridhisha ndio maana tunataka tujitoe kwenye utumwa wa ajira za kusubiri miaka na miaka.
njoo tuungane boss
 
Siwezi jilaumu kwanini nilisoma kwani elimu inafaida yake kubwa sana.
Baada ya kusoma sasaa nataka nitumie ujuzi wangu huu kujipatia kipato halali.
Nimeamua kwenda shamba kulima na kufuga ngombe na kuku.
Baadhi ya mazao ya shamba kama mahindi, mboga, maharagwe, matunda(Maembe, machungwa, matikiti, ndizi, nanasi n.k) nitauza mengine ntatumia mgahawani kwangu kuuza kama chakula (Nimegundua biashara ya chakula inalipa sana hasa ukiwa na wateja wa kuaminika kulingana na eneo ulilopo kama vyuoni, eneo lenye wapiti njia biashara nyingi).
-Mahindi ya kuchoma uanalipa.
-Chipsi zinalipa.
-Wali, ugali, vitafunwa vya hasubuhi kama mandazi na chapatti vinalipa.

Fiada za kuku na ngombe.
-Mimi nataka ngombe watatu au wane hawa wanatosha kunipa maziwa ya kutosha nikawa nauza mgahawani kama chai au maziwa mgando.
-Kuku kama 200 wanatosha kwaajili ya mayai tuu yakuuza.
-Mbalea itokayo kwa kuku na ngombe nitaitumia kupandia bustani za mboga na mazao mengine.


Faida za shamba
-Unakuwa huru! Hakuna wakukupelekesha wala kuwa kibaraka wa Fulani.
-Unaweza fanya kazi nyingi Zaidi hivyo kukuongezea kipatao chako kuliko kuajiriwa ambapo unapaswa uweo ofisini muda wote.
-Unakuwa na muda mwingi wa kufanya mambo yako kwa Amani.
-Hakuna makato yani pesa unayoipata ndio inayoingia mfukoni moja kwa moja.

Plan
-Kutafuta eneo lenye shughuli nyingi za watu hao watu ni mtaji wangu.
-Inategemea naweza nunua uwanja nijenge mgahawa au nikodishe mgahawa.
-Kujifunza kupika vyakula vitamu ili niteke soko plus chakula cha kutosha ili nipate raia wengi. Hii ni faida kisoko kwa sababu unapotoa huduma nzuri ndipo watu wanavutiwa kuja.
-Kodi ya mgahawa nitajipanga siku zote mwanzo ni mgumu.


NB: Bye bye kutembeza bahasha... naweza pata pesa nyingi namna hii Zaidi ya laki nane kwa mwezi hapo bado makato ya HESLB, sijui wapo huko mwishowe take home inakaribia kali tano kwa siku 30 hapo sijala, sijalipia kodi ya nyuba, usafiri, sijaumwa, sijanunua vocha, sijasaidia ndugu kwa laki 5 hapo ni kudanganyana.
Inapendeza kufikiri nje ya boki. Huku ndiko kujiajiri japo watu wengi hudharau sana wasomi sasa mimi nataka ni wa prove wrong.
Pole sana
 
Kilimo kinahitaji mtaji mkubwa mno. Sio kulima lima tu
Kama mnataka mali mtayapata Shambani.Nafikiri walimu wetu shule za msingi hawakulitendea haki shairi hili.wangelivaa na kutuvalisha tungependa kilimo wengi
 
Kilimo kitakupa kula tuu na kubadilisha mboga, hutalala njaa...utajiri sahau
 
Hivi tajiri ambae ni mkulima tu ni nani hapa TZ.Watu wenye pesa ni wafanya biashara sio wakulima.Wakulima ni watu wa kuliwa tu.Ukumbuke kutupa mrejesho maana mvua ndio zinaanza hivi.Karibu kigoma kuna mvua ma mapori ya uhakika.
 
Ng'ombe wa 4 mmh!
Ulishawahi fuga kabla?

Kuku 200!!

Anyway nisikukatishe tamaa sana ila hivyo vitu ulivyoandika nadharia ni 98% uhalisia 2%
 
Ni kweli, inapendeza umetulia shambani kwako, mazao yamestawi vizuri, una afya nzuri, hauna madeni.......yani ile life hauko kwenye rat race.

Tatizo la mazao ya kilimo bei yake hubadilika haraka sana. Leo bei imepanda mara 2 baada ya miezi michache bei inashuka zaidi ya mara 4.

Hii inaathiri sana faida mkulima anayotarajia.

Mara nyingi huwa ni hasara tu.

Nimeona baadhi ya wakulima wanalima kwa contracts. Mtu au kampuni fulani inahitaji kiasi kadhaa cha kitunguu unaingia shambani kupiga mzigo.

Labda kulima hivi ni vigumu? Wakulima hawajazoea/hawaoni kama inawezekana?

Nadhani kuwekeza kwenye Kilimo ieleweke kwa namna hii. Kiasi fulani inampa mkulima uhakika kuwekeza nguvu, fedha na muda.

Kama unajilimia shamba dogo tu kwaajili ya vijisenti vichache sawa, unaamua unavyoona inafaa.
 
Ni kweli, inapendeza umetulia shambani kwako, mazao yamestawi vizuri, una afya nzuri, hauna madeni.......yani ile life hauko kwenye rat race.

Tatizo la mazao ya kilimo bei yake hubadilika haraka sana. Leo bei imepanda mara 2 baada ya miezi michache bei inashuka zaidi ya mara 4.

Hii inaathiri sana faida mkulima anayotarajia.

Mara nyingi huwa ni hasara tu.

Nimeona baadhi ya wakulima wanalima kwa contracts. Mtu au kampuni fulani inahitaji kiasi kadhaa cha kitunguu unaingia shambani kupiga mzigo.

Labda kulima hivi ni vigumu? Wakulima hawajazoea/hawaoni kama inawezekana?

Nadhani kuwekeza kwenye Kilimo ieleweke kwa namna hii. Kiasi fulani inampa mkulima uhakika kuwekeza nguvu, fedha na muda.

Kama unajilimia shamba dogo tu kwaajili ya vijisenti vichache sawa, unaamua unavyoona inafaa.
Sasa mkuu kabla ya kuingia shamba inakupasa ufanye research za masoko almost yote na nje ya mkoa.
Kabla ya kuingia shamba kuna vitu unapaswa kuvichunguza kwanza kama soko, ardhi, maji, usalama n.k ni somo refu linalohiaji uzi wake special
 
Back
Top Bottom