Nimegundua utajiri upo shambani

Nimegundua utajiri upo shambani

Hongera bt tafuta mahali penye uhakika wa maji, mvua. It takes time. Na inataka uvumilivu. Angalia isiwe nadharia.
 
Aisee?!
Halafu waTZ wengi hawajui kula mbaazi sijui kwanini!
Mbaazi na jamii ya mikunde zinafaida nyingi kula kuliko nyama!
Yani Hivi msimu wa mbaazi mbichi unavyoishia nanunua kiloba kizima tunachambua nyumbani usiku na mchana kisha tunaweka Kwenye vikontena tunaweka Kwenye deep freezer tutakuwa tunatumia Kwa miezi hadi 3 !
Wenzetu wazungu ukiwaona wananunua nyama ni Kwaajili ya wageni maana wanajua wabongo tunapenda kula nyama!
Wao ukienda jikoni kwao utakuta vikopo vya maharagwe, kunde, choroko, mbaazi, njegere, njugu mawe n.k
Sana sana labda Kuku na Samaki!
Nnahisi labda wengi wetu hatujazoeshwa toka udogoni
 
Utajiri upo kwenye ufugaji na kilimo ila unahitaji nguvu kazi ya kujitolea kwa muda Fulani kabla ya kuanza kupata faida. Ndio maana wafugaji wengi wenye mifugo mingi huoa wake wengi kutafuta nguvu kazi. Tafuta eneo linalostawisha migomba ,pata ekari mbili tu ,komaa hapo utakuwa tajiri
 
Utajiri upo kwenye ufugaji na kilimo ila unahitaji nguvu kazi ya kujitolea kwa muda Fulani kabla ya kuanza kupata faida. Ndio maana wafugaji wengi wenye mifugo mingi huoa wake wengi kutafuta nguvu kazi. Tafuta eneo linalostawisha migomba ,pata ekari mbili tu ,komaa hapo utakuwa tajiri

Wafugaji nao Siku hizi wamekata tama kabisa wanasema hawajapangiwa maeneo ya malisho!
Nikikutana na wamasai flani Handeni ukiwasikiliza vizuri utagundua kuwa wanahoja ya msingi!
Kifupi ni kuwa kusipokuwepo na mpango mkakati Juu ya maswala Haya baada ya miaka michache ijayo matokeo yanaonekana Kwa bei ya kitoweo cha nyama na maziwa kupanda bei maradufu kutoka na uhaba ktk kupatikana kwake!
Mark my words !
 
Utajiri upo kwenye ufugaji na kilimo ila unahitaji nguvu kazi ya kujitolea kwa muda Fulani kabla ya kuanza kupata faida. Ndio maana wafugaji wengi wenye mifugo mingi huoa wake wengi kutafuta nguvu kazi. Tafuta eneo linalostawisha migomba ,pata ekari mbili tu ,komaa hapo utakuwa tajiri

Mkuu hii nimeipenda hebu nisaidie kwa ufafanuzi zaidi nijaribu na mini
 
Mkuu hii nimeipenda hebu nisaidie kwa ufafanuzi zaidi nijaribu na mini
Kuna mkulima yupo kijijini kwetu analima migomba ana ekari mbili tu . Kwa wiki -yeye anauza ndizi kila jumapili-hakosi laki sita hadi nane.ila ni uwekezaji unaohitaji uvumilivu wakati unasubiri kukomaa. Hivyo tafuta eneo ambalo ardhi yake inaweza himili hicho kilimo.Maeneo niayoyajua yanakubali ndizi ni kasulu kigoma,sehemu kubwa ya mkoa wa Mbeya,tarime mara,moshi Kilimanjaro ,sehemu kubwa ya mkoa wa kagera
 
Siwezi jilaumu kwanini nilisoma kwani elimu inafaida yake kubwa sana.
Baada ya kusoma sasaa nataka nitumie ujuzi wangu huu kujipatia kipato halali.
Nimeamua kwenda shamba kulima na kufuga ngombe na kuku.
Baadhi ya mazao ya shamba kama mahindi, mboga, maharagwe, matunda(Maembe, machungwa, matikiti, ndizi, nanasi n.k) nitauza mengine ntatumia mgahawani kwangu kuuza kama chakula (Nimegundua biashara ya chakula inalipa sana hasa ukiwa na wateja wa kuaminika kulingana na eneo ulilopo kama vyuoni, eneo lenye wapiti njia biashara nyingi).
-Mahindi ya kuchoma uanalipa.
-Chipsi zinalipa.
-Wali, ugali, vitafunwa vya hasubuhi kama mandazi na chapatti vinalipa.

Fiada za kuku na ngombe.
-Mimi nataka ngombe watatu au wane hawa wanatosha kunipa maziwa ya kutosha nikawa nauza mgahawani kama chai au maziwa mgando.
-Kuku kama 200 wanatosha kwaajili ya mayai tuu yakuuza.
-Mbalea itokayo kwa kuku na ngombe nitaitumia kupandia bustani za mboga na mazao mengine.


Faida za shamba
-Unakuwa huru! Hakuna wakukupelekesha wala kuwa kibaraka wa Fulani.
-Unaweza fanya kazi nyingi Zaidi hivyo kukuongezea kipatao chako kuliko kuajiriwa ambapo unapaswa uweo ofisini muda wote.
-Unakuwa na muda mwingi wa kufanya mambo yako kwa Amani.
-Hakuna makato yani pesa unayoipata ndio inayoingia mfukoni moja kwa moja.

Plan
-Kutafuta eneo lenye shughuli nyingi za watu hao watu ni mtaji wangu.
-Inategemea naweza nunua uwanja nijenge mgahawa au nikodishe mgahawa.
-Kujifunza kupika vyakula vitamu ili niteke soko plus chakula cha kutosha ili nipate raia wengi. Hii ni faida kisoko kwa sababu unapotoa huduma nzuri ndipo watu wanavutiwa kuja.
-Kodi ya mgahawa nitajipanga siku zote mwanzo ni mgumu.


NB: Bye bye kutembeza bahasha... naweza pata pesa nyingi namna hii Zaidi ya laki nane kwa mwezi hapo bado makato ya HESLB, sijui wapo huko mwishowe take home inakaribia kali tano kwa siku 30 hapo sijala, sijalipia kodi ya nyuba, usafiri, sijaumwa, sijanunua vocha, sijasaidia ndugu kwa laki 5 hapo ni kudanganyana.
Inapendeza kufikiri nje ya boki. Huku ndiko kujiajiri japo watu wengi hudharau sana wasomi sasa mimi nataka ni wa prove wrong.
Ha ha ha poa mkuukaribu huku tuliko ndo utajua Kilimo kinahitaji moyo. Utalima peke yako, pembejeo peke yako , ukishaivisha inakuwa si mali yako tena. Leo utasikia usiuze mahindi mabichi, mara ni marufuku kuuza mazao nje ya nchi na wakati mwingine huruhusiwi kuuza nje ya Wilaya au Mkoa. Ukienda kuuza utakutana na mtu anaitwa dalali, huyu dalali atataka apate faida mara mbili au tatu ya bei anayokupa. Ukitoa gharama za uzalishaji na usafirishaji unabaki huna kitu, unaweza hata kujinyonga. Usije huku na matumaini makubwa utakufa muda si wako,
 
Umechunguza ukajua hawa mama ntilie wanaingisza shingapi kibindoni?
Unajua faiada ya mchoma mahindi pale stend, chuoni au shuleni?
Umejiuliza wale wanaoza mandazi, keki, bagia, sambusa, chapatti n.k shuleni wanaingiza shingapi?
Mkuu fanya deep analysis ndipo uje utoe kauli hapa?
Watu tumejiridhisha ndio maana tunataka tujitoe kwenye utumwa wa ajira za kusubiri miaka na miaka.
Hao wote uliowataja mbona sio wakulima?
 
Kilimo cha kutegemea mvua?
Mkuu ukishafanya research yako utajua na aina ya mazao yanayokubali eneo husika.
The rest unaweza mwagilia kama navyyona watu waliochimba visima mashambani kwa ajili ya umwagiliaji.
 
Siwezi jilaumu kwanini nilisoma kwani elimu inafaida yake kubwa sana.
Baada ya kusoma sasaa nataka nitumie ujuzi wangu huu kujipatia kipato halali.
Nimeamua kwenda shamba kulima na kufuga ngombe na kuku.
Baadhi ya mazao ya shamba kama mahindi, mboga, maharagwe, matunda(Maembe, machungwa, matikiti, ndizi, nanasi n.k) nitauza mengine ntatumia mgahawani kwangu kuuza kama chakula (Nimegundua biashara ya chakula inalipa sana hasa ukiwa na wateja wa kuaminika kulingana na eneo ulilopo kama vyuoni, eneo lenye wapiti njia biashara nyingi).
-Mahindi ya kuchoma uanalipa.
-Chipsi zinalipa.
-Wali, ugali, vitafunwa vya hasubuhi kama mandazi na chapatti vinalipa.

Fiada za kuku na ngombe.
-Mimi nataka ngombe watatu au wane hawa wanatosha kunipa maziwa ya kutosha nikawa nauza mgahawani kama chai au maziwa mgando.
-Kuku kama 200 wanatosha kwaajili ya mayai tuu yakuuza.
-Mbalea itokayo kwa kuku na ngombe nitaitumia kupandia bustani za mboga na mazao mengine.


Faida za shamba
-Unakuwa huru! Hakuna wakukupelekesha wala kuwa kibaraka wa Fulani.
-Unaweza fanya kazi nyingi Zaidi hivyo kukuongezea kipatao chako kuliko kuajiriwa ambapo unapaswa uweo ofisini muda wote.
-Unakuwa na muda mwingi wa kufanya mambo yako kwa Amani.
-Hakuna makato yani pesa unayoipata ndio inayoingia mfukoni moja kwa moja.

Plan
-Kutafuta eneo lenye shughuli nyingi za watu hao watu ni mtaji wangu.
-Inategemea naweza nunua uwanja nijenge mgahawa au nikodishe mgahawa.
-Kujifunza kupika vyakula vitamu ili niteke soko plus chakula cha kutosha ili nipate raia wengi. Hii ni faida kisoko kwa sababu unapotoa huduma nzuri ndipo watu wanavutiwa kuja.
-Kodi ya mgahawa nitajipanga siku zote mwanzo ni mgumu.


NB: Bye bye kutembeza bahasha... naweza pata pesa nyingi namna hii Zaidi ya laki nane kwa mwezi hapo bado makato ya HESLB, sijui wapo huko mwishowe take home inakaribia kali tano kwa siku 30 hapo sijala, sijalipia kodi ya nyuba, usafiri, sijaumwa, sijanunua vocha, sijasaidia ndugu kwa laki 5 hapo ni kudanganyana.
Inapendeza kufikiri nje ya boki. Huku ndiko kujiajiri japo watu wengi hudharau sana wasomi sasa mimi nataka ni wa prove wrong.
Mkuu karibu ulingoni.. ila usi sahau kua mwanzoni huta kua na wk end wala siku kuu kwa maana mtu pekee anaejua unapo elekea ni wewe
 
Utalima mwisho wa siku utakosa pa kuuzia mazao yako au utauza kwa hasara
Bora uchague mazao tofauti na mazao waliyolima kwa wingi watu wa eneo lako kwa sababu kila mtu akivuna ndo hivyo utauza kwa hasara.
 
Ngoja aende ataleta mrejesho!

Kilimo cha internet kitamu sana, anahisi fukara walioko shambani hawana mawazo haya!
Pengine kuna sehemu wanakosea.
Kwa mfano mimi siwezi kulima kama nitakosa chini ya masoko matatu au watu Zaidi ya watano ninao waamini.
Tatizo watu wanalima halafu hawana masoko ya uhakika sasa wategemea nini hapo?

Wanalima mazao ya aina moja watu kibao hapo kuna faida?
Hawana plan B kwamba vipi soko likikosekana kabisa watafanyaje?
Yapo mazao kamamchele, maharagwe .a mahindi unayoweza kuyahifadhi kwa muda mrefu lakini vipi nyanya< mboga, matunda n.k lazima ufikirie possible outcomes zote ndipo uzame shamba.
Ni kwa mawazo yangu mkuu.
 
Mawazo mazuri sana...
Tunaweza ita hiyo plani A kwamba ni idea! Plan B ni practice hapo ndio hatua nyingine tena muhimu sana kwa sabau ukiharibu hapo umeharibu kila kitu. Hiyo plan B itahusisha watu na vifaa vya kazi, mbegu na wewe uwe unafatilia maendeleo ya shamba na mifugo yako kwa karibu
 
Pengine kuna sehemu wanakosea.
Kwa mfano mimi siwezi kuliama kama nitakosa chini ya masoko matatu au watu Zaidi ya watano ninao waamini.
Tatizo watu wanaliama halafu hawana masoko ya uhakika sasa wategemea nini hapo?

Wanalima mazao ya aina moja watu kibao hapo kuna faida?
Hawana plan B kwamba vipi soko likikosekana kabisa watafanyaje?
Yapo mazao kamamchele, maharagwe .a mahindi unayoweza kuyahifadhi kwa muda mrefu lakini vipi nyanya< mboga, matunda n.k lazima ufikirie possible outcomes zote ndipo uzame shamba.
Ni kwa mawazo yangu mkuu.
Kwa kiasi chake unaelewa nini kipo shambani sio hawa wakulima wa google.

Mkulima wa Tanzania tangu tupate uhuru hajawahi kuwa na uhuru wa soko wa wala unafuu na kuwa na maamzi na mazao yake.

Mara zote anapangiwa bei kulingana na matakwa ya mteja(buyer) wake anavyotaka, imeenda mbali zaidi serikali ambayo ilitakiwa iwakingie kifua hawa watu nayo ikajitoa na kuwaacha wakulima wafe peke yao bila kujali gharama za uzalishaji wa hayo mazao na bei ya mauzo( mapato) ili apate faida.

Nawakumbusha tu. Nikibahatika kufanya kilimo sitaenda shambani bali nitajikita kwenye Food chain value addition.
 
Back
Top Bottom