Nimegundua rafiki yangu anacheza kamari

Nimegundua rafiki yangu anacheza kamari

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
58,638
Reaction score
220,410
Huyu rafiki ni kati ya wale wachache niliokua nao mtaa mmoja. Hizi familia zetu za ki Africa, wazazi wake unawaonav kama wazazi wako na birthdays mlikunywa soda pamoja.

Huyu bwana aliogopewa kwa akili tangu akiwa primary school. Alisomea maswala ya fedha. Na amefika mbali.

Tulipoteana kwa miaka mingi, tumekutana miaka mitano iliyopita. Mawasiliano ya udada na ukaka yalianza tena. Alipata kazi kwenye international organisation nje ya Tanzania. Aliniaga na kunieleza donge watakalo mlipa . Ilikuwa donge nono na nkawabia watoto, uncle wenu amefika pale kwakua amefanya urafiki na vitabu.

Baada ya miaka miwili ananipigia simu, dada hali ni mbaya. Nilikuwa na vijiakiba vyangu nikampa, alishukuru na kuondoka. Kumbe alishapoteza kazi.

Jamaa CV yake ni nzuri sana. Haikuchukua muda alipata kazi nyingine kwenye kampuni ya nishati. Mambo yake yalipokaa vizuri kuna siku alinifanyia surprise alinipa 2 millon kwenye bahasha akamiambiacwema ulionifanyia kipindi kile siwezi kuusahau.

January alinipigia simu kuwa anashida ya pesa. Hata mimi hali yangu hazikuwa nzuri, wiki iliyopita alinipigia tena, nilimpa pesa niliyokuwa nayo. Baada ya muda alinipigia kuomba kuja nyumbani tuongee.

Alinishukuru tena na kunieleza amepata kazi nyingine, sasa atachukua zaidi ya 10 million kwa mwezi. Tukiwa na ka wine nilimwambia kaka huu nivwakati sasa utafute mke our, alinijibu wanawake wananikimbia wanadai I’m a gambler. Hapa ndipo niliposhtuka haiwezekani mtu wa position yake aishiwe asiwe hata na laki moja ya dharura.

Nitamsaidia vipi?
 
IMG_20180306_141145.JPG
 
Mpe ushauri wa bure akishindwa kukuskia asubil muujiza wang. Ila kwa huu utawala wa yule jamaa ambae kwao ni chato inabidi asichezee pesa
 
Huyo anahitaji maombi maana kama mpaka wanawake zake wameshindwa kumbadilisha ni kazi kweli.
Wazazi wake wako hai? Labda uongee nao waongee na mtoto wao.
 
Huyo anahitaji maombi maana kama mpaka wanawake zake wameshindwa kumbadilisha ni kazi kweli.
Wazazi wake wako hai? Labda uongee nao waongee na mtoto wao.
Juzi alinieleza mengi ya kusikitisha. Hajamaliza kulipa mikopo wake wa Masters na akiwa hana hela sasa hivi ni baba yake ndiyo anaulipa. Mzee mwenyewe ni pensioner na ndiyo maana hawezi kuwaeleza shida zake nyingine
 
Betting ni gambling disorder ukianza huwezi acha unakua addicted kama drug user vile,na hilo ndio tatizo linalomtafuna huyo ndugu yako,anatakiwa akae chini na ajiulize,toka ameanza kucheza hizo kamari anapata mafanikio au anarudi nyuma? Akipata jibu achukue maamuzi magumu yakubadilika.
 
anahitaji mke zaidi
inawezekana anawaza kamali kutokana na hana wa kumuwazia
 
Madeni, madeni, madeni ndio kikwazo kwa wacheza kamari wasipige hatua, mabadiliko ya tabia hayawezi kutokea kwa ghafla au kwa haraka bali ni taratibu sana, kwa kuwa mmekua nae bila shaka anakuheshimu ndio maana anakushirikisha mambo yake, njia ya kumsaidia ni kuendelea kuwa nae karibu ikibidi na wewe ujue A,B,C,D za kamari uweze kumsaidia zaidi mbeleni, kama kweli umedhamiria kumsaidia inawezekana na itakugharimu pia sababu hata badilika katika usiku moja, kumlaumu, kumtenga na kumpinga haita kuwa suluhu ya kutatua tatizo lake.

Kila la heri, vaa viatu vyake kama anataka kubadilika, vinginevyo muache tu
 
Huyu ana gambling disorder, I almost went through the same phase wakati naishi nje, nilikuwa nikilipwa hela Ijumaa nacheza michezo mbali mbali ya karata au spinning wheels. It is so addictive yaani nahisi more than drags. Ilifika kipindi I once lost 1000£ in just 2 hours. I felt like taking my life. Ila I had to come clean and tell my partner and she had to take control of my finances.

Yaani hapo kama anakuamini basi inabidi ujue all his source of income, tambua akaunti zake zote za benki and take control. Yaani yeye asiwe karibu na hela, pia he needs to avoid kuwa alone.
 
Back
Top Bottom