Senegali walifanya tukio la aibu mbele ya wageni na dunia nzima. Wakati mpira wa Afrika ukianza kuimarika na kutazamwa na watu wote dunia wao Senegal hawakuona hilo na wala hawakuweza kufikiri nini kinafuata.
Mpira ni biashara na hatima za maelfu ya watu unawezaje kufanya blander kama ile kwenye uwanja wenye watazamaji zaidi ya elfu 50? Ulitaka wauane? Ulitaka wadhamini wa mashindano walifikirie vipi soka la Afrika?
1. Juventus – Serie A (2005 & 2006)
Walitwaa ubingwa wa Serie A
Baadaye walinyang’anywa makombe yote mawili kutokana na kashfa ya kupanga waamuzi (Calciopoli)
2005 haikupewa mtu, 2006 walipewa Inter Milan
2. Olympique de Marseille – Ligue 1 (1992–93)
Walitangazwa mabingwa wa Ligue 1
Baadaye walinyang’anywa ubingwa huo baada ya kuthibitika kupanga matokeo (match-fixing)
Huo ubingwa haukupewa timu nyingine
3. Steaua Bucharest vs Dinamo Bucharest – Kombe la Romania (1988)
Mechi ya fainali ilisimamishwa kwa utata
Kwanza kombe walipewa Steaua, kisha likaondolewa/kuhamishwa kwa maamuzi ya kamati
Tukio hili linajulikana kwa mzozo mkubwa wa kisiasa wakati huo
4. FC Sion – Kombe la Uswisi
Walishinda Swiss Cup
Baadaye wakanyang’anywa haki ya kushiriki mashindano ya Ulaya kwa kutumia mchezaji asiye halali
Ingawa kombe lenyewe halikuondolewa moja kwa moja kila wakati, ushindi wao uliathiriwa rasmi
5. Legia Warsaw – Ligi ya Poland (1992–93)
Walimaliza juu kwenye Ekstraklasa
Lakini walinyang’anywa ubingwa kwa tuhuma za kupanga matokeo mechi ya mwisho
Ubingwa ulipewa timu nyingine