Aisee pole sana mkuu. Ulisema tar 7 mwezi huu una mtihani LST. Leo ni tar 8, bilashaka umefanya jana na mambo hayakuwa mabaya. Nakutakia kila la kheri.Pole sana bwana Amicus Curiae , Mungu akupe nguvu na kukuimarisha upite kipindi hiki ulichopo. Wewe ni wakili, kama ulivyosema kuwa unatarajia kufungua ofisi yako wiki ijayo, Mungu awe nawe.
Oktoba 2019 nilifukuzwa kazi katika ofisi ya serikali ambako nilihudumu kama mwanasheria. Nilifukuzwa kazi kwa uonevu tu, kosa likiwa ni utoro kazini - mimi naita uonevu kwa kuwa nilihamishwa kituo hicho kimkakati kuwa nisipafurahie kwa kuwa ni ndanindani na nikose fursa kama vile kujiendeleza kielimu (masomo ya jioni) ambayo kwa Dar ni possible bila hata kuwa na ruhusa kazini, pia uhamisho ulikuwa umefanyika ndani ya mwaka 1 toka nilipopata uhamisho mwingine (taratibu zinasema uhamisho ufanyike baada ya miaka 3 toka mtumishi awepo kituoni) hata hivyo niliripoti. Baada ya kuripoti kituo kipya, Mkurugenzi akagoma kunipa fedha za uhamisho ambazo kimsingi na kisheria nilipaswa kulipwa zote kabla ya kuhamia kituo kipya, sababu za kutonipa akawa anazijua mwenyewe. Huyu Mkurugenzi kabla alikuwa ni HR wa kituo nilichotoka. Nilipoona hali ni ngumu nikaandika barua kuwa ninaondoka mpaka nitakapolipwa malipo stahili ndipo nitarudi.
Ofisi niliyotoka, wafanyakazi wenzangu wakawa wanaongea na Mkurugenzi (ex HR) kuwa nipo mjini (Dar), wakawa wanachochea na kufitinisha, huo ni mwezi Mei 2019, mwezi juni nikasimamishwa mshahara mpaka Septemba 2019. Nikiuliza sababu ya kusimamisha, barua hazijibiwi ila salary slip inaonesha ni utoro. Nikaona hii ni constructive termination, nimefanyiwa zengwe ili nionekane nina makosa lakini kiuhalisia msababishi ni Mwajiri, nikafungua kesi CMA.
Kesi ikiwa CMA mwaka 2019 (Agosti), Septemba 2019 Mkurugenzi akaanzisha 'mchakato' wa kunifukuza kazi kwa kosa la utoro, nikapinga pale CMA uwepo wa mchakato huo kwa kuwa unataka kuharibu kesi iliyopo CMA nikaomba zuio, lakini CMA ikakataa kutoa zuio kwa kudai kuwa haina mamlaka hayo. Kesi ya CMA ilifutwa nikakata Rufaa Makahama Kuu nako ikafutwa kwa sababu za kuwa sijaexhaust local remedies (S.32A ya the Public Service Act), kwa sasa ipo Mahakama ya Rufaa ikisubiri vikao.
Kupunguza urefu wa andiko, nilifukuzwa kazi mwezi Oktoba 2019, kwa bahati mbaya nilikuwa sijamaliza Law School of Tanzania (nilikuwa na vimeo 2) muda huo nikawa nasubiri matokeo, yalipotoka nikawa nimefeli vyote. Nimefanya sana mitihani pale bado nina kimeo kimoja inabidi nikifanye Disemba hii (itakuwa mara ya kumi na... kufanya somo hilo). Sababu ya kufeli sijui, maana hakuna marking scheme pale - kwa hiyo jibu rahisi na lisilo na lawama ni maandalizi yangu mabovu. Ndoto yangu ni kuwa wakili wa kujitegemea, Sijakata tamaa, naendelea kupambana mpaka nikamilishe ndoto hiyo. Najua sababu za kunikwamisha ni nyingi zikiwemo za kibinadamu na kiroho lakini namwamini Mungu atanipitisha. Sina kazi rasmi kwa kuwa sijasajiliwa kama wakili, ninafanya biashara ndogo ndogo (hasa udalali) na kufanya uwakilishi binafsi CMA kwa wahanga wengine kama mimi.
Mwezi Agosti, 2021 nilipata habari kuwa Mkurugenzi aliugua ugonjwa wa akili toka mwezi Machi 2021 akapotea kazini na kukutwa Dodoma akiongea vitu visivyoeleweka, kwa sasa yupo Dar anauguzwa nyumbani kwake akiwa hana akili, hamtambui mtu yeyote. Inaweza kuwa ni Karma (sio kwa ajili yangu tu, bali na wengine aliowaumiza) au ikawa ni magonjwa tu ya kawaida, lakini vyovyote vile kuna la kujifunza.
Usikate tamaa wala kuvunjika moyo, pambana, jiamini na umuombe Mungu, usipoteze imani kwake maana Mungu pekee ndiye ajuaye kesho yako. Disemba 7, 2021 nitafanya mtihani pale LST, ninajiandaa na kuomba Mungu nifaulu, niombeeni pia.
Karibu mkuu..pole kwa matatzo wakil nna stuation kama yako lkn nahtaj msaada wa kisheria kimawazo mkuu
Mungu atafanya njia pasipo na njiaHakika mkuu.
My name is Amicus Curiae, a very prominent lawyer in ..... City.
Nilifika pale ofisini mapema sana miaka kadhaa iliyopita wakati ofisi iko kwenye kipindi kigumu, nikaishi nao hivyohivyo tena kwa upendo, nikawafundisha kazi makumi ya Wanasheria (Mawakili), wakafanikiwa na wengine hawakuaga baada ya kuona mafanikio, boss akawa anawanung'unikia kwangu.
Boss wangu akawa amefanya mambo makubwa sana lakini kipindi hicho kilikuwa kipindi cha nyuma mno. Nikaiga mambo yaleyale ya boss akanisifia yeye mwenyewe na kwa wengine ofisini.
Kumbe mule ndani ofisini watu wakawa wananionea wivu ila ukikutana nao wanakuchekeaaaa... (jamani unafiki upo).
Nikawa nafanya kazi zote zenye malipo makubwa ofisini huku kwa upendo nikiwapa kazi za kunisaidia sambamba na fedha kwa vijana wote pale ofisini ili na wenyewe wapate pesa za kujikimu.
Kumbe roho inawauma. Juzijuzi bila mimi kujua wakapanga njama kwamba nifukuzwe ili wao ndiyo waonekane. Yale yote niliyokuwa nawashirikisha kwa upendo wakayaweka bayana. Boss pamoja na kuniamini akawaamini wao zaidi na kinifukuza kwasababu alishapandikizwa sumu kali sana.
Jamani don't trust anyone. Nakumbuka niliitwa kwenye ofisi ya hasimu (mpinzani) wa ofisi ya boss wangu mara mbili ili niiodhoofishe ofisi ya boss wangu ila nikakataa. Siku niliyoenda kukataa hiyo offer nilikuwa na huyo mtu wa ofisini aliyenichafua, kumbe yeye ndiye aliyefanya yote hadi kufikia hapa nilipo.
Leo nimefukuzwa, HAKUNA ALIYENIPIGIA SIMU HATA YA KINAFKI KUNIPA POLE.
Jamani ukijiona una kitu cha PEKEE kinachopendwa na boss wako jihadhari na hao mashost au mabest wa ofisini, utaula wa chuya.
Nimewasamehe wote and I am moving on.
Mungu na wanadamu. Naomba kubakia. Amen.
Umeiba?au utakuwa umeenda kinyume xha maadili ya kazi zakoMungu na wanadamu. Naomba kubakia. Amen.
Huu ndio ukwelihivyo tuendelee kuish vizuri na marafiki zetu wa kweli waliokua nasi hata kipindi ambacho tulikua hatuna kazi wale ndo marafiki wa kweli japo huwa tunawatenga tukipata ramani.
Ahsante mkuu, juzi nimefanya mtihani. Mungu ni mwema ameonekana kwenye mtihani. 🙏🏿Aisee pole sana mkuu. Ulisema tar 7 mwezi huu una mtihani LST. Leo ni tar 8, bilashaka umefanya jana na mambo hayakuwa mabaya. Nakutakia kila la kheri.
Wala usisikitike mkuu, kuna kitu Mungu ana kuepusha.My name is Amicus Curiae, a very prominent lawyer in ..... City.
Nilifika pale ofisini mapema sana miaka kadhaa iliyopita wakati ofisi iko kwenye kipindi kigumu, nikaishi nao hivyohivyo tena kwa upendo, nikawafundisha kazi makumi ya Wanasheria (Mawakili), wakafanikiwa na wengine hawakuaga baada ya kuona mafanikio, boss akawa anawanung'unikia kwangu.
Boss wangu akawa amefanya mambo makubwa sana lakini kipindi hicho kilikuwa kipindi cha nyuma mno. Nikaiga mambo yaleyale ya boss akanisifia yeye mwenyewe na kwa wengine ofisini.
Kumbe mule ndani ofisini watu wakawa wananionea wivu ila ukikutana nao wanakuchekeaaaa... (jamani unafiki upo).
Nikawa nafanya kazi zote zenye malipo makubwa ofisini huku kwa upendo nikiwapa kazi za kunisaidia sambamba na fedha kwa vijana wote pale ofisini ili na wenyewe wapate pesa za kujikimu.
Kumbe roho inawauma. Juzijuzi bila mimi kujua wakapanga njama kwamba nifukuzwe ili wao ndiyo waonekane. Yale yote niliyokuwa nawashirikisha kwa upendo wakayaweka bayana. Boss pamoja na kuniamini akawaamini wao zaidi na kinifukuza kwasababu alishapandikizwa sumu kali sana.
Jamani don't trust anyone. Nakumbuka niliitwa kwenye ofisi ya hasimu (mpinzani) wa ofisi ya boss wangu mara mbili ili niiodhoofishe ofisi ya boss wangu ila nikakataa. Siku niliyoenda kukataa hiyo offer nilikuwa na huyo mtu wa ofisini aliyenichafua, kumbe yeye ndiye aliyefanya yote hadi kufikia hapa nilipo.
Leo nimefukuzwa, HAKUNA ALIYENIPIGIA SIMU HATA YA KINAFKI KUNIPA POLE.
Jamani ukijiona una kitu cha PEKEE kinachopendwa na boss wako jihadhari na hao mashost au mabest wa ofisini, utaula wa chuya.
Nimewasamehe wote and I am moving on.
Mungu na wanadamu. Naomba kubakia. Amen.
nilichojifunza kazini ni sawa na vitani kila mtu anapigania maisha yake na hakuna rafiki wa ukweli kazini.My name is Amicus Curiae, a very prominent lawyer in ..... City.
Nilifika pale ofisini mapema sana miaka kadhaa iliyopita wakati ofisi iko kwenye kipindi kigumu, nikaishi nao hivyohivyo tena kwa upendo, nikawafundisha kazi makumi ya Wanasheria (Mawakili), wakafanikiwa na wengine hawakuaga baada ya kuona mafanikio, boss akawa anawanung'unikia kwangu.
Boss wangu akawa amefanya mambo makubwa sana lakini kipindi hicho kilikuwa kipindi cha nyuma mno. Nikaiga mambo yaleyale ya boss akanisifia yeye mwenyewe na kwa wengine ofisini.
Kumbe mule ndani ofisini watu wakawa wananionea wivu ila ukikutana nao wanakuchekeaaaa... (jamani unafiki upo).
Nikawa nafanya kazi zote zenye malipo makubwa ofisini huku kwa upendo nikiwapa kazi za kunisaidia sambamba na fedha kwa vijana wote pale ofisini ili na wenyewe wapate pesa za kujikimu.
Kumbe roho inawauma. Juzijuzi bila mimi kujua wakapanga njama kwamba nifukuzwe ili wao ndiyo waonekane. Yale yote niliyokuwa nawashirikisha kwa upendo wakayaweka bayana. Boss pamoja na kuniamini akawaamini wao zaidi na kinifukuza kwasababu alishapandikizwa sumu kali sana.
Jamani don't trust anyone. Nakumbuka niliitwa kwenye ofisi ya hasimu (mpinzani) wa ofisi ya boss wangu mara mbili ili niiodhoofishe ofisi ya boss wangu ila nikakataa. Siku niliyoenda kukataa hiyo offer nilikuwa na huyo mtu wa ofisini aliyenichafua, kumbe yeye ndiye aliyefanya yote hadi kufikia hapa nilipo.
Leo nimefukuzwa, HAKUNA ALIYENIPIGIA SIMU HATA YA KINAFKI KUNIPA POLE.
Jamani ukijiona una kitu cha PEKEE kinachopendwa na boss wako jihadhari na hao mashost au mabest wa ofisini, utaula wa chuya.
Nimewasamehe wote and I am moving on.
Mungu na wanadamu. Naomba kubakia. Amen.
HahahahahMimi nilitiliwa fitna na watu niliowapigiania wakapata ajira kwenye taasisi wakawa wanazunguka wanapeleka maneno kwa manager mkuu hii ngozi nyeusi Ila laana hawakujua mm ndio nilikuwa nawabeba baada ya kuondoka alipokuja manager mwingine akawafyatua wote