Wakuu, naomba kuchuwa nafasi hii kuwashukuru nyote kwa ushirikiano wenu na kuonyesha kujali kwenu. Kuna ambao wameniandikia email na wengine PM, lakini kwa bahati ghafi sikuweza kuwajibu, ni matumaini yangu kuwa wataelewa situation niliyokuwa nayo...!
Nilikuwa kwenye maombolezo ya siku tatu, maana ndio sheria ya dini, msiba ni siku tatu tu. Baada ya hapo basi tunatawanyika kwenda kujitafutia riziki.
Nawashukuru wale wote walio onyesha nia dhati kabisa ya kutoa rambi rambi zao (Ubani) kwangu, Insha'allah Mwenyezi Mungu atawalipa kwa niya yako safi kwa kuonyesha kujali, binafsi sina cha kukulipa, zaidi ya kuwaombea dua na Insha'Allah Mwenyezi Mungu atawarahisishia mambo yao na kuwaepusha na mitihani ya kidunia.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.