NrNe.....
Wakuu Kuna namna watu wa hii nchi wanajitoaga akili sana..
Mwaka Jana Kuna binti alinifata kuniomba ushauri,. Na Kwa jinsi alivyonihadithia matendo ya My wake nikamshauri kiroho safi aachane nae afanye mambo yake ya msingi,. Nikaongea na maneno mawili matatu ili binti anielewe anatakiwa kufanya Nini...
Eti Jana amenipigia simu wamerudiana,. Na alivyokua mshenzi asiniambie mda huo wako wote, me nimeongea maneno yote nimemaliza kumbe wananiskia wote na ilikua video call.....
Hivi ujue kusutwa na mwanaume aibu sana, yaani nilijiskia kufedheheka, mwili mzima baridi, eti naambiwa me Kwa maneno yangu ndo nilisababisha wao wasiwe pamoja,. Eti nimetenganisha familia? Wakati sikua najua kama mda Wana maugomvi Yao binti alikua mjamzito ...
Nakaa nawaza how come amwambie Baby dad wake kwamba mimi ndio nilisababisha ,wakati binti alinifata mwenyewe kuomba ushauri na nikamshauri, . Kama ushauri wangu ulikua hauna maana mbona aliufanyia kazi....
Haya mambo sio ya kunitokea Mimi umri huu... Washenzi kweli hawa