Nimedanganya jinsia yangu

Nimedanganya jinsia yangu

T 1990 ELY

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2014
Posts
12,934
Reaction score
30,093
Habari wana jamiiforum.

Mimi ni kijana wa kiume mwenye umri wa miaka kati ya 20-25 hivi. Siku moja nilisitukia nimeingiza kwenye group moja la whatsapp (jina kapuni) pasipo mimi kuwa na taarifa yoyote ile, sasa kule kuingizwa nikawa napimishia tu chating zako nikawa nimetuma sms ya hodi wadau wakaitia karibu.

Kuna mdau moja akawa ametuma sms ya mgeni tunaomba picha yako nikatuma picha ya demu fulani hivi mzuri sana wadau wakaanza ooh mgeni we mzuri sana mara ooh! Mgeni upo wapi mara ooh mgeni nimekupenda nikasitukia mdau moja kanifata inbox nikawa nachati nae na ikumbukwe kuwa hapo nimeficha,nimeongopea jinsia yangu so jamaa akawa anajua kuwa anachati na demu kwa sababu ya ile picha niliyotuma kwenye group.

Nilichati nae vizuri kwa kujifananisha kuwa mimi ni msichana mpaka jamaa akafikia hatua ya kuvunja ukimya juu ya ile picha nikawa nimemkubalia jama. Sasa jamaa amenituma nauli nimfate aliko maana yupo mkoa tafauti na nilipo mimi na nauli yake si chini ya elfu 80000 na jamaa kanitumia laki moja(100000) na hali niliyonayo mimi huku si nzuri kwa kweli kiuchumi.Sasa napenda mnishauri kuwa jamaa nimwambie ukweli kuhusu jinsi yangu? Au niitumie tu hii hela kwa mambo yangu binafsi? Au nimurudishie tu hii hela?.

Wapendwa ushauri wenu tafadhali.
 
Habari wana jamiiforum.Mimi nikijana wa kiume mwenye umri wa miaka kati ya 20-25 hivi.Siku moja nilisitukia nimeingiza kwenye group moja la whatsapp(jina kapuni) pasipo mimi kuwa na taarifa yoyote ile,sasa kule kuingizwa nikawa napimishia tu chating zako nikawa nimetuma sms ya HODI wadau wakaitia karibu.Kuna mdau moja akawa ametuma sms ya mgeni tunaomba picha yako nikatuma picha ya demu fulani hivi mzuri sana wadau wakaanza ooh mgeni we mzuri sana mara ooh mgeni upo wapi mara ooh mgeni nimekupenda nikasitukia mdau moja kanifata inbox nikawa nachati nae na ikumbukwe kuwa hapo nimeficha,nimeongopea jinsia yangu so jamaa akawa anajua kuwa anachati na demu kwa sababu ya ile picha niliyotuma kwenye group.Nilichati nae vizuri kwa kujifananisha kuwa mimi demu mpaka jamaa akafikia hatua ya kuvunja ukimya juu ya ile picha nikawa nimemkubalia jamaa.Sasa jamaa amenituma nauli nimfate aliko maana yupo mkoa tafauti na nilipo mimi na nauli yake si chini ya elfu 80000 na jamaa kanitumia laki moja(100000)na hali niliyonayo Mimi huku si nzuri kwa kweli kiuchumi.Sasa napenda mnishauri kuwa jamaa nimwambie ukweli kuhusu jinsi yangu??au niitumie tu hii hela kwa mambo yangu binafsi???au nimurudishie tu hii hela????.Wapendwa ushauri wenu tafadhali.

images


Sorry bro, but you sound La-di-da-di to me​
 
Hapa naona mambo mawili: wewe kidume utajifanyaje kijike, acha tabia za kike, pili unajifunza utapeli ushauri acha utapeli na udada.
 
Wewe unakokwenda pabaya? Ss hv watakupumulia kisigon

Hapana mkuu nilikuwa namwonyeshea dalili zote kabisa kuwa Mimi mwanaume so jamaa hata hakusitukia aiseeeeee.Ivi kweli utashindwa kujua or kuhisi tu kuwa unachati na mwanaume mwenzio hata kwa mwandiko?????Dah sisi mwanaume bhana huwa tunatapeliwa kizembe kweli.
 
Hapa naona mambo mawili: wewe kidume utajifanyaje kijike, acha tabia za kike, pili unajifunza utapeli ushauri acha utapeli na udada.
Akhsante kwa ushauri wako mkuu ila kweli ushindwe kujua kuwa unachati na mwanaume mwenzio??Dah
 
Uko hatarini. dume gani unatuma picha ya demu. utashtukia 'kabang' endelea tu na upuzi.
 
hahahahahahaaaaaa..yani nimecheka hadi machozi yamenilenga
 
Aahhaa kumbe ndio maana haupokeagi cmu eeehh, nirudishie pesa zangu la siivyo nakushusha busha..
 
T 1990 ELY

daah labda nikuulize swali mwanzoni ulipoambiwa utume picha yako kwanini ulituma ya demu?halafu ulivyopewa sifa mara wee mzuri,cjui nini na nini we ukaendelea kukubali kwamba we ni demu ulitegemea nini hapo?in short me sijui hata nikushauri nini hadi jamaa kajikamua katoa kilo(laki) ya nauli akijua wewe ni demu kumbe ni men mwenzake....take care badae utalia ndg yangu
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom