Nimechoka Kuota Napaa Usiku

Nimechoka Kuota Napaa Usiku

Nimechoka Kuota Napaa Usiku...


Ni mwaka Sasa mara kwa mara nimekuwa naota Napaa angani au kucheza mchezo WA kupaa milimani au angani na kutua vizuri tu bila matatizo yoyote uku nikifurahi

Kuna muda naota Kuna tatizo linatokea na tukiwa sehemu watu wengi na mi pekee nafanikiwa ku escape kwa kupaa uku nikiwaacha wengine wakishindwa kuescape,siku nyingine naota Napaa angani uku nikiwa na furaha sana

Iyo Ndoto inamaanisha Nini kwa wajuzi WA mambo ya Ndoto?
Mkuu hiyo ni ndoto yenye dalili nzuri sana kwa maisha yako, inaashiria ukiweza kutumia vizuri fursa na uwezo wako uliopewa utafika mbali na kuwa juu ya wengi. Utavuka viunzi vingi maishani wa urahisi kuliko wengine, ila yahitaji ujitume na uwe na nidhamu binafsi.
NB: Wengi huota ndoto hiyo na kuichukulia kawaida ila iina maana kubwa
 
tatizo limeanzia nilipoanza kula Malaya na kunywa pombe Hadi kupitiliza Kuna muda napoteza kumbukumbu,pia ninapitia kipindi kigumu nimeapply sana kazi tangu graduation 2021 mpaka Sasa ila siitwi interview na saa ingine naitwa muda ukiwa umeenda,ila iyo Ndoto imekuwa ikijirudia
Mkuu bado upo gizani Mara ya MWISHO kula Malaya ilikua lini?
 
Hiyo ndio Hand brake ya kupaa?
Hapana ukilala kifudi fudi ukaachia miguu na mikono mwili unakuwa free kupitiliza(hapa kuna wanaoshikwa na jinamizi).
Kiimani ni kuwa ukionanunaota unapaa ujue kuna watu wanakuguatilia kukukamata ila malaika wako wanakupeperusha usikamatwe
Zamani hiyo ndoto ilinisumbua sana kipindi nalala peke yangu ila kwa sasa nina mwenzangu imekata yenyewe
 
Hii ndoto miaka 3 nyuma nilikuwa naota karibu kila siku mpaka akili ikwa inawaza naweza kupaa. Huwa siamini sana hizi habari ila baadae nikaanza kuamini kabisa I can fly.
Kwa sasa sioti tena baada ya kupuuzia nikachukulia mambo ya kawaida tu.
But naamini roho zetu huwa zinafanya mambo makubwa sana tuwapo tumelala kupitia ndoto.
Yaan exactly kama unavyoota wewe.
 
Nimechoka Kuota Napaa Usiku...

Ni mwaka Sasa mara kwa mara nimekuwa naota Napaa angani au kucheza mchezo WA kupaa milimani au angani na kutua vizuri tu bila matatizo yoyote uku nikifurahi

Kuna muda naota Kuna tatizo linatokea na tukiwa sehemu watu wengi na mi pekee nafanikiwa ku escape kwa kupaa uku nikiwaacha wengine wakishindwa kuescape,siku nyingine naota Napaa angani uku nikiwa na furaha sana

Hiyo Ndoto inamaanisha nini kwa wajuzi wa mambo ya Ndoto?
Kuna kitu kinaitwa ndoto, ufunuo na Maono

Mungu huwa unazungumza na wanadamu kupitia Ndoto
Maono na Ufunuo ni kwa wale wanadamu wapo wanaomwabudu Mungu kwa roho na kweli.

Ndoto unaoyoota Mungu anakufikiashia ujumbe hali yako ya kiroho Siyo Nzuri ipo chini inawezekana ikawa wewe ni mchawi kipofu wewe mwenye haujuwi. Mchawi kipofu ni Mtu anayetumiwa na kazi za kichwi bila yeye mwenye kujua. Watu hawa ni wengi sana.

Kuna Mtu mmoja alikuwa anaota Ndoto anaendesha Gari, huyu Mtu akawaa anaamini ipo Siku atapewa gari kuendesha lakini Mungu alikuwa anamfikishia ujumbe kwa yeye ni Dereva wa wachawi usiku.
 
Kuna kitu kinaitwa ndoto, ufunuo na Maono

Mungu huwa unazungumza na wanadamu kupitia Ndoto
Maono na Ufunuo ni kwa wale wanadamu wapo wanaomwabudu Mungu kwa roho na kweli.

Ndoto unaoyoota Mungu anakufikiashia ujumbe hali yako ya kiroho Siyo Nzuri ipo chini inawezekana ikawa wewe ni mchawi kipofu wewe mwenye haujuwi. Mchawi kipofu ni Mtu anayetumiwa na kazi za kichwi bila yeye mwenye kujua. Watu hawa ni wengi sana.

Kuna Mtu mmoja alikuwa anaota Ndoto anaendesha Gari, huyu Mtu akawaa anaamini ipo Siku atapewa gari kuendesha lakini Mungu alikuwa anamfikishia ujumbe kwa yeye ni Dereva wa wachawi usiku.
Wewe una fikra pana sana mkuu sio kila ndoto ni MUNGU anakuotesha
 
Ni uwezo wako wa kuyashinda majaribu/magumu katika maisha yako ya kila siku,ndio maana unakuwa na furaha.
 
images.jpeg
 
Ndoto kama hiyo mwenzio ujue hapo kampokea Yesu,

Kupaa huko ni Mungu anamuonesha jinsi gani ambavyo Neno la Mungu (Kumjua Mungu) limemsaidia kukwepa vikwazo na matatizo katika maisha.
Basi sawa,, vizuri kama ndo hivyo 🤗
 
Ndoto nzuri zidisha bidii kwenye utafutaji au ongezq kujikomba kwa bos wako utanishukuru
 
Back
Top Bottom