Mpap Ndabhit
JF-Expert Member
- Jan 15, 2014
- 380
- 534
Nilimaliza elimu yangu ya juu na kutunukiwa shahada ya KWANZA mwaka 2012. Tangu wakati huo nimekuwa nikifanya application NYINGI, mpaka sasa nimefikisha 289 application letters. Nimeitwa kufanya interview mara 12 kati ya hizo nimehudhuria 9 ambapo sijabahatika hata moja. Na Age yangu nayo inanikimbiza vibaya. Kwa kweli jamani NAOMBA USHAURI, nishaurini. Mimi ni mtoto wa mkulima na nilikuwa mkulima na mfugaji mzuri sana. kupitia shughuli hizi niliweza kujenga nyumba, kutunza mke na watoto na hata kujisomesha japo baadaye SERIKALI ilinisapoti kupitia bodi ya Mikopo. Baada ya kumaliza masomo nilijikuta nimemaliza mtaji wote wa kuendeleza shughuli zangu na sasa nimekuwa mtumwa wa kutafuta ajira ambazo hazipo, na kama zipo zinatolewa kwa rushwa, upendeleo, kujuana na vigezo vigumu. JE mawazo yangu ni sahihi? Na Hawa bodi ya Mkopo HSELB wanayo haki yakufuatilia huko shambani?