real G
JF-Expert Member
- Feb 7, 2013
- 5,227
- 5,303
mkuu unahama vodacom uhamie wapi? tigo? airtel , zantel, smart, au halotel?Heshima sana wanajamvi,
Wiki mbili zilizopita simu yangu ilikwapuliwa na watoto wa mjini kwakuwa nilikuwa na safari nyingi nje ya mkoa sikupata nafasi ya kurenew line yangu.
Leo nikaamua kwenda ofisi za Voda Uhuru road kwanza nikakutana na foleni kubwa kiofisi kidogo hewa gongana nikataka kuondoka lakini nikaona isiwe taabu ngoja nikomae.Kwanza nikapewa fomu nikatakiwa kujaza simu tano za mwisho,m pesa tano za mwisho,sijui kifurushi cha internet......Mara kitambulisho nikamaliza kupeleka fomu kwa mdada mwenye maringo ya kijinga kaona ajira ya Voda mali sana imemwezesha kupaka wanja na kubadili vigauni vya mtumba kabonyeza bonye computer kanirejeshea fomu namba za watu wa mwisho kuongea nao tatu sio sahihi nikamwambia kwakuwa mbili ni sahihi na simu iliibwa wiki mbili zilizopita si rahisi kukumbuka zote.Kachukua fomu kaandika loss report nenda polisi wakakujazie ebo nikamwambia nani kakwambia nina muda mchafu kwani Voda ipo yenyewe kwa taarifa yako nina line nyingine za mitandao 3 hizi si zama za TTCL na ukiritimba za enzi za Mwl nikachana fomu nikaitupia kwenye dustbin nikamwambia Vadacom kwaheri.
Masharti ya kupata line mpya iwapo simu imepotea/imeibwa yamekaa kizamani sana kama taarifa zangu zipo sahihi eg kitambulisho nilichosajilia simu,majina na nk yapo sawa kwanini wanaleta urasimu wa kuangaisha wateja.
kwa taarifa yako tu, kama umeona huo ni usumbufu hadi ukaondoka voda, huduma kwenye hii mitandao mingine ni za kusuasua sana
alafu kwa ninavyokuona wewe ni mswahili na mtu wa lawama sana, hapo umepoteza line ukakaa wiki 2 bila ku renew ukasahau namba wewe unakutana na dada ambaye anafuata masharti ya kazi yake unamlaumu?
na vodacom hayo masharti waliyowekwa ndiyo yaliyowekea na tcra na yanatakiwa yafuatwe na kila mtandao, voda hawana njaa sana na wateja nenda labda halotel au tigo huko ambao una renew line kwa taarifa fake kiasi kwamba unaweza ku renew hata line isiyo yako ukafanya nayo utapeli
acha kumtusi dada wa watu makosa unayo wewe