Nimeamua kuachana rasmi na Vodacom

Nimeamua kuachana rasmi na Vodacom

...i wish angekuona ulivyoikunja hiyo form yao,halafu uitupie kwenye dustbin akikuona, halafu, aendelee kujipaka lipshedo vizuri!
 
Karibu Halotel buku unapata mb 800. Unata nini zaidi. Hao wadada wa voda ni wajinga sana, nawafahamu, wana nyodo sana
 
Loss report ya polisi sio mbaya maana inakulinda na wewe. Ila all in all Vodacom lazima wabadilike maana hamna namna nyingine sasa! Nyuma kidogo nilikosea kutuma hela nikawaomba wanirudishie hela yangu... hadi kesho sijapata nawavumilia tuu ila nawategea!! Kuniondolea unlimited ya 1000 kwa siku nimewamaindi sana asee!!! Manyanyaso yanazidi kuwa mengi asee!! Wapi halotel!!!!!!!!!!!!!!
 
Haaa haaaa napata picha sasa Dada we unaishi wapi halafu una macho mazuri karaha zote za nini bora kuhamia mitandao mingine.

Niliripoti simu nikaishia kutongozwa. Kwa heri simu yangu note4
 
Kweli voda majanga. Tigo nikiweka MB8 naperuzi internet 24 hrs.. Sasa Voda the same package (MB8), dk 1, haiishi. Ni majanga matupu.....najuta kuwafahamu Voda..tupa kule
 
Yaaan mm cku hz cna hbri nao cjui voda,tigo nawakati airtel kaboresha huduma mpka raha vifurushi vya kutosha na vinaeleweke wao waacheni waendelee na ukubwa wa jina tu mwisho watajua nn ni nn
 
haaa! voda siku za hivi karibuni wamekuwa na huduma mbovu kupindukia anyway mimi niliisha wakimbia loooong time ago nipo kwa zain
 
Ni walawale wanaoajiliwa bila ya ujuzi. Customer service zito. Nani wakulaumiwa wateja wkikikimbia?

Vijana hawaelewi mshahara unatoka kwa wateja, bila ya wateja hakuna wanja mama.
 
Nadhani Voda wamejisahau hawajui wapo katika mfumo wa soko wangeweza kufanikiwa iwapo wangekuwa wenyewe.

Yaaan mm cku hz cna hbri nao cjui voda,tigo nawakati airtel kaboresha huduma mpka raha vifurushi vya kutosha na vinaeleweke wao waacheni waendelee na ukubwa wa jina tu mwisho watajua nn ni nn
 
Kurenew laini ya simu vodacom wanacompicate sana. Wanaish ujima bado.
 
Heshima sana wanajamvi,

Wiki mbili zilizopita simu yangu ilikwapuliwa na watoto wa mjini kwakuwa nilikuwa na safari nyingi nje ya mkoa sikupata nafasi ya kurenew line yangu.

Leo nikaamua kwenda ofisi za Voda Uhuru road kwanza nikakutana na foleni kubwa kiofisi kidogo hewa gongana nikataka kuondoka lakini nikaona isiwe taabu ngoja nikomae.Kwanza nikapewa fomu nikatakiwa kujaza simu tano za mwisho,m pesa tano za mwisho,sijui kifurushi cha internet......Mara kitambulisho nikamaliza kupeleka fomu kwa mdada mwenye maringo ya kijinga kaona ajira ya Voda mali sana imemwezesha kupaka wanja na kubadili vigauni vya mtumba kabonyeza bonye computer kanirejeshea fomu namba za watu wa mwisho kuongea nao tatu sio sahihi nikamwambia kwakuwa mbili ni sahihi na simu iliibwa wiki mbili zilizopita si rahisi kukumbuka zote.Kachukua fomu kaandika loss report nenda polisi wakakujazie ebo nikamwambia nani kakwambia nina muda mchafu kwani Voda ipo yenyewe kwa taarifa yako nina line nyingine za mitandao 3 hizi si zama za TTCL na ukiritimba za enzi za Mwl nikachana fomu nikaitupia kwenye dustbin nikamwambia Vadacom kwaheri.

Masharti ya kupata line mpya iwapo simu imepotea/imeibwa yamekaa kizamani sana kama taarifa zangu zipo sahihi eg kitambulisho nilichosajilia simu,majina na nk yapo sawa kwanini wanaleta urasimu wa kuangaisha wateja.

Hawajapata hasara yeyote ile,wateja wapya kila siku si chini ya 100000.mimi mwenyewe nilikua nasajili wateja wastani 20 daily.
 
Mbona Airtel hakuna huo upuuzi.Wakikupatia line maana yake line iliyoibwa haiwezi kufanyakazi tena.Loss report ni kama nilikuwa nataka kuifatilia simu yangu lakini si muda huo hata kidogo.
Kwa sasa kama hujafanya simswap maana yake ni kuwa ile line yako iliyoibwa inaweza kutumika na mtu aliyeiiba. Pengine utaratibu wa Voda sio mzuri, lakini kwa ujumla wake matukio mengi ya wizi katika simu (mobile money) mara nyingi yanahusisha simswap.

Kwa kutoripoti polisi, hiyo ni hatari (risk) kwako. Hata kama hutaki kupata line yako ya zamani lakini kuripoti polisi kuwa imeibwa ni kinga muhimu.

Well, pengine sio jambo kubwa kivile!
 
mtoa Huduma angeonekana na busara iwapo angefata customer care principles!!
busara ni dawa
 
teheteh Ngongo Una huishiwi vituko.............nakumbuka miaka ya nyuma Ulipoamua kuachana na Arsenal(kama sijakosea) ukaleta uzi na kichwa kama hiki..''Nimeamua kuachana rasmi KUISHABIKIA ...''
 
Back
Top Bottom