X_INTELLIGENCE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2014
- 10,700
- 14,768
Wanajamvu MMU nimerudi tena kijana mwenzenu naombeni ushauri kuna msichana nampenda sana na tumedumu kwa muda mrefu japo si sana mimi namuamini sana na kwa mujibu wake pia ana niamini ilikudhihirisha upendo wangu wa dhati kwake niliamua kumuweka in relation kwenye account yangu ya FACEBOOK.
La ajabu mpenzi wangu alinijia juu na kunitaka nifute kabisa hayo maandishi kule FACEBOOK jambo hilo limesababisha tuwe na mawasiliano mabaya inafikia kipindi nikimpigia simu hapokei wala hanitumii message kama zamani hivi kweli facebook inaweza kusababisha mimi na yeye tuachane?
Roho inaniuma sana kwani ananiacha kipindi ambacho bado namuhitaji na inavyoonekana yupo serious na uamuzi wake.
Naombeni ushauri wenu wana jamvi wenzangu.
La ajabu mpenzi wangu alinijia juu na kunitaka nifute kabisa hayo maandishi kule FACEBOOK jambo hilo limesababisha tuwe na mawasiliano mabaya inafikia kipindi nikimpigia simu hapokei wala hanitumii message kama zamani hivi kweli facebook inaweza kusababisha mimi na yeye tuachane?
Roho inaniuma sana kwani ananiacha kipindi ambacho bado namuhitaji na inavyoonekana yupo serious na uamuzi wake.
Naombeni ushauri wenu wana jamvi wenzangu.