Sumba-Wanga
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 5,349
- 1,224
Hebu kaa na mume wako na mwambie kwamba unamwacha uone atafanya nini....
jamani hivi m.me mzinzi huwa anabadilika?mimi siamini hicho kitu,kama kubadilika mpaka yamkute ndio hubadilika.ila hata umuwekee vikao ni ngumu au labda aamue mwenyewe tu.kikubwa utaambiwa vumilia,muombe mungu kuna mawili uvumilie uletewe ukimwi ndani ya nyumba,au uvumilie uishi maisha ya huzuni kila siku.tangu sister wangu,tulimzika kwa ukimwi kwa kuambiwa neno la vumilia,muombe mungu.{kwa upande wangu simvumilii m.me mzinzi}bora niwe sina mtu niwe lonely maisha kuliko kuvumilia.sister jitahidi kujikomboa kimaisha.wewe ndio unaishi nae,unajua mazuri na mabaya yake.unavyoamua,amua kwa ajili ya mtoto wako na usiamue kwa kuiridhisha jamii.kwa miaka yako,bado mdogo,
Sasa kama mume humpendi wala humtaki wa nini unabaki nae?!Kama umeona hamna kitakachobadilika kaanze maisha yako upya mlee kila mmoja akiwa kwake!
vidumu oyeeeeeeeeeeeeee,kwani huwezi kuwakeeep wote wawili?mbona wengine wanaweza?lol:confused2::whistle:
...... nakumbuka ni kama miezi 2 imepita kuna kijana alionyesha kunipenda sana, huyo kijana ni mwanafunz wa chuo kikuu kimoja na yupo mwaka wa 3, na alikuwa anaishi jirani na nyumbani kwangu. kweli nikatokea kumpenda sana na tukaanzisha mahusiano bila yy kujua kwamba me ni mke wa mtu......
Lizzy, ni ushauri mzuri, lakini huyu dada yupo kwenye ndoa, na sio vizuri ku-solve tatizo kwa kukimbia, kwani hadi wanaoana alikuwa hajui kuwa anampenda?
Hapo kwenye RED ndio ukweli..
Dada, Mama K, asante kwa kutuomba na sisi tukushauri ufanye nini...
Kikubwa ninachokiona mapenzi na huyo mwanafunzi yajengwa katika misingi ya ngono..na mara nyingi ngono ya uwizi inaonekana ni tamu, lakini madhara yake ni makubwa.
Tayari umefanya vyema kumshauri huyo kijana atafute maisha mengine; na sioni sababu ya wewe kuendelea kuwa naye wakati umeshajua nini kinaendelea.
Nakushauri utafute muda ukae na mumeo muongee yanayowasibu..Kama umekuwa na ushahidi wa kutosha kwa mumeo kuwa anatoka nje ya ndoa, kwanini usiyapeleke kwa wazazi au washenga wenu?
Hapa unasema;
Umefanya kosa, ndo maana hata moyo wako unakusuta..na huwezi kulipiza baya juu ya baya, na ikanonekana ulifanya haki. Kosa ni kosa tu.
Mie ninaona wewe bado ni msichana mdogo, 24, na maamuzi unayoyafanya ni ya kitoto. Angalia sana, usije ukapoteza ndoa yako kwa sababu tu ya huyo mwanafunzi. Hapa unasema mume wako yuko busy,ni mtu wa safari, una hakika gani kwamba amekuwa ni mtu kutoka nje??..
Hakuna ndoa iliyokamilika dada, zote zina shida kuliko..na unayofurahia mapenzi ya huyo kijana kwa sababu tu hakuna majukumu mengine mazito kama huyo kijana kutafuta chakula, kulea mtoto, yaani kwa kifupi, kinachowakutanisha nyie ni ngono tu..
Sasa kama unataka kuona maisha machungu, achana na huyo mume wako, na ukaishi na huyo kijana, halafu ndo utajua nini maana ya majukumu.. Inaonesha wewe ni mama ya nyumbani, sidhani kama mumeo hakupi matunzo mengine. Sina mengi, ila achana na huyo kijana kama ulivyoamua na uanze kujenga ndoa yako upya. Simama mwanamke..simamia ndoa yako.