MURUSI
JF-Expert Member
- Jun 25, 2013
- 4,491
- 8,721
Nilifanikiwa kuhudhuria mikutano miwili siku ya Ijumaa na Jumamosi. Kuna vitu nilivishuhudia ambavyo kwa kweli kama Wakristo tunapotoka sana.
1. Kwenye mkutano hakuna aliyekuwa amebeba Bible-Hiki ndo kitabu cha mwongozo kwa Wakristo ila pale sijaona mtu mwenye bible.
2. Mtumishi alivyo mkuwa anafika Jukwaani anaanza na watu watoe shuhuda. Nilishangaa sana kwa kweli badala watu wahubiriwe wokovu mtumishi anaanza na watu wenye shuhuda.
3. Watoa shuhuda wana utata sana. Baadhi ya miujiza ina utata kwa kweli. Mmoja wa mtoa ushuhuda alidai baada ya simu yake kuombewa na Nabii alitumiwa pesa laki 2 na baada ya kufika nyumbani akakuta na mume wake ametumiwa laki 3 kimiujiza.
Hakufafanua alitumiwa na nani hasa. Je ni alikuwa anadai mtu? Je kuna ndugu yake alimtumia? Je ni Vodacom walimtumia? Je ni pesa ilitumwa kimakosa kwake? Hapa kuna utata.
4. Watoa shuhuda wengi ni wanawake na hasa kwenye mambo ya uzazi.
5. Mtumishi anasisitiza sana watu watoe sadaka ile noti yenye thamani.
6. Mpaka naondoka siku ya pili sikusikia sehemu mtumishi anahubiri kuhusu watu waache dhambi, watu wawe wema, watu wajiandae na kurudi kwa yesu mara ya pili. Haya sikuyasikia kabisa.
7. Ni sehemu chache sana mtumishi alikuwa anatumia bible. Mahubiri yake mengi ni juu ya mikosi, kurogwa na kadhalika.
8. Mkutanoni mtumishi aliuza sana stika, mafuta ya upako, Jarida lake na Maji. Sijajua maji kama ni kampuni yake.
9. Mtumishi alikuwa anaingia na V8 tinted na hakuna cha kupungia hata waumini mkono.
Kwa kuhitimisha sasa.
Kwa kweli zile shuhuda nyingi ni za kupangwa watu wanapangwa watoe shuhuda.
Baada ya ule mkutano nimeapa.kutokwenda kwenye mikutano ya Manabiii.
Kwenye kukanyaga wese ya upako mimi niliwahi kukanyaga wa kwanza kwanza hivyo wakati majanga yanaanza tayari nilikuwa nje ya uwanja.
Sent using Jamii Forums mobile app
1. Kwenye mkutano hakuna aliyekuwa amebeba Bible-Hiki ndo kitabu cha mwongozo kwa Wakristo ila pale sijaona mtu mwenye bible.
2. Mtumishi alivyo mkuwa anafika Jukwaani anaanza na watu watoe shuhuda. Nilishangaa sana kwa kweli badala watu wahubiriwe wokovu mtumishi anaanza na watu wenye shuhuda.
3. Watoa shuhuda wana utata sana. Baadhi ya miujiza ina utata kwa kweli. Mmoja wa mtoa ushuhuda alidai baada ya simu yake kuombewa na Nabii alitumiwa pesa laki 2 na baada ya kufika nyumbani akakuta na mume wake ametumiwa laki 3 kimiujiza.
Hakufafanua alitumiwa na nani hasa. Je ni alikuwa anadai mtu? Je kuna ndugu yake alimtumia? Je ni Vodacom walimtumia? Je ni pesa ilitumwa kimakosa kwake? Hapa kuna utata.
4. Watoa shuhuda wengi ni wanawake na hasa kwenye mambo ya uzazi.
5. Mtumishi anasisitiza sana watu watoe sadaka ile noti yenye thamani.
6. Mpaka naondoka siku ya pili sikusikia sehemu mtumishi anahubiri kuhusu watu waache dhambi, watu wawe wema, watu wajiandae na kurudi kwa yesu mara ya pili. Haya sikuyasikia kabisa.
7. Ni sehemu chache sana mtumishi alikuwa anatumia bible. Mahubiri yake mengi ni juu ya mikosi, kurogwa na kadhalika.
8. Mkutanoni mtumishi aliuza sana stika, mafuta ya upako, Jarida lake na Maji. Sijajua maji kama ni kampuni yake.
9. Mtumishi alikuwa anaingia na V8 tinted na hakuna cha kupungia hata waumini mkono.
Kwa kuhitimisha sasa.
Kwa kweli zile shuhuda nyingi ni za kupangwa watu wanapangwa watoe shuhuda.
Baada ya ule mkutano nimeapa.kutokwenda kwenye mikutano ya Manabiii.
Kwenye kukanyaga wese ya upako mimi niliwahi kukanyaga wa kwanza kwanza hivyo wakati majanga yanaanza tayari nilikuwa nje ya uwanja.
Sent using Jamii Forums mobile app