: Majibu ya Ushuhuda jimboni karatu
Nimesoma ushuhuda wa mwanajamvi anayejiita KASHAGA kwamba Slaa hajafanya kitu Karatu hivyo hafai kuwa Rais kwasababu hakumaliza tatizo la maji karatu kwa miaka 15 aliyopewa.
Kwanza niseme Ushuhuda wako hapa Jamvini umeniwezesha nisiumize akili kujua kuwa una uwezo mdogo kutafakari mambo na unasumbuliwa na tatizo kubwa la Itikadi ya chama na chuki binafsi dhidi ya Dr. Slaa. Huwezi kusema umeshuhudia tatizo la maji Karatu ukiwa kwenye gari kwenda Loliondo kufuata dawa ya babu. Kwanza ulikuwa na matatizo ya afya wakati unafanya utafiti ukiwa kwenye gari, pili ulikuwa unawaza utapataje dawa ya Babu hasa ukizingatia foleni ya watu, TATU tatizo la maji karatu haikuwa ajenda yako kuitafiti umeiibua tu kwa mawazo yako finyu ukaona ni HOJA hapa, NNE hujamhoji hata mtu mmoja kupata maoni yao kujua hilo tatizo la lini?, TANO hujui historia ya jimbo la Karatu ndo maana ukiona watu wanafata foleni kupata maji unaona ajabu. Zamani hakukuwa na mabomba ya maji kupanga foleni kupata hayo maji zaidi ya msituni, leo umepita hapo kufuata dawa Loliondo umeona mabomba ya maji hiyo ni hatua. CCM imeongoza jimbo hilo tangu enzi na hata baada ya mwaka 1980 ilipogawanywa kutoka Mbulu hawakuweka bomba zaidi ya mabomba ya mjerumani, sasa Slaa kashirikiana na wananchi kwa miaka 15 kaweka mabomba kila kijiji na wananchi wanajisimamia wenyewe huoni ni hatua nzuri unakimbilia kukosoa. Haumtendei haki hata kidogo. Please badilika kimtizamo ndugu yangu. Kwa taarifa yako katika mwanzo wa uwakilishi wa Slaa hapo jimboni alipata sana shida kushirikisha wananchi kuleta maendeleo kwasababu CCM walivuruga kila alichotaka kufanya, mikutano ya hadhara na wananchi kujadili kero zao zilizuiwa kupitia vyombo vya dola, mabomba ya maji yalivyowekwa CCM walikata usiku, yote hiyo ni kutotaka juhudi za mbunge mpinzani isionekane ili warejeshe jimbo uchaguzi uliofuata. Walishindwa kwasababu wananchi wa Karatu tunamisimamo yetu, hatujui itikadi tunajua maslahi ya taifa letu. Fuatilia historia ya jimbo la MBULU tangu wakati wa Nyerere, hatutaki kitu kinaitwa maslahi ya chama au watu binafsi, tunajua demokrasia, Mwaka 1965 Nyerere alimleta Chief Sarwat kama mgombea wa TANU Mbulu wananchi wakamwambia huyo ni wako umetoka naye Dar es Salaam, sisi tunaye kijana wetu wa hapa tutamtuma Bungeni, wakamsimamisha Dodo.Hiyo ndo historia ya misimamo ya wananchi wa Karatu, Babati na Hanang' wakati huo hizo zikiwa tarafa za Wilaya ya Mbulu.
NOTE:Ungekuwa na mawazo hayo ya kuhukumu basi usingechagua CCM mwaka jana kwasababu JK na CCM hawakumaliza matatizo ya jamii kama maji na afya katika majimbo waliyopewa, lakini pia si hukumu halali kwasababu hata babu yetu marehemu Nyerere aliongoza taifa hili kwa miaka 24 na hakumaliza tatizo la umaskini. "Development is a Process"
Natumai kwa haya machache ndugu yangu KASHAGA utabadilika kimtizamo na utaacha kuhitimisha jambo kwa ushahidi mdogo.
Nawasilisha.