Kaka Mpendwa
JF-Expert Member
- Jan 10, 2008
- 772
- 415
mimi siwezi kuwa mnafiki jimbo langu ni la moshi mjini ambalo nimeishi zaidi ya miaka 20 sasa,lakini ki ukweli ndugu Ndesamburo amefanya mengi sana pale na ndio maana unapokuja uchaguzi tunaweka vyama pembeni a kumchagua huyu mzee kwani yeye kama mbunge amefanya mengi sana na hata ukimuuliza mtoto mdogo atakuonyesha aliyofanya mzee Ndesa si kwenye maji tuu,Ndesa kasaidia,mashule,barabara,hospitali,masoko,michezo etc,sasa Slaa yeye kwanini jimbo lake liko kwenye hali duni hivi,miaka yote alikuwa anafanya nini?
mkuu wewe una umri gani?? na umezunguka hii Tanzania kiasi gani?
Kuna wabunge wangapi wamedumu kwenye majimbo yao miaka na miaka lakini hakuna kitu??? Wewe umewahi kuwasikia watu wa Karatu wakilalamika??
Mbona Kikwete anashindwa kutawala hapa Tanzania, lakini anapata ulaji kusuluhisha migogoro huko nchi za watu? Hapa namaanisha kuwa kushindwa kuongoiza watu 2 haimaanishi utashindwa kuwaongoza maelfu.. Kuwa mbunge ni kuwa mwakilishi wa wanajimbo kuna baadhi ya mamlaka unayakosa..Huwezi kuamrisha serikali ijenge miundo mbinu, ila unachoweza kufanya ni kuiomba.
Lakini unapokuwa Rais una mamlaka yote! Unaagiza tu.