Niliyojifunza Kuhusu maisha

magombe junior

JF-Expert Member
Sep 13, 2012
2,015
1,032
Mimi ni mwenyeji kidogo JF,nakumbuka enzi hizo nauliza maswali yakijinga (hili nimekuja kulijua baadae) mpaka sasa nimekua mtu mzima kidogo kuna mambo nimeyafaham na nimeona ni muhimu kuwajuza vijana wenzangu.

Let me share my little experience and facts about life;

1.Usilazimishe jambo/mambo.Mtu akikukataa kwenye kazi au jambo lolote ambalo unaliona kua ndio njia yako pekee yakutoka kwenye maisha achana nae/nalo maana huwezi amini huenda kuna jambo kubwa na zuri zaidi mbele yako linakisubiri.( Nimeshuhudia hili).

2.Usilazimishe mapenzi au mahusiano.Kama kuna jambo la hovyo unaweza kulifanya kwenye maisha yako nikulazimisha mapenzi au mahusiano na mtu.Kimsingi mahusiano huja au hutokea kwa muda sahihi na mtu sahihi.Haijalishi utapaswa kusubir kwa muda gani ila "Never rush into a relationship"

3.Usioe kwa hisia.Kama kuna makosa makubwa kijana anaweza kufanya nikuoa kwa kutumia hisia,kudhani kwa sababu unampenda Hamida basi nisababu yakumuoa.Mariage is a tricky thing,unahitaji sababu za msingi mnoo kumfanya binti awe mke wako.Choose wisely.

Ntaendelea wakati mwingine.
 
Back
Top Bottom