Sehemu ya 4
bhas bhana..baada ya msiba kuisha tukakaa kama siku 3 yanne faza akaondoka mjini tuka baki pale na bimkubwa ..
bimkubwa akasema nimuonyeshe ule mchanga wakizee kichawi..nikamuonyesha akasema nimpe auhifadhi nikampa akasema, kwavile bado yupo yupo kidogo tutaupeleka baada yandugu nawageni wakishaondoka
Bhasi bhana baada ya siku4 dingi akasepa mjini tukabaki na bimkubwa
Tukakaa kusubiri msiba uishe kabisa nawageni wakishaondoka ndo tutaupeleka kwa sangoma.
Bhasi bhana kweli wageni walivyo isha isha bimkubwa akaenda kwa shangazi kidogo..
Nikaitwa kule msibani nirudishe majembe ya yule kizee mchawi nikaleta visingizio nisipeleke nikaambiwa wendo uliyaleta
Ikabid niseme mkono unaniuma sitaweza kubeba mwenyewe
Bhasi nikaambiwa utabeba nahuyu kijana tuka beba kuondoka
Tukafika tuka vikuta vile vizee vimekaa nje ilikuwa mida yaa saa6 hiv mchana..tukasalimia vikasema mmezaliwa wakat mzur
Ketini hapo tule nimda wakula bibi yenu asha ivisha minikadakia asanten sana tumeshiba kale kazee kakasema mbona unamsemea
mwezako ananjaa..kibibi nacho kikadakia kaeni wajukuuzangu jaman mle bibi yenu nimerosti
Kabla cjajibu lile kijana likakaa chap minika mwambia bibi asanten sana ntakula sikunyingine..kale kizee kakasema weka bakuli mbili nasamaki ulete mara 1.
Bibi kakaruka fasta ndani kakatoka navibakuli viwili vyenye samaki mikabla cjaongea kababu kaka nishika mkono kakaniambia kaachini
Kijana wangu ule nikajishangaa nimeketi nikanawa nikaanza kuufinya ugali.
Bhasi bhana tukala ila samaki walikuwa watam balaa baada yakumaliza nikashukuru nikasimama
Ilenataka kuondoka kazee kakasema tulia kijana unaenda wapi nahapa nikwako.
Mkewangu emu mletee maziwa mme mdogo na mwenzake kabibi kakacheka kakaruka ndani chap, kakatoka navikombe viwili kakatupatia tukanywa
Huku kazee kanasema hapa kwangu mtu hawezi kuja wakat wakula akaondoka hivhv bila kula. Huku kibibi kana msapoti mihata sielewi
Nataka kuondoka Bhasi tukamaliza tukaaga tukapiga hatua tatu tukasikia vinacheka na kugongesha mikono nikapotzea tukasepa.
Bhasi tukakaa siku kama mbili tumbo likaanza kuuma uma likawa kama linavimba gesi si gesi..nikawa nakula kidogo nashiba balaa.
Bro akawa ananishangaa dogo mbona siku hz unakula kizungu umegundua nn nkamwambia tumbo linazingua bhasi ikapita hivo
Wakiwa wanapika samaki najiskia vibaya kinyama kichefu chefu nikawa siwezi kula kabisa nakunywa uji tu hivyo hivyo na maji
Iikawa nikienda chooni kukata gogo kudadek gogo halikatiki..nikaona nakufa bimkubwa sahyo hajui naona aibu kusema .bimkubwa atanionaje
Nikaona mficha maradh kifo humuumbua ikabidi nimchane bimkubwa tulienda kwa yule mzee
Akatukaribisha ugali tukala nika mweleza nilivo kaa bila kupenda.
Nikaona bimkubwa kaachini ameshika kichwa akaniambia mwanangu umekwisha mwee.
Bhasi bimkubwa akasema kesho mapema tunaenda kwa mganga
Usiku ukapitaa kibishi bishi asubuh
Bimkubwa akawa anatafta alipo weka ule unyayo wa kichawi..hauoni
Bimkubwa akachanganyikiwaa tafuta tafuta pamoja na bro. Wapi akasema haka kazee kamenipiga changa. Wakatafta mpaka jioni
Huko jioni bimkubwa akacheki uvunguni kwenye kiatu akafanikiwa kuuona mda ukawa umeenda akasema jikaze kesho tutaenda
Usiku huo hakuja lalika tumbo na mimi tumbo tumbo jaman linauma bhasi kuka kucha tuka anza safari.
Lakini tulipo kuwa tutaenda bimkubwa akasema njia zinachanganya mbona tumetembea wee tunajikuta tunatokeapale pale kwanzia saambili mpka sa nne bado,
Tupo palepale bimkubwa akasema.
Hakuna kurudi nyuma
Hapa lazima tufike Leo Leo kaa nisubiri na kuja akaenda akarudi na mdada mmoja akanipa turatura akasema niweke mfukoni kisha. Tukaondoka mdada yuko mbele
Tukafika sehem kuna duka aka mpa yule dada kitu kidogo .akarudi zake
Tuka nunua maji juisi biskut tukala misjala nikanywa maji tu.
Boda Boda ikapita tukasimamisha tukapanda mpaka kwa mganga tukasubir zamyetu tukachoma, ndani bimkubwa wakasalimiana na mganga akamweleza yote
Mganga akapiga manyanga yake akanguruma, akatulia akasema huyu ametupiwa kombora na kale kazee nikachawi kakubwa kiongozi ..
Akasema huyu amelishwa nyama zawatu na damu iliyooza ya fisi alikuwa afe kama mende lakini kutokana nakinga yake namizimu yake ndomaana mpaka sahv bado yupo. Mganga akasema ngoja anitoe uchafu niliolishwa akavuta kibuyu
Akaniambia shika kunywa nikanywa akanipa kindoo aasee nilitapika nilitapika karibu kindoo kijae akavuta kibuyu kingine akanipa nikanywa sijatapika tena hapo nipo hooii. .
Bhasi mganga akasema inaitajika kuku mweupe tuka mpa hela kuku akaletwa..mganga akasema
Wachawi wakianzisha vita nawewe hawakati tamaa watakujia kwanjia yoyote ile mpaka wakunase kama utakata tamaa Umekwisha.
Anasema hatapale tulipo kosea njia nikilekizee kilikuwa kinataka, kuzuia unyayo wake usifike kwake maana nihatar kwake itampunguzia nguvu
Akaendelea kusema kale kazee nikakiongozi kakichaw pande zile ndomaana kanapambana kunichukua ili kaweke heshima kwenye kikundi chao cha babu kunoga.
Bhas mganga akasema ata nipambania kasi nisogelee.
Kwavyovyote vile bhasi mganga akanifunika shuka jeupe akaniambia lala chali akaniwekea kibuyu juu yatumbo akanipa dua zake ,
Kama nusu saa aka niamsha akasema amesha maliza akasema leta huo mchanga iliamfunge asinisogelee aitenganishe unyayo wangu nawake....
Itaendelea seem ya 5( nilivyo tenganishwa na kazee kichawi kwa kuku mweupe na unyayo wake na tulivyo potea njia ya kurudi kwenye korongo la chui) nilisha andika mpaka mwisho sema kwenye ku save nika cancel ikabidi nianze moja nime fupisha fupisha