Nilivyoishi na UKIMWI kwa wiki mbili

Nilivyoishi na UKIMWI kwa wiki mbili

LENDEYSON

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2013
Posts
2,996
Reaction score
2,659
Habari zenu wandugu,

Poleni kwa majukumu ya hapa na pale.

Ijumaa ya tarehe 13 mwezi huu niliamua kwenda kupima Afya yangu hususani VVU kwani nilikuwa na wasi wasi uliosababishwa na ndoto iliyojirudia kama mara 3.Nilifika katika Zahanati 1 hapa jijini ambayo ina huduma ya vijana ya kupima na ushauri nasaha.

Kipimo cha kwanza kilitoa majibu ambayo hayakueleweka. Kile kimstari kinachoonesha kama mtu kaathirika hutoa rangi fulani endapo uko Positive.Kile kimstari kilikuwa kimefifia, hali iliyopelekea kuchukuliwa Kipimo cha aina nyingine.Kipimo hiki cha pili kikaonesha niko Negative.Daktari akashauri nirudi baada ya wiki mbili kwani majibu yanapishana,inabidi waangalie mgongano wa vifaa hivyo.

Cha kwanza hakijatoa jibu, cha pili kimetoa jibu.Hizi wiki mbili tu nimekata kilo nyingi kwa mawazo, nilijikuta nafikiria majibu yale ya kipimo cha kwanza yasiyoeleweka. Nikafikiri vipi kama baada ya wiki mbili ikawa confirmed ni Positive nitaishije mie.

Leo nimeenda ikiwa ni wiki mbili tayari.Dokta kaniambia ingia maabara,akatoa maelezo kwa mtu wa maabara juu ya kilichotokea mwanzo.Nikatolewa damu,baada ya hapo nikaambiwa nisubiri nje. Jasho kila mahali, mapigo ya moyo yakiwa juu, Usiombe hali hii ikukute, unaweza dondoka kwa pressure.

Baadae nikaitiwa majibu yangu, Dokta kaanza kwa kunipa Hongera na pole kwa kilichotokea wiki mbili ilizopita kwani majibu yanaonesha nipo Negative. Nilijihisi kuongezeka kilo kadhaa hapohapo.Njia nzima nilikuwa nikiimba sifa na ukuu wa Mungu.

Zipu haishushwi tena hadi siku iliyokusudiwa.

Namshukuru Mungu hata sasa.

UKIMWI upo na unauwa, usiombe hii hali ya sintofahamu ikutokee.
 
hongera kwa uamuzi wako kupima maambukizi ya VVU, sio mchezo mimi nilikimbia majibu
 
Hongera kwa kupima.
Mijanaume mengi hayapimi kwa kisingizio akipima mkewe inatosha wakati huo huo inamichepuko kila kona!!!!!!!!!
 
Hahahaaaa! Inaonesha kichwa kidogo kimesiz kidizain, ila kinatabu sana hicho coz kikisimama kichwa kikubwa chali.

Hongera kwa mpango mzuri mdau.
 
pole kijana! Ni maamuzi magumu kwa wengine kupima lakini ni muhimu kujitambua. Hongera sana
 
hongera kwa uamuzi wako kupima maambukizi ya VVU, sio mchezo mimi nilikimbia majibu

Nashukuru mkuu. Ila asubuhi wakati wa kwenda almanusura nighairi, ila nikajipa moyo huku Sala na maombi hayapungui kinywani mwangu.
 
punguza mechi za mchangani sasa

Nilicheza moja tu ya mchangani,tena 2013.Na ndo hiyo iliyokuwa inanipa wasiwasi ingawa mwaka jana februari nilikuwa nimepima,hapo ikiwa ni miezi 6 baada ya game hiyo ya mchangani. Since then niliapa kutokucheza rough tena,na sasa hata zipu yangu haitashushwa tena hata utakapofika muda muafaka!
 
hongera kwa hilo....ila tulivyowasaulifu.....baada ya mwaka tu mambo yanarudi.kulekule.....utulie kweli.kama unavyoahidi hapa.....
 
pole kijana! Ni maamuzi magumu kwa wengine kupima lakini ni muhimu kujitambua. Hongera sana

Thanks mkuu. Ni uamuzi ambao nashauri watu waufanye,hasa pale wanapotaka kufanya maamuzi magumu kwenye mipango ya maisha.
Pamoja na sababu niliyoisema, hiyo ilitokana na mimi kutaka kuamua kuanzisha familia,taasisi ambayo naona kuingia huko kunahitaji kujitathmini ipasavyo kuliko kuji disappoint wakati ukifika.
 
Kuzaa sio kazi,, kazi kulea watoto,, na Kupima sio kazi,, kazi kujitunza kaka, mimi nimepima kama mara 6 hivi,, lakin mh
 
Hivi UKIMWI bado ni janga au zimebakia ni hadithi tu za "hapo zamani za kale...."
 
Hahahaaaa! Inaonesha kichwa kidogo kimesiz kidizain, ila kinatabu sana hicho coz kikisimama kichwa kikubwa chali.

Hongera kwa mpango mzuri mdau.

Kimesharudi katika Uimara wake, ila usiombe,hali ilikuwa tata.
Nashukuru, ila c vibaya nawe ukipitia maeneo hayo, ni vyema kumulika afya mara kwa mara.
 
Achana na ngoma, achana na pressure ya kupima. Ukiwa unasubiri majibu unatamani ardhi ipasuke usishuhudie masikio yako...!

Lakini ukijua status yako utaishi na amani moyoni, iwe negative au positive!!!
 
Hongera kwa kupima.
Mijanaume mengi hayapimi kwa kisingizio akipima mkewe inatosha wakati huo huo inamichepuko kila kona!!!!!!!!!

Ni kweli, kati ya mambo magumu kwetu wanaume ni kupima vvu. Hapo utatafuta ugomvi kwa kweli. Hata wanawake nao wajitokeze kupima,hususani wale wasiopo kwenye ndoa.
 
Kimesharudi katika Uimara wake, ila usiombe,hali ilikuwa tata.
Nashukuru, ila c vibaya nawe ukipitia maeneo hayo, ni vyema kumulika afya mara kwa mara.

Presha za ovyo ovyo sipendi. Kule si kuzuri kiasi cha kujipeleka peleka tu.
 
Achana na ngoma, achana na pressure ya kupima. Ukiwa unasubiri majibu unatamani ardhi ipasuke usishuhudie masikio yako...!

Lakini ukijua status yako utaishi na amani moyoni, iwe negative au positive!!!

Kweli. Hicho kipindi ni Pressure tupu, hadi nywele niliambiwa zinatoa jasho, nilikuwa natetemeka,nawaza nini zitakuwa results!
 
Back
Top Bottom