crome20
JF-Expert Member
- Feb 5, 2010
- 1,130
- 721
Kama unatafuta mchumba vigezo na asilimia zake ziwe hivi. Uzuri uwe 60% Tabia 35% mambo mengine kama elimu, n.k 5%. Sababu kuu ni kuwa 60% za uzuri maana ndio chanzo kikuu cha kusisimua mapenzi hatimaye tendo la ndoa. Na kwa sheria ya ndoa TZ kama tendo la ndoa halifanyiki kwa usahihi, ndoa hiyo inaweza kuvunjwa. Pili uzuri ni permanent, huwezi kuubadilisha, zaidi unaweza kuuboresha kwa urembo, lakini uzuri kwa maana ya body morphology huwezi kuubadili tofauti na tabia au elimu ambayo unaweza kuibadili kwa mambo kama mazingira, elimu, exposure, na kuonya. Tabia nimeipa 35% nikiwa na maana awe na reasonable tabia ambayo hataonekana kituko katika jamii japo anaweza akawa na mapungufu kadhaa yanayovumilika na ambayo yanaweza kurekebishika. 5% ya mengineyo ni ziada tu wala hayatakiwi kiwe kikwazo kwa mtu ambaye amepata score ya 95%. Je ndugu zangu mnaonaje ushauri niliompa rafiki yangu? Kumbuka sijataja Jinsia hapa maana ushauri huu kwangu ni any gender. Karibu tujadili . . .