Roadmap
JF-Expert Member
- Aug 19, 2013
- 2,898
- 5,796
Wakuu kwema jamvini siku moja mida ya usiku nikiwa katika speed kali Niligonga binti wa miaka 15 Sikusimama kutokana na eneo kuwa na watu nilivuta gari ila mwisho roho iliniuma sana ivo kupelekea kuahirisha safari baada ya umbali na nikachukua Guest na kulala kesho ndo nkapata nguvu ya kuendelea na safari baada ya wiki moja baada ya kukosa amani ya moyo niliamua kurudi eneo la tukio wakati huu nilitumia public transport Bus nilifika mpaka apo na kushuka nilianza kufanya follow up na hatimae nikampata mhanga niliemjeruhi nilimkuta kavunjika mkono na majeraha madogo madogo bila kujitambulisha nilianza kutoa support japo binti huyo alikuwa tayari alishapewa huduma ya hospital kufupisha story ni mwaka sasa umepita binti niliamua kumsomesha boarding likizo anaenda kwao au aje kwangu mana nimekua baba yake kabisa.. Natamani kumsimulia mkasa mzima ila najiuliza je anaweza kunichukia na kuwa na hasira na mimi naombeni ushauri kwa sasa yupo secondary.