Nilichokiona NHIF

Nilichokiona NHIF

Gama

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
13,264
Reaction score
4,740
Amani iwe nanyi,

Majuzi nikitembelea ofisi za bima ya Afya ya taifa, mambo niliyoyaona yalinifedhehesha mno:

1. Kwenye front desk kulikuwa na Afisa mmoja aliyekuwa akiwapokea wateja na kuwahudumia na ukumbi ulikuwa na watu wengi kiasi kwamba wale walioona kuwa wanachelewa kupata huduma walikuwa wakimkaripia.

2. Wateja waliokuwa wakiwasilisha form zao za kujiunga wanaambiwa wake kuchukua kadi zao baada ya mwezi mmoja, hii ilinistaajabisha ikafanya nijiulize, kwanini kadi ya utambulisho tu ichukue mwezi mmoja wakati taasis nyingine huweza kutoa ID siku hiyohiyo? MF. Backleys bank, kitambulisho cha mpiga kula nk.

3. Wateja waliokuja kuomba vibali vya matibabu kupewa kibali baada ya siku saba, hii ilinistaajabisha zaidi, kwanini vibali visitolewe siku hiyohiyo?

Nashauri mamlaka husika iige mfano wa bima nyingine za Afya mf, Jubilee amabo ukisha sajiliwa unapewa barua maalum ya utambulisho pending kusubiri ID.

Nawasilisha
 
Hilo la 3 ndio limenisikitisha zaidi...
Inakuwaje kama mgonjwa yuko ICU kuna vipimo vinahitajika?
Siku 7???!!!!!
NHIF jirekebisheni...msitake kuendeleza imani kuwa hakuna kitu cha umma chenye ufanishi...mnachukua michango ya watu mtoe huduma kwa wakati...suala la afya si la kusubiri,,,
Mbona zamani hamkuwa hivyo; ...yani mnataka tuseme afadhali ya jana?! Mnataka watu wajigharimie afu mkatae kuwa refund?!
 
Hilo la 3 ndio limenisikitisha zaidi...
Inakuwaje kama mgonjwa yuko ICU kuna vipimo vinahitajika?
Siku 7???!!!!!
NHIF jirekebisheni...msitake kuendeleza imani kuwa hakuna kitu cha umma chenye ufanishi...mnachukua michango ya watu mtoe huduma kwa wakati...suala la afya si la kusubiri,,,
Mbona zamani hamkuwa hivyo; ...yani mnataka tuseme afadhali ya jana?! Mnataka watu wajigharimie afu mkatae kuwa refund?!
Hiyo NHIF ni wasumbufu,na ukienda huko ofisini kwao wako slow sana wamebweteka sana na bado Mr presida atawatumbua tu
 
Hiyo ni kama saccos tu zingine haimsaidii masikini zaidi ya kumnyang'anya hata kidogo alichonacho. unakuta dawa fulani, vipimo fulan hawavilipii ...
 
ase kwel,haijakaa poa kabisa h serikali inatakiwa kuweka utartbu mzuri mbna saiv tupo kidigtal ishu kam hzo ni za kuchkua muda mchache tuu,afu ni suala zito la afya sio la kuendeshwa au kutozingatiwa kias iko.hayo mapunguf yaangaliwe kwa umakini kabsa ase,kwa ajili ya maish yetu.
 
Hawa jamaa wanakera sana,mimi nilikisahau kitambulisho nlipofika ofisini kwao nikaomba wanipe kibali cha matibabu ili nikipata kitambulisho changu niendelee kukitumia,wakanambia wewe umeshapoteza nenda kalete lost report na kalipie bank elfu 20000 ila baada kama ya wiki nikapata kitambulisho changu nawaambia nimeshakipata warudishe pesa yangu wamekataa eti kwamba hawarudishi pesa!!!
 
Amani iwe nanyi,

Majuzi nikitembelea ofisi za bima ya Afya ya taifa, mambo niliyoyaona yalinifedhehesha mno:

1. Kwenye front desk kulikuwa na Afisa mmoja aliyekuwa akiwapokea wateja na kuwahudumia na ukumbi ulikuwa na watu wengi kiasi kwamba wale walioona kuwa wanachelewa kupata huduma walikuwa wakimkaripia.

2. Wateja waliokuwa wakiwasilisha form zao za kujiunga wanaambiwa wake kuchukua kadi zao baada ya mwezi mmoja, hii ilinistaajabisha ikafanya nijiulize, kwanini kadi ya utambulisho tu ichukue mwezi mmoja wakati taasis nyingine huweza kutoa ID siku hiyohiyo? MF. Backleys bank, kitambulisho cha mpiga kula nk.

3. Wateja waliokuja kuomba vibali vya matibabu kupewa kibali baada ya siku saba, hii ilinistaajabisha zaidi, kwanini vibali visitolewe siku hiyohiyo?

Nashauri mamlaka husika iige mfano wa bima nyingine za Afya mf, Jubilee amabo ukisha sajiliwa unapewa barua maalum ya utambulisho pending kusubiri ID.

Nawasilisha
3. Hujaelewa mkuu. Unapewa kibali ambacho kinakuwa valid for 7 days. Ulisikia vibaya mkuu. Ulienda ofisi za wapi??
 
Ila mbona mimi niliwahi kuyaokoa maisha ya mzazi wangu kupitia bima ya afya tena katika hali ya dharura na nilipata kibali cha matibabu kwa haraka bila hata ya usumbufu ila mimi naona ni bora tungefanya uchunguzi kwanza juu ya ukweli wa habari hii jamani
 
Amani iwe nanyi,

Majuzi nikitembelea ofisi za bima ya Afya ya taifa, mambo niliyoyaona yalinifedhehesha mno:

1. Kwenye front desk kulikuwa na Afisa mmoja aliyekuwa akiwapokea wateja na kuwahudumia na ukumbi ulikuwa na watu wengi kiasi kwamba wale walioona kuwa wanachelewa kupata huduma walikuwa wakimkaripia.

2. Wateja waliokuwa wakiwasilisha form zao za kujiunga wanaambiwa wake kuchukua kadi zao baada ya mwezi mmoja, hii ilinistaajabisha ikafanya nijiulize, kwanini kadi ya utambulisho tu ichukue mwezi mmoja wakati taasis nyingine huweza kutoa ID siku hiyohiyo? MF. Backleys bank, kitambulisho cha mpiga kula nk.

3. Wateja waliokuja kuomba vibali vya matibabu kupewa kibali baada ya siku saba, hii ilinistaajabisha zaidi, kwanini vibali visitolewe siku hiyohiyo?

Nashauri mamlaka husika iige mfano wa bima nyingine za Afya mf, Jubilee amabo ukisha sajiliwa unapewa barua maalum ya utambulisho pending kusubiri ID.

Nawasilisha

Amani iwe nawe pia.
Naomba nikupe ushauri kidogo kuhusu malalamiko yako maana mi ni mwanachama mwenzako ambaye bima ya afya umewahi kunisaidia sana.

1. Kila taasisi kuna utaratibu wa kupata huduma. Mwanachama wa bima ya afya anatakiwa afanye maombi ya vitambulisho anapoajiriwa tu au pale anapopewa taarifa na mwajiri wake kuwa michango yake imewasilishwa bima ya afya.....Lakini wengi hupuuzia na kuleta maombi ya kupewa vitambulisho vya dharura pale wabapougua.

2. Pamoja na wengi kupuuzia (1) vitambulisho vya muda hutolewa papo hapo kwa wanachama waajiriwa isipokuwa wale wa Kikoa, Toto Afya kadi na wanachama binafsi.

3. Kuhusu foleni kwenye ofis za bima hua inatokea haswa kwa ofis za dar es salaam but sijawahi kusubiri zaidi ya nusu kwa ajili ya kupewa huduma.

4 Hawa jamaa wa nayo number ya bure kwa wateja wao. Free call ambayo unapopata shida yoyote mahala popote kuhusu huduma za bima ya afya unapiga free of charge na kusaidiwa.
0800 11 0063

Nadhani wote kama tutafuata taratibu zilizopo lawama zitakuwa hakuna.
 
Amani iwe nanyi,

Majuzi nikitembelea ofisi za bima ya Afya ya taifa, mambo niliyoyaona yalinifedhehesha mno:

1. Kwenye front desk kulikuwa na Afisa mmoja aliyekuwa akiwapokea wateja na kuwahudumia na ukumbi ulikuwa na watu wengi kiasi kwamba wale walioona kuwa wanachelewa kupata huduma walikuwa wakimkaripia.

2. Wateja waliokuwa wakiwasilisha form zao za kujiunga wanaambiwa wake kuchukua kadi zao baada ya mwezi mmoja, hii ilinistaajabisha ikafanya nijiulize, kwanini kadi ya utambulisho tu ichukue mwezi mmoja wakati taasis nyingine huweza kutoa ID siku hiyohiyo? MF. Backleys bank, kitambulisho cha mpiga kula nk.

3. Wateja waliokuja kuomba vibali vya matibabu kupewa kibali baada ya siku saba, hii ilinistaajabisha zaidi, kwanini vibali visitolewe siku hiyohiyo?

Nashauri mamlaka husika iige mfano wa bima nyingine za Afya mf, Jubilee amabo ukisha sajiliwa unapewa barua maalum ya utambulisho pending kusubiri ID.

Nawasilisha
Tatizo wamelewa pesa hao watu....hata mikoani wanaringa sana kutoa huduma zao na wanakua na lugha chafu kwa wateja......especially kuna manager wa moro anamajibu ya hovyo kwa kigezo kuwa anatembea na moja wa wakurugenzi huko juu.

Sasa permit ya matibabu watoe baada ya siku 7 si mgonjwa anaweza kufa njiani hapo.
 
Tatizo wamelewa pesa hao watu....hata mikoani wanaringa sana kutoa huduma zao na wanakua na lugha chafu kwa wateja......especially kuna manager wa moro anamajibu ya hovyo kwa kigezo kuwa anatembea na moja wa wakurugenzi huko juu.

Sasa permit ya matibabu watoe baada ya siku 7 si mgonjwa anaweza kufa njiani hapo.

Ndugu ...Nadhani ukifuata yaliyoelezwa hapo juu huduma za Nhif zitakua rahisi sana kwako. Tatizo watanzania tunapenda sana last minutes na hatupendi kufuata taratibu. Kwa nini usubirie kuugua ndo ukaombe kutambulisho cha dharura? Jaza form yako mapema upewe kitambulisho chako mapema
 
Kibali ndani ya siku 7?

Kibali hutolewa ndani ya dkk chache tu mbona...any way kwa kuwa umeshuhudia sawa...lakini kwa uzoefu wangu hao jamaa sijawahi kukwama kwenye ishu ya kibali.
 
3. Hujaelewa mkuu. Unapewa kibali ambacho kinakuwa valid for 7 days. Ulisikia vibaya mkuu. Ulienda ofisi za wapi??
Sure itakuwa alisikia tofauti..kibali NHIF wanatoa right away....ukiwa na passport size picha ya mgonjwa na uthibitisho tu bas.
 
Ndugu, Katika hoja zako hoja ya 3. haijakaa vema. Kibali ni ishu ya madakika tu ukiwa na vithibitisho kutoka hospitali husika. nimetumia huduma za hawa jamaa toka 2016. Na kuna wakati huduma zilisogezwa katika hospitali kubwa.

Pengine mambo yamebadilika. Japo pia kuna kero ndogondogo ambazo hazikwepeki!

Amani iwe nanyi,

Majuzi nikitembelea ofisi za bima ya Afya ya taifa, mambo niliyoyaona yalinifedhehesha mno:

1. Kwenye front desk kulikuwa na Afisa mmoja aliyekuwa akiwapokea wateja na kuwahudumia na ukumbi ulikuwa na watu wengi kiasi kwamba wale walioona kuwa wanachelewa kupata huduma walikuwa wakimkaripia.

2. Wateja waliokuwa wakiwasilisha form zao za kujiunga wanaambiwa wake kuchukua kadi zao baada ya mwezi mmoja, hii ilinistaajabisha ikafanya nijiulize, kwanini kadi ya utambulisho tu ichukue mwezi mmoja wakati taasis nyingine huweza kutoa ID siku hiyohiyo? MF. Backleys bank, kitambulisho cha mpiga kula nk.

3. Wateja waliokuja kuomba vibali vya matibabu kupewa kibali baada ya siku saba, hii ilinistaajabisha zaidi, kwanini vibali visitolewe siku hiyohiyo?

Nashauri mamlaka husika iige mfano wa bima nyingine za Afya mf, Jubilee amabo ukisha sajiliwa unapewa barua maalum ya utambulisho pending kusubiri ID.

Nawasilisha
 
kwanini kadi ya utambulisho tu ichukue mwezi mmoja wakati taasis nyingine huweza kutoa ID siku hiyohiyo? MF. Backleys bank, kitambulisho cha mpiga kula nk.


Hiyo NHIF ni mgogoro mwingine unaowapa ulaji watu wachache, mimi nashauri hizo kadi ziwe digital na ziwe synchronized na mfumo wa malipo wa hazina, ili mnufaika akishafikisha vielelezo vyake, palepale inaingizwa kwenye mfumo na kutoa hati ya muda ya utambulisho, then baada ya siku chache inatengeneza smart card ambayo itatumika kwa kulambisha kwenye machine maalumu kwa mtoa huduma na kufanya deductions moja kwa moja badala ya makaratasi mengi yanayoongeza gharama za uendeshaji bila sababu,

Mbona mifumo hiyo inafanya kazi kwenye mabenki, vituo vya mafuta nk, why not ninyi NHIF, mna maslahi gani binafsi kwenye huo urasimu wenu?
 
Amani iwe nanyi,

Majuzi nikitembelea ofisi za bima ya Afya ya taifa, mambo niliyoyaona yalinifedhehesha mno:

1. Kwenye front desk kulikuwa na Afisa mmoja aliyekuwa akiwapokea wateja na kuwahudumia na ukumbi ulikuwa na watu wengi kiasi kwamba wale walioona kuwa wanachelewa kupata huduma walikuwa wakimkaripia.

2. Wateja waliokuwa wakiwasilisha form zao za kujiunga wanaambiwa wake kuchukua kadi zao baada ya mwezi mmoja, hii ilinistaajabisha ikafanya nijiulize, kwanini kadi ya utambulisho tu ichukue mwezi mmoja wakati taasis nyingine huweza kutoa ID siku hiyohiyo? MF. Backleys bank, kitambulisho cha mpiga kula nk.

3. Wateja waliokuja kuomba vibali vya matibabu kupewa kibali baada ya siku saba, hii ilinistaajabisha zaidi, kwanini vibali visitolewe siku hiyohiyo?

Nashauri mamlaka husika iige mfano wa bima nyingine za Afya mf, Jubilee amabo ukisha sajiliwa unapewa barua maalum ya utambulisho pending kusubiri ID.

Nawasilisha
Hakuna kitu hapo, ni uzushi mtupu. Kupata kadi ya mwanangu ilichukua miezi miwili, na hapo baada ya kupiga sana kelele.
Inawezekana tayari washakuwa Mufilisi, wanashindwa tu kusema ukweli.
 
Back
Top Bottom