MR MAJANGA
JF-Expert Member
- Oct 4, 2014
- 3,524
- 10,817
Leo wakati nipo ferry nimeshuhudia kitu cha kusikitisha, licha rais wetu anajitahidi kudhibiti rushwa na kukusanya mapato, lakini kuna watz wachache wamethibitisha mtoto wa haramu hata umfiche ndani ya chupa atatoa kidole tu ili kuonyesha uwepo wake.
Ni hivi, nimefika ferry mwanzoni kabisa nakutana na geti na kibanda cha kukatia tiketi, nikalipa nauli nikapewa tiketi iliyochapwa kwa kompyuta. Nikaingia ndani nakutana na kijana ambaye anakusanya zile tiketi na kuzimulika ( jina silijui) na kitu kama sensor fulani ambazo husoma zile tarakimu na kuziingiza kwenye mfumo wa ukusanyaji mapato pale kivukoni,
Sasa huyu jamaa anachokifanya ni kukusanya tiketi kama kumi halafu anaimulika ya juu tu halafu anazichana, kwa hiyo zile tisa za chini zinakuwa hazijaingizwa kwenye kompyuta kuonyesha kuwa tiketi zile zimenunuliwa.
Nashauri kuwe na mashine ambazo ikitoa tiketi isome moja kwa moja bila kuhitaji mtu wa pili wa kumulika kama zile za madukani.
Ni hivi, nimefika ferry mwanzoni kabisa nakutana na geti na kibanda cha kukatia tiketi, nikalipa nauli nikapewa tiketi iliyochapwa kwa kompyuta. Nikaingia ndani nakutana na kijana ambaye anakusanya zile tiketi na kuzimulika ( jina silijui) na kitu kama sensor fulani ambazo husoma zile tarakimu na kuziingiza kwenye mfumo wa ukusanyaji mapato pale kivukoni,
Sasa huyu jamaa anachokifanya ni kukusanya tiketi kama kumi halafu anaimulika ya juu tu halafu anazichana, kwa hiyo zile tisa za chini zinakuwa hazijaingizwa kwenye kompyuta kuonyesha kuwa tiketi zile zimenunuliwa.
Nashauri kuwe na mashine ambazo ikitoa tiketi isome moja kwa moja bila kuhitaji mtu wa pili wa kumulika kama zile za madukani.