Nilichojifunza leo katika Ibada ya Ijumaa Kuu

Nilichojifunza leo katika Ibada ya Ijumaa Kuu

Abraham Lincolnn

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2018
Posts
3,157
Reaction score
6,039
Mimi ni muumini wa Kanisa Katoliki na siku ya Leo ni siku ya amri ya kanisa, Kwamba ni lazima kuhudhuria misa ya Ijumaa kuu.

Katika Ibada ya Ijumaa kuu moja ya sehemu ya Ibada ni maombi mbalimbali yanayotolewa kuyaombea mataifa, viongozi wa dini na serikali, walegevu wa imani, wasiomwamini Mungu, Wenye vita, Njaa n.k

Ni kweli kwamba wapo wahubiri wanaoliombea Taifa kwa ujumla lakini hapa ninazungumzia kumwombea yule ambaye anaonekana kutofautiana kwa namna moja ama nyingine kwa zaidi ya mara moja. Tena kwa kumtaja wazi.

Leo katika Ibada moja kati ya maombi yaliyotajwa ilikuwa kuwaombea waumini wote wa madhehebu mengine ya kikristu.

Nikawaza, Moja kati ya kanisa linaloongoza kwa kushambuliwa na madhehebu mengine ni hili la RC likishutumiwa kwa mambo mbalimbali kama vile kubadili Sabato, kuitwa mpinga Kristu n.k Lakini pamoja na yote bado Kanisa linawaombea na kuwakumbuka waumini wote wakristu na madhehebu yao popote walipo.

Jambo hili limenifunza unyenyekevu wa hali ya juu kama muumini wa Kristu ni jambo la muhimu na la pekee sana.Hata pale unapodhulumiwa na kushitakiwa kwa uongo ukiwa kama Mkristu unapaswa kuwa mnyenyekevu kama jinsi Kristu alivyokuwa mnyenyekevu hata pale aliposhtakiwa kwa uongo, Kanisa linatufundisha kuwa wanyenyekevu daima.

Nawatakia Ijumaa Kuu Njema na Maandalizi Mema Ya Pasaka
 
Mkuu unashangaa RC kuwaombea waumini wengine wa kikristu nakuona kama hiyo ni Love?

Unaelezeaje kundi lingine lililosahaulika kwenye hayo maombi ambalo sio la kikristu?

Mwakasege, Gwajima na mzee wa upako nimewashuhudia wakiliombea taifa yani ni sala iliyohusisha watanzania wote wa dini zote na wasio na dini dhidi ya shetani

Hii kwako unaichukuliaje mzee?
 
Mkuu unashangaa RC kuwaombea waumini wengine wa kikristu nakuona kama hiyo ni Love?

Unaelezeaje kundi lingine lililosahaulika kwenye hayo maombi ambalo sio la kikristu?

Mwakasege, Gwajima na mzee wa upako nimewashuhudia wakiliombea taifa yani ni sala iliyohusisha watanzania wote wa dini zote na wasio na dini dhidi ya shetani

Hii kwako unaichukuliaje mzee?
Ni kweli kwamba wapo wahubiri wanaoliombea Taifa kwa ujumla lakini hapa ninazungumzia kumwombea yule ambaye anaonekana kutofautiana kwa namna moja ama nyingine kwa zaidi ya mara moja.Tena kwa kumtaja wazi.
 
Mkuu unashangaa RC kuwaombea waumini wengine wa kikristu nakuona kama hiyo ni Love?

Unaelezeaje kundi lingine lililosahaulika kwenye hayo maombi ambalo sio la kikristu?

Mwakasege, Gwajima na mzee wa upako nimewashuhudia wakiliombea taifa yani ni sala iliyohusisha watanzania wote wa dini zote na wasio na dini dhidi ya shetani

Hii kwako unaichukuliaje mzee?
Bwashee, kipo kipengele cha kuwaombea wapagani, wasio muamini Mungu nk.
 
Ndugu yangu, bila haya mathehebu yanayoibuka hivi sasa Amani ingekua zaidi ya sasa.
Niseme kweli Roman Katoric, ni dhehebu pekee kongwe Tanzania kuliko yote, pia ni dhehebu pekee, unaona muumini anachokitoa kinaelekezwa kuisadia jamii siyo mtu.
 
Mkuu unashangaa RC kuwaombea waumini wengine wa kikristu nakuona kama hiyo ni Love?

Unaelezeaje kundi lingine lililosahaulika kwenye hayo maombi ambalo sio la kikristu?

Mwakasege, Gwajima na mzee wa upako nimewashuhudia wakiliombea taifa yani ni sala iliyohusisha watanzania wote wa dini zote na wasio na dini dhidi ya shetani

Hii kwako unaichukuliaje mzee?
Wote hao wameombewa leo.
 
Mimi ni muumini wa Kanisa Katoliki na siku ya Leo ni siku ya amri ya kanisa, Kwamba ni lazima kuhudhuria misa ya Ijumaa kuu.

Katika misa ya Ijumaa kuu moja ya sehemu ya Liturjia ya misa ni maombi mbalimbali yanayotolewa kuyaombea mataifa,viongozi wa dini na serikali,walegevu wa imani , wasio mwamini Mungu,Wenye vita,Njaa n.k
Ni kweli kwamba wapo wahubiri wanaoliombea Taifa kwa ujumla lakini hapa ninazungumzia kumwombea yule ambaye anaonekana kutofautiana kwa namna moja ama nyingine kwa zaidi ya mara moja.Tena kwa kumtaja wazi.

Leo katika misa moja kati ya maombi yaliyotajwa ilikuwa kuwaombea waumini wote wa madhehebu mengine ya kikristu.

Nikawaza, Moja kati ya kanisa linaloongoza kwa kushambuliwa na madhehebu mengine ni hili la RC likishutumiwa kwa mambo mbalimbali kama vile kubadili Sabato,Kuitwa mpinga Kristu n.k Lakini pamoja na yote bado Kanisa linawaombea na kuwakumbuka waumini wote wakristu na madhehebu yao popote walipo.

Jambo hili limenifunza unyenyekevu wa hali ya juu kama muumini wa Kristu ni jambo la muhimu na la pekee sana.Hata pale unapodhulumiwa na kushitakiwa kwa uongo ukiwa kama mkristu unapaswa kuwa mnyenyekevu kama jinsi Kristu alivyokuwa mnyenyekevu hata pale aliposhtakiwa kwa uongo, Kanisa linatufundisha kuwa wanyenyekevu daima.

Nawatakia Ijumaa Kuu Njema na Maandalizi Mema Ya Pasaka
Katoliki ni mbuyu usiotikiswa na vingedele vipitavyo
 
Ukristo ni dini ya upendo..ndio msingi wake mkuu..achana na ile ya wavaa suicide vest.

Tunahimizwa kuwapenda na kuwaombea wote hata maadui zetu na wanao tuchukia.

Bwana Yesu asifiwe.

#MaendeleoHayanaChama
 
Ukristo ni dini ya upendo..ndio msingi wake mkuu..achana na ile ya wavaa suicide vest.

Tunahimizwa kuwapenda na kuwaombea wote hata maadui zetu na wanao tuchukia.

Bwana Yesu asifiwe.

#MaendeleoHayanaChama
Siyo wakristo au madhehebu yote, isitoshe inaonyesha hujasoma alichokiandika ukaelewa.

Rudia kusoma ulichoandika, kama utaona upendo ulio uandika, Romani Catoric KKT, na Wasabato wale wa mwanzo, ndiyo madhebu yenye upendo yapo kwa ajili ya Mungu.

Hawahubili chuki zidi ya wengine ili kuvuna wafuasi hapana.
 
Mimi nilichojifunza leo ni kwamba mara ya mwisho kwenda ijumaa kuu ni wakati wa mafundisho ya kipaimara mwaka 2008.
Yaani hii ibanda nilikuwa nimeshaisahau kabisa.

Pia mimi nimeshangaa kwamba kanisa linawaombea wale wanaolipinga.
 
Mzee wa mpako aliwahi kusema "ukiona Mchungaji wa madhehebu mengine analisemea dhehebu la Roma vibaya huyo ana matatizo kwani Roman Catholic ndio msingi wa madhehebu yote ya kikristu" mwisho wa nukuu
 
Nakupa homework.
Katafute maana ya Neno KANISA kibiblia.
Na wewe katafute nani alitoa amri watu wapumzike ijumaa kuu kwenye biblia

Nani alitoa amri watu washerekee Christmass na siku ya boxing day wa napumzika tena

Ukipata majibu njoo
 
Mimi ni muumini wa Kanisa Katoliki na siku ya Leo ni siku ya amri ya kanisa, Kwamba ni lazima kuhudhuria misa ya Ijumaa kuu.

Katika misa ya Ijumaa kuu moja ya sehemu ya Liturjia ya misa ni maombi mbalimbali yanayotolewa kuyaombea mataifa,viongozi wa dini na serikali,walegevu wa imani , wasio mwamini Mungu,Wenye vita,Njaa n.k
Ni kweli kwamba wapo wahubiri wanaoliombea Taifa kwa ujumla lakini hapa ninazungumzia kumwombea yule ambaye anaonekana kutofautiana kwa namna moja ama nyingine kwa zaidi ya mara moja.Tena kwa kumtaja wazi.

Leo katika misa moja kati ya maombi yaliyotajwa ilikuwa kuwaombea waumini wote wa madhehebu mengine ya kikristu.

Nikawaza, Moja kati ya kanisa linaloongoza kwa kushambuliwa na madhehebu mengine ni hili la RC likishutumiwa kwa mambo mbalimbali kama vile kubadili Sabato,Kuitwa mpinga Kristu n.k Lakini pamoja na yote bado Kanisa linawaombea na kuwakumbuka waumini wote wakristu na madhehebu yao popote walipo.

Jambo hili limenifunza unyenyekevu wa hali ya juu kama muumini wa Kristu ni jambo la muhimu na la pekee sana.Hata pale unapodhulumiwa na kushitakiwa kwa uongo ukiwa kama mkristu unapaswa kuwa mnyenyekevu kama jinsi Kristu alivyokuwa mnyenyekevu hata pale aliposhtakiwa kwa uongo, Kanisa linatufundisha kuwa wanyenyekevu daima.

Nawatakia Ijumaa Kuu Njema na Maandalizi Mema Ya Pasaka
Zaburi 95:6-7
[6]Njoni, tuabudu, tusujudu,
Tupige magoti mbele za BWANA aliyetuumba.
[7]Kwa maana ndiye Mungu wetu.

Siku ya ijumaa ni siku ya kuombea viongozi wa kanisa na serikali. Sababu kuu ni Yesu-mnazareth alihukumiwa kutokana na fitina na viongozi wa dini na serikali, hiii inaamanisha tunapaswa kuwaombea viongozi wetu ili watuongoze vyema. Mifalakano na madhehebu inatokana na Tamaa mbalimbali za viongozi tu na migogoro ya kijamii mingi inatokana na Tamaa mbalimbali za viongozi wa serikali.

Nimuhimu kuwaombea wenye mamlaka kwa maana wananafasi ya kuyatumia vibaya na kuleta shida.

Mathayo 26:59
[59]Basi wakuu wa makuhani na baraza yote wakatafuta ushuhuda wa uongo juu ya Yesu, wapate kumwua;
 
Shida ipo hapa Roman Catholic wao sijui wana kipaji gani cha kujua hata yatakayotokea kesho?kwa ufupi ibilisi huwa anapita kwenye ukweli halafu anapenyeza ka mtego kake ili ukiingia tu anaenda kushtaki kwa Mungu,kumbuka ibilisi ndio mfalme wa Dunia ambae anazijua siri za ufalme wa mungu tusubiri siku 2300 zitimie.
 
Mkuu hebu nitajie ni amri ya ngap inasema hudhuria misa ijumaa kuu?
 
Back
Top Bottom