Nilibahatika sikupitia njia hii ila najua ni njia inayowaumiza sana watoto kisaikolojia na kuwaacha na chuki kwa wazazi

Fohadi

JF-Expert Member
Jul 24, 2020
770
2,408
Kuna mambo yanafanyika ila athari zake huja huonekana baada ya muda mrefu sana..Ukifatilia asilimia kubwa watoto wanakuwa na migogoro na baba zao kuliko mama zao. Yaani ukisikia mtoto ana bifu na mzazi mmoja au amemtelekeza, basi asilimia 99% ya mzazi aliyetelekezwa anakuwa ni Baba. Moja kwa moja hisia za wengi huwa tunawaza kuwa mtoto amelishwa sumu na mama yake, au baba alikataa ujauzito na majukumu. Huenda huwa tupo sahihi kwa hypothesis zetu lakini sio mara zote huwa tunakuwa sahihi. Leo nimegundua sababu nyingine.

Nina rafiki yangu ambae tumekua wote na tulisoma wote hadi kidato cha nne. Baada ya hapo tukapotezana hadi tulipokutana wikendi iliyopita. Tukaanza kupiga story na kukumbushana matukio ya nyuma hasa hasa pale shuleni kwa wajeda...waliosoma hizi shule watanielewa.

Ilikuwa moment nzuri kukutana na rafiki yangu na tulifurahi sana kukumbuka past zetu..Tulivyoanza serious talk, nikagundua jamaa hana time kabisa na baba yake mzazi. Yeah, mshikaji yuko well off kimaisha na yupo kitengo kizuri sana. Sikutarajia kukuta jamaa anamchukia baba yake kwa jinsi ambavyo naijua familia yao kumbe kuna vitu vingi sana sivijui..Nikamdadisi jamaa kwa hiari yake kama hatojali anaweza share na mimi then niweze kumpa ushauri..Aliamua kufunguka na kuniambia sababu kuu ya kumchukia Baba yake.

Kipindi anakua, ameshuhudia mara kibao Baba yake akimpiga mama yao..Yaani Mzee alikuwa anampiga mama mbele ya watoto..Ile hali imemtesa sana jamaa kisaikolojia kiasi kwamba hadi leo amekua bado anamchukia Baba yake na hana time nae..Amejitahidi kusahau na kusamehe ila zile taswira za kilio cha mama huwa zinamrudia na kumuumiza sana nafsi..Amejiapiza hatakuja kumpiga mkewe mbele ya watoto maana impacts zake ni kubwa sana..Ameniahidi kusamehe, kusahau na kujitahidi kumpa heshima mzee wake.

Nakuja sasa kwenu wakuu. Hivi unaanzaje kumpiga mkeo mbele ya watoto wenu. Unadhani watoto wanajisikiaje? Aisee, chuki na visasi vyao huwa zinadumu muda mrefu sana. Hata kama ni hasira basi kuna namna mnaweza tafuta solution ila sio mbele ya watoto. Basi stress zikiziwazidi sana Hamieni Yanga.

Mimi nashukuru sijawahi kushuhudia haya matukio.

Nawasilisha.

Mzee Mpili na Rais watakuwepo Kigoma tarehe 25.
 
Amekua au bado mvulana?? Anaisha na mwanamke?

Hajawahi mchapa mwanamke yoyote hata kibao??
Kama hajawahi good for him ila kama keshawahi ajue huyo mwanamke ni mama wa mtu na yeye atachukiwa tu.

Hawa watoto wakifanikiwa ndio wanajifanya wanachuki ma wazazi
PUMBAAAAAVU SANA.

Ndio mambo ya akina SADALA
 
Amekua au bado mvulana?? Anaisha na mwanamke?

Hajawahi mchapa mwanamke yoyote hata kibao??
Kama hajawahi good for him ila kama keshawahi ajue huyo mwanamke na mama wa mtu. na yeye atachukiwa tu.

Hawa watoto wakifanikiwa ndio wanajifanya wanachuki ma wazazi
PUMBAAAAAVU SANA.

Ndio mambo ya akina SADALA
Mara nyingine tatizo sio kumpiga ila kumpiga mbele ya watoto. Kama baba wa huyo jamaa angekua anampiga mama yake chumbani unafikiri huyo jamaa angejuaje? Kumpiga tu mwanamke sio vzr lakni kumpiga mwanamke mbele ya watoto wenu ni kumdhalilisha kukubwa mno.
 
Mara nyingine tatizo sio kumpiga ila kumpiga mbele ya watoto. Kama baba wa huyo jamaa angekua anampiga mama yake chumbani unafikiri huyo jamaa angejuaje? Kumpiga tu mwanamke sio vzr lakni kumpiga mwanamke mbele ya watoto wenu ni kumdhalilisha kukubwa mno.
😇
 
Mara nyingine tatizo sio kumpiga ila kumpiga mbele ya watoto. Kama baba wa huyo jamaa angekua anampiga mama yake chumbani unafikiri huyo jamaa angejuaje? Kumpiga tu mwanamke sio vzr lakni kumpiga mwanamke mbele ya watoto wenu ni kumdhalilisha kukubwa mno.
Umeongea point kubwa sana mkuu
 
Nimesoma mkuu na nimeelewa sana..Hoja yako ipo tofauti kidogo na hii niliyoileta..Yako imebase katika kukemea tabia ya watoto kuamini kila kitu baada ya kulishwa 'sumu' na mama zao..Lakini hii yangu inaonesha au inazungumzia ile hali ya Baba kumpiga mama mbele ya mtoto...I mean huku mtoto akishuhudia..inaumiza sana saikolojia ya mtoto...

Huu uzi uliouweka unazungumzia kitu kingine tofauti na hiki..By the way, uzi wako una madini sana.
 
Binafsi na mimi niko na hii hali,simkubali kabisa mzee wangu kwani sijawahi kuyajua mapenzi yake kwangu wala malezi yake ningali mdogo...mama hakuniambia mambo mengi kuhusu baba ila nilipomaliza darasa la saba na kwenda kwake ili ikiwezekana aniendelele kielimu ilitosha kabisa kunionyesha baba yangu ananichukuliaje.

Alisomesha watoto wake wengine na kuwajali pia...mambo yake yalipoanza kuyumba aliamua kuuza nyumba yake (Tandale) na akawapa watoto wake wengine (wadogo zangu) almost 2M kila mmoja but mimi sikukumbukwa hata kwa buku.

Watoto aliowathamini leo hii hawamjali,mzee ameamua kurudi kwangu na kuhitaji msaada kila leo..mimi mwenyewe sina kipato cha kutosheleza maana nakomaa na wanangu wapate elimu iliyo bora.

Inafika mahali sipokei kabisa simu zake,najitahidi kusahau na kusamehe lakini kutokana na niko na kipato duni inakuwa ngumu sana kusahau aisee.
 
Shukrani sana mkuu kwa matusi yako..umepewa busara lakini unaamua kuitumia kumtukana mtu ambae hata hajakutukana au hajatumia lugha ya matusi dhidi yako au dhidi ya yeyote humu ndani...Hivi akili yako ipo sawa kweli?
Nina stress mkuu, nisamehe.
 
Huyo chalii yako bado mvulana, ngoja akinyooshwa na mkewe akili zitamrejea.
 
Kuna mambo yanafanyika ila athari zake huja huonekana baada ya muda mrefu sana..Ukifatilia asilimia kubwa watoto wanakuwa na migogoro na baba zao kuliko mama zao...Yaani ukisikia mtoto ana bifu na mzazi mmoja au
Kabla sijaoa niliwaona wanaume wote waliooa ambao wanawapiga wake zao hawana akili na wala hawana upendo kwa wake zao, nilipoingia kwenye ndoa nikagundua walikuwa na akili na mapenzi ya dhati, ila za kuambiwa changanya na zakwako
 
Back
Top Bottom