Ghaysh
Member
- Feb 12, 2015
- 33
- 58
NILIAHIDI NATEKELEZA.
Tunaanzia mbali kidogo kujenga msingi....
Katikati ya umri wa kuhitaji malezi bora yanayohusisha wazazi wote wawili, baba na mama yake wanafarakana kiasi cha kufikia kutengana... Hali hii inamuweka kwenye wakati mgumu wa wapi aelekee... Mchungaji Philemon Ndelemu anabeba jukumu la kumchukua na kumfanya sehemu ya familia yake kwa kumpatia malezi anayostahili mtoto...
Miaka inasogea... umri unachochea kuni... ujana (Maji ya moto) unafikia fukuto la nyuzi joto (⁰C) 100... Maswali 39 ya ujana yanaanza kufanya ziara kwenye kichwa chake na kujikuta anaanza safari ya kutafuta majibu ili afikie jawabu...
Kijeba cha mtu kinaingia mtaani kujitafuta... kinakula nondo (kunyanyua vyuma) mitaa ya mchikichini kujenga na kuimarisha mwili.... anakula dili za ubaunsa kwenye milango ya nyumba za starehe... anajiongeza kucheza michezo ya kutumia nguvu za mwili kuonesha uwezo mkubwa alionao... anakuwa kama Power Mabula, ananyanyua na kuvuta vitu vizito kwa meno...
Anaona haitoshi anaamua kuwa Mandonga wa enzi hizo... Mwili na utundu unamruhusu kurusha apakati panchi za maana... anazoea ringi anakuwa mwanamasumbwi... anapigana ndondi mapambano kadhaa mpaka anatolewa meno... Anaona cha kufia ilingoni nini? Anaamua kubadili harakati za kutafuta hela kwani anazitaka tena nyingi...
Katika yale maswali 39 ya ujana anapata jibu la swali moja... "BORA KUISHI PAKA PARIS UFARANSA KULIKO MTU TANZANIA". Harakati za kuiacha Tanzania bila hati ya kusafiria zinaanza... Njia pekee ni zile za panya kwenye mipaka isiyo na ulinzi...
Inatafutwa kwanza SA (Afrika Kusini) [emoji1221] kupitia Malawi [emoji1156], nashindikana... Inajaribiwa njia ya Zambia [emoji1268] kupitia Tunduma, inashindikana...
Inawekwa kambi Chunya na shughuli za kuchimba madini zinashika hatamu... inatafutwa dhahabu kwa jasho, mzuka wa madini unakolea kambi inahamia Congo [emoji1078], mambo yanakuwa si mambo shughuli zinahamia Arusha kuyasaka madini adhimu zaidi Duniani, Yes... Tanzanite.
Wakati shughuli za migodi zinaendelea huku akijiona kama nataka anafulia zaidi, mwamba anajitafuta zaidi... anakumbuka anacho kipaji kingine kinachoweza kumuongezea kipato, naam kipaji cha Kuchora na kuchonga Vinyago... anaanza kujitendea haki kwa kuchonga Vinyago na kuvitega kwenye mahoteli makubwa ikiwemo Kilimanjaro Hotel [emoji545] Arusha...
Richard Hananja ndilo jina lake maarufu kwa sasa, Mchungaji fulani mtukutu sana wa maneno.... wakati huo anakijulikana kwa jina la Richie na sasa unaweza kumuita Richie Bilionea...
Hakuna maisha ya kijanja na utukutu wakati huo Richie hajapitia... Ofisi za vyombo vya dola ilikuwa sehemu ya maisha yake kwa kukamatwa mara kadhaa kwenye mampambano ya maisha... Moja ya matukio asiyo yasahau ni pamoja na wakati Nchi ya Tanzania inapitia msoto mkali yeye alikuwa miongoni mwa watu wanaokula bata kiana... Wakati huo kuvaa jeans [emoji158] tu unaweza kupewa mke bure. Alishawahi kukamatwa na kushitakiwa kwa kukutwa na Sabuni, Dawa ya mswaki na mafuta ya kupakaa...
Na kuonesha siyo bahati mbaya mahakamani alitinga akiwa amevalia kinachofuata sana Shati kali, Jeans ya maana na Raba mamtoni imesimama hiviii... Anasema hakimu mwenyewe alipomuona tu akamuelewa na akampa dhamana kibabe sana...
Pamoja na utukutu wake wote Richie hakuwa mtumiaji wa kilevi chochote na kwa mujibu wake ni kwamba akiwa kawaida tu anajiona basi limewaka sasa akiongeza kilevi itakuwaje? Hivyo busara kwake ikawa kutojiingiza kwenye matumizi ya vileo ili ndoto yake ya kuwa bilionea itimie kwa nidhamu... Hii ilimsaidia kuweza kumiliki viwanja maeneo ya Pugu Kajiungeni karibu na Kanisa. Alifanikiwa kujenga nyumba na kwa kuwa alililelewa katika misingi ya Kikristo basi akiwa Pugu kwake alikuwa anapenda kuhudhuria zaidi Kanisani. Na safari ya Uchungaji ikaanzia hapa kwa ushawishi mkubwa wa nje huku msukumo wa ndani nao ukiitikia....
Itaendelea...
Timothy Levy
Tunaanzia mbali kidogo kujenga msingi....
Katikati ya umri wa kuhitaji malezi bora yanayohusisha wazazi wote wawili, baba na mama yake wanafarakana kiasi cha kufikia kutengana... Hali hii inamuweka kwenye wakati mgumu wa wapi aelekee... Mchungaji Philemon Ndelemu anabeba jukumu la kumchukua na kumfanya sehemu ya familia yake kwa kumpatia malezi anayostahili mtoto...
Miaka inasogea... umri unachochea kuni... ujana (Maji ya moto) unafikia fukuto la nyuzi joto (⁰C) 100... Maswali 39 ya ujana yanaanza kufanya ziara kwenye kichwa chake na kujikuta anaanza safari ya kutafuta majibu ili afikie jawabu...
Kijeba cha mtu kinaingia mtaani kujitafuta... kinakula nondo (kunyanyua vyuma) mitaa ya mchikichini kujenga na kuimarisha mwili.... anakula dili za ubaunsa kwenye milango ya nyumba za starehe... anajiongeza kucheza michezo ya kutumia nguvu za mwili kuonesha uwezo mkubwa alionao... anakuwa kama Power Mabula, ananyanyua na kuvuta vitu vizito kwa meno...
Anaona haitoshi anaamua kuwa Mandonga wa enzi hizo... Mwili na utundu unamruhusu kurusha apakati panchi za maana... anazoea ringi anakuwa mwanamasumbwi... anapigana ndondi mapambano kadhaa mpaka anatolewa meno... Anaona cha kufia ilingoni nini? Anaamua kubadili harakati za kutafuta hela kwani anazitaka tena nyingi...
Katika yale maswali 39 ya ujana anapata jibu la swali moja... "BORA KUISHI PAKA PARIS UFARANSA KULIKO MTU TANZANIA". Harakati za kuiacha Tanzania bila hati ya kusafiria zinaanza... Njia pekee ni zile za panya kwenye mipaka isiyo na ulinzi...
Inatafutwa kwanza SA (Afrika Kusini) [emoji1221] kupitia Malawi [emoji1156], nashindikana... Inajaribiwa njia ya Zambia [emoji1268] kupitia Tunduma, inashindikana...
Inawekwa kambi Chunya na shughuli za kuchimba madini zinashika hatamu... inatafutwa dhahabu kwa jasho, mzuka wa madini unakolea kambi inahamia Congo [emoji1078], mambo yanakuwa si mambo shughuli zinahamia Arusha kuyasaka madini adhimu zaidi Duniani, Yes... Tanzanite.
Wakati shughuli za migodi zinaendelea huku akijiona kama nataka anafulia zaidi, mwamba anajitafuta zaidi... anakumbuka anacho kipaji kingine kinachoweza kumuongezea kipato, naam kipaji cha Kuchora na kuchonga Vinyago... anaanza kujitendea haki kwa kuchonga Vinyago na kuvitega kwenye mahoteli makubwa ikiwemo Kilimanjaro Hotel [emoji545] Arusha...
Richard Hananja ndilo jina lake maarufu kwa sasa, Mchungaji fulani mtukutu sana wa maneno.... wakati huo anakijulikana kwa jina la Richie na sasa unaweza kumuita Richie Bilionea...
Hakuna maisha ya kijanja na utukutu wakati huo Richie hajapitia... Ofisi za vyombo vya dola ilikuwa sehemu ya maisha yake kwa kukamatwa mara kadhaa kwenye mampambano ya maisha... Moja ya matukio asiyo yasahau ni pamoja na wakati Nchi ya Tanzania inapitia msoto mkali yeye alikuwa miongoni mwa watu wanaokula bata kiana... Wakati huo kuvaa jeans [emoji158] tu unaweza kupewa mke bure. Alishawahi kukamatwa na kushitakiwa kwa kukutwa na Sabuni, Dawa ya mswaki na mafuta ya kupakaa...
Na kuonesha siyo bahati mbaya mahakamani alitinga akiwa amevalia kinachofuata sana Shati kali, Jeans ya maana na Raba mamtoni imesimama hiviii... Anasema hakimu mwenyewe alipomuona tu akamuelewa na akampa dhamana kibabe sana...
Pamoja na utukutu wake wote Richie hakuwa mtumiaji wa kilevi chochote na kwa mujibu wake ni kwamba akiwa kawaida tu anajiona basi limewaka sasa akiongeza kilevi itakuwaje? Hivyo busara kwake ikawa kutojiingiza kwenye matumizi ya vileo ili ndoto yake ya kuwa bilionea itimie kwa nidhamu... Hii ilimsaidia kuweza kumiliki viwanja maeneo ya Pugu Kajiungeni karibu na Kanisa. Alifanikiwa kujenga nyumba na kwa kuwa alililelewa katika misingi ya Kikristo basi akiwa Pugu kwake alikuwa anapenda kuhudhuria zaidi Kanisani. Na safari ya Uchungaji ikaanzia hapa kwa ushawishi mkubwa wa nje huku msukumo wa ndani nao ukiitikia....
Itaendelea...
Timothy Levy