Hi All,
Mwenzenu yamenikuta, niliyempenda kwa miaka mingi hatimaye amekataliwa na wazazi na ndugu zangu, kisa ni tofauti ya kidini baina yangu na mpenzi wangu huyo wa kike, licha ya yeye mwenyewe kuwa wazi na kunihakikishia kwamba atabadilil dini , still haiawashawishi wazazi na baadhi ya ndugu zangu. hoja kubwa ni kwamba hawa wadada ambao wanatoka islam na kuhamia ukristo huwa mbeleni wanabadilika sana, mi sina uhakika na hilo but msimamo wa wazazi ndio huo na sioni dalili ya kubadilika, ni binti ambaye ninampenda sana, mno yani. nawaza je niwapuuze wazazi nikae naye hata bila ndoa? au nimpe mimba halafu niwatege wazazi? bado sijamwambia kama nyumbani kwetu wamemkataa. help plse. (nitarudi jukwaani kesho jioni). Usiku Mwema.
Mie nilikuwa na waalim walio oana dini tofauti tofauti.
Na watoto wao, wengine wakitwa PETER, HASSANI, marry na Fatuma.
Na kuna waalim wengine watoto wao wakiwaita majina ya kiswahili, kama vile PENDO, SIRI, TUMAINI, IMANI, Vita, nk.
Kuna nesi mmoja na bwana afya mmoja dini tofauti, walipo zaa mtoto wakamuita DINI. Na mwingine Wakamwita MATATIZO.
Ushauri wangu, nendeni kaoaneni mahakamani ki siri, wazazi wasijue.
Mkitoka hapo munaishi pamoja daima bila wazazi kujua kama mumeoana.
Ndio munaweza kuzaa, na mukizaa watakuwa wanaheshm malezi ya watoto.
Kaishi mbali na wazazi wenu kunusuru penzi lenu. Na musipende kuishi na ndugu zenu nyumbani kwenu, kila mtu na maisha yake. Ila penda kuwasaidia wazazi wako, na kuwatembelea tembelea mwaka mara moja.
Nafikiri wanahofia utakimbilia kwenye uislam na watakupoteza. Watoto wako nenda nao kanisani, nenda kanisani kama kawaida ila husilazimishe mtu abadili dini, rangi yeke, ngozi yake, na umbile yake kwa ajiri eti wazazi wako hawapendi alivo. Na wazazi au jamaa wa mwanamke wakisema hawakutaki kisa wewe ni mkristo, mutaenda dini gani? wewe utabadili au yeye atabadili?
Hata ukioa mkristo anaweza kubadilika pia, binadam ni binadam.
Kuna watu wanaoana dini sawa na wanashindwana na kuna watu wanaoana dini tofauti na wanadumu daima.
Wazazi unaweza kuwazungusha zungusha, mwisho wata give up, wewe ni mwanaume bwana.
Hivo ukisikiliza wazazi jamaa ndugu watakuaribia maisha yako na watoto wako, fuata moyo wako.
Mjomba wangu alioa mkristo, hivo wazazi walimshauri amuache na aoe wa kislam.
Mjomba alimpenda sana mkewe, hivo ikabidi atumie akili yake adanganye wazazi wake.
Akawambia akimpata binti wa kiislam atakae mpenda utamuacha mkewe.
Miaka nenda miaka rudi akawa anaishi na mkewe wa kikristo, wakimtaftia mke wa kislam anaenda kunywa pombe siku ya kumuona, binti anakimbia na kutangaza bwana wenyewe mlevi. Mara ingine akivaa kipensi na singrend, alifanya vitendo akijua atakataliwa na akikataliwa basi ndio kajiokoa kuoa mke hasie panga yeye mwenyewe.
Wameishi miaka zaidi ya 40 pamoja, na wamezaa watoto 8.
Hii story niliambiwa na huyo shangazi yangu wa kikristo, alikuwa hapendwi na mama zetu hivo ugomvi kila siku na alivumilia kwa vile alimpenda mjomba na mjomba alimpenda shangazi.
Jiongoze baba, husikubali kuongozwa utaribikiwa.
Fanya vituko vya ajabu ajabu, kuwa mjanja kama wazee wa zamani.
GOOD LUCY