Niko Njia Panda... Msaada Please

Ingekua mie ningeshampa John kiti akae moyoni mwangu! Lol! Huyo Peter muzee ya mission town mmh angalie asije kuchuma mali zako mwisho wa siku akatokomea ati!za kwangu changanya na zako..
 
''Peter'' my name mate...haya bana,ntarudi baadae kuona maamuzi yako.
 
Hali zenu wana JF...
Naomba ushauri wenu tafadhali maana niko njia panda.

kuna huyu m-baba, sitamuita kaka maana ni mtu mzima. tulifahamiana miaka kama 7 iliyopita. Alinipenda sana, mpaka sasa naamini ananipenda kupita maelezo. Mimi binafsi hajawahi kuniingia moyoni. anajua simdondokei, lakini anaamini kuna siku nitabadili mawazo. Wakati huo naanza kufahamiana nae alikua na mke. ana bidii kwa kweli ya kuniweka sawa, lakini mimi wapi. kuna wakati anachoka na kukata mawasiliano, lakini vile mimi sina time nae, wala hainikeri. Mwaka unakatika anarudi tena, lakini mambo ni yale yale kwa upande wangu. Ana matatizo yake huyo kaka, sitapenda kuyaeleza ila kwa kifupi we are not compatible, nionavyo mimi we cant be togather.
Miezi kama mitatu iliyopita, karudi tena kwa nguvu mpya, na this time ni divorcee. nimeamua kua mpole fulani, japo still roho inakataa. ana kazi nzuri, ana watoto wake anaishi nao, anataka ndoa, anadai nafsi yake imeelekezwa kwangu, pamoja na kuwa namuudhi siku zote, lakini bado he thinks we can have a good life togather. Huyu nitamuita John.

Kuna mwingine, huyu namuita Peter. Peter yeye, tuliwahi kua na mahusiano miaka kama mitano iliyopita ambayo yalidumu kama miaka miwili na kiasi fulani. Tulipendana sana mpaka tulipewa majina mji huu. tukatofautiana kidogo sana na kitu cha kijinga mno, sababu ya kila mmoja kua na hasira na mwenzie, tuka break-up. niliumia na yeye naamini aliumia sana. Peter hana ajira inayoeleweka zaidi ya mission town niseme japo ana elimu. ni wale watu ambao they think hawawezi kuajiriwa.
From nowhere Peter nae anataka kurudisha majeshi, kwa nguvu zote. kibaya ni kwamba kaja wakati mmoja na John.
Peter nafsi yangu inampenda sana, na yeye naamini ananipenda, tuna match kwenye kila kitu, very compatible, interests na hobby zetu ni moja. maongezi yanalandana, namzidi kidogo umri, lakini kwangu sio issue.

Niko njia panda. John ananipenda sana na anataka ndoa, maisha yake mazuri, nikiolewa nae najua sitabahitisha kuishi, nina uhakika wa maisha bora, pesa yangu najua nitaotoa kwa kusaidia tu, lakini si lazima. Tatizo bado hayuko moyoni mwangu.

Peter, tunapendana sana, naamini hivyo, lakini hana ajira, maisha ni mishe mishe mjini mradi kunakwenda. aliwahi kuoa nae akaachana na mkewe. kwa sasa nae ni single. nikiwa nae ina maana maisha ni ku share au mimi niwajibike zaidi pale mission zinapokataa.

Mimi mwenyewe nina maisha yangu, I cant complain, najiweza, hata nisipopata msaada wa mtu maisha yangu yanakwenda vizuri bila kukuna kichwa.

Wana JF, ushauri na nasaha zenu ni muhimu. Kina dada, kama ni wewe utaenda kwa Peter au John...

Nimecheka sana leo na mm yalinikuta hao hao wakina pita na john yani hivo hivo,john alikua amenizidi 20 yrs yani anaweza kunizaa ila km unavojua wanaume hawazeeki mapema,nikamueka peter pembeni john maisha mteremko kl kitu bwerere nikaona pepo ya duniani,peter ananipa elf 10 cz ni mishen town john ananipa mpk laki kwa matumizi madodo dogo2 we shoga yalonikuta mpk nilitani ardhi ipasuke yy hakuwahi kuoa pamoja na ukubwa wake wote,kumbe alikua ana mtandao mkubwa yani ana totos hazina hesabu na ana mmama ambae anamtu mumewe,cjui uyo mume nae km anamtu na mm na uyo m_baba,kumbe yule fisadi gari,nyumba,zote ni za huyo mwanamke nae anapewa mali na mumewe, shosti mpaka yl mwanamke alihatarisha maisha yangu,nikamkumbuka peter wangu alikua anauwezo mdogo lakini hakunipa msongo wa mawazo ht kdg mda wt nilikua na tabaasam alinpnd na kunithamini,john alikua ananipa wakati mgum na alikua cheater,nikarudi kwa peter na kuomba msamaha kwa usalit,nimejifunza utu na kitu ni vitu vicvyo landana,mapenzi kwanza ndo kigezo pesa c ișue.
 
Inakuwaje mtu ambaye humpi nafasi katika nafsi yako akuweke njia panda?(John) Na issue za relationship kwangu binafsi kushauri ni kazi maana inakuwa kama vile kumchagulia mtu partner wa kuishi nae for the rest of his/her life. Kama unampenda Peter na ni mwenye kipato duni endelea nae na huyu John kinachokuweka njia panda ni pesa yake and not true love kitu ambacho huenda kikaathiri maisha yako vile vile. For JUST FOLLOW YOUR HEART only thing I can say.

Nikweli njia panda anaipata ksb ya pesa,pesa anazitesa nafc zetu wanawake,
 
Yaani mpaka sasa John anaongoza kwa kura nyingi.

Afu tayari ana kura turufu ya kwako na ya kwangu. Imebaki moja tu ya Babu mwenzangu Dark City.

Vote For John... (Nimekumbuka mshiko wangu Superman kanirusha, au adhawaiz fellow tablet klorokwini atakuwa katuuzia kibudu kwenye kiroba.... Do something Kongosho asali ya ODM)

Mkuu mwenzangu,

Niko hai hai, naitwa na wajukuu niwasaidie wasitoane macho. Nimeweza kusoma posts 2 tu, ile ya mleta mada na hii ya kwako.

Sina objection...John is my big choice....Maisha hayahitaji pressure kama hizo za Peter.

Ila mbaya zaidi na kadri ya kwa principles zangu, si jambo zuri mdada kuolewa na mdogo wake.

Nitarudi tena asubuhi kuwasalimia......

Babu DC!!
 
narudi badae kidogo

Nilisema ntarudi sababu nilikuwa nakumbuka hii story hapo chini, nadhani huyu ni Peter.

Si kila mwanamme anaweza ndoa, Peter ulishampa nafasi na akashindwa kuitumia, je unadhani sasa kaenda okota wapi akili ya kuwa mume?

Endelea na John, mapenzi yatajiset huko huko mkiwa ndani, wakati mwingine tunajifunza kupenda.
kweli konnie
 
narudi badae kidogo

Nilisema ntarudi sababu nilikuwa nakumbuka hii story hapo chini, nadhani huyu ni Peter.

Si kila mwanamme anaweza ndoa, Peter ulishampa nafasi na akashindwa kuitumia, je unadhani sasa kaenda okota wapi akili ya kuwa mume?

Endelea na John, mapenzi yatajiset huko huko mkiwa ndani, wakati mwingine tunajifunza kupenda.

umemaliza kila kitu Kongosho, kazi kwake
 
Last edited by a moderator:
Moyo wako unajibu kamili!!. Nina hakika ndicho utakachofuata hatimayeee ... all the best Dear!!
 
We Da Asia, sikiliza ushauri wangu mie kikongwe babu ODM.

Ni hivi... :

Maisha ni mafupi sana.... ukipata nafasi ya kuinjoi usiipoteze.
Peter mlishawahi kuwa pamoja na ikashindikana mkaachana. Nani alikudanganya jasiri anaacha asili? Hakuna kitu kibaya kama kuumizwa mapenzini mara mbili na mtu mmoja. Usisahau alishakuwa na mwanamke mwingine na ujue kuwa mahawara hawaachani. Pia huyu Peter huyu kama we umemshindwa, na huyu mwingine pia kamshindwa... huyu ni kunguru huyu, hafugiki huyu. (SAmahani najua unampenda lakini ndo hivyo, kunguru ni kunguru tu)

John anakupenda sana... hakuna kitu kizuri mapenzini kama kupendwa. Ana mahela, ni mtu mzima..... (Kama necha itachukua mkondo wake atakufa kabla yako, unaukwaa utajiri lol) Jifunze kumpenda bana ule maisha. maisha mafupi haya.

Kama hujanielewa namaanisha hivi... Go For John Bana.:clap2::clap2:
Hivi leo jumangapi vile? Damn!

kama mie ninavyikupenda, hapa nasubiria babu Asprin udondoke niwe bilionea....
 
Last edited by a moderator:
mwanaume hapo John tu.......
Kwanza inaelekea anakupenda.......

Achana na Peter, si ajabu kaona maisha yamempiga anataka kuja kupumzika.....
Kingine kwenye mapenzi majaribu toka kwa wenza wa zamani yanatokea....

Au peter kabadilika nini mpaka uwe nae? Asia, speaking from experiece kama kuna kosa kubwa utafanya ni kurudia mpenzi wa zamani.....atakavyokuumiza utabaki kinywa wazi...
 
Kumbe mimi mshamba sana...........sikujua mapenzi yana tafsiri tofauti kabisa nyakati hizi....Nimejifunza
 
Ningekushauri umkubali Peter lakini maelezo yako ya sababu za nyie kuachana na wakati wote mliumia hayaingii akilini

Je kama wote ni watu wa hasira mnadhani mtadumu kwenye ndoa?

Huyo mwenye kids wala sikushauri, ingawa inawezekana hata Peter ana watoto si alikuwa na mke au yeye hakuzaa. Na umesema Peter ni mdogo kwako; uoni hiyo ni sababu ya yeye kukudengulia na kwenda kuoa wa umri wake yalipomshinda ndio anakukumbuka. Be careful. Asijekuwa anakurudia umlee.

Jaribu kutafuta kwingine; achana nao wote.

"Kuna mwingine, huyu namuita Peter. Peter yeye, tuliwahi kua na mahusiano miaka kama mitano iliyopita ambayo yalidumu kama miaka miwili na kiasi fulani. Tulipendana sana mpaka tulipewa majina mji huu. tukatofautiana kidogo sana na kitu cha kijinga mno, sababu ya kila mmoja kua na hasira na mwenzie, tuka break-up. niliumia na yeye naamini aliumia sana"
 
kama mtu hum-feel kama unavyosema, unakuwa na uhusiano naye kwa miaka 7 wa kazi gani? halafu haya mambo ya kuwa na parallel relationships kumbe yapo sana eeh.... mwingine anakiri kabisa kwambs huku akichukua elfu kumi kule anachukua laki....
 
Huyo John alikuwa anakufatilia miaka saba na wakati akiwa kwenye ndoa; je ungemkubali unadhani alikuwa tayari ku divorce au alitaka uwe mpango wa kando. Je amemuacha mkewe ili awe na wewe? Ni kwa nini umeamua kuwa mpole kama unavyosema baada ya kukufuatilia sasa akiwa divorcee? Je ulimwambia kama anakupenda kweli amuache mkewe? Ana kasoro nyingine ambazo umeamua kutoziweka adharani nadhani ni kasoro kubwa ndio maana umeona hata nourma kuzianika hapa. Huyo John si mume ndugu ukimkubali utanambia hata miaka 7 alokaa mwenzio hutamaliza. Na huwezi jua si ajabu anajaribu na kwa wengine wakati huu; sidhani kama ni wewe peke ulokuwa unamvutia huku akiwa na mkewe.

Na ukiolewa na John itakuwa ngumu kwa wanaowafahamu kuamini kuwa hukuwa na uhusiano nae kwenye hiyo miaka saba ya ndoa yake. Kwa kujiweka karibu na waume/wake za watu na kuwapa vifua vy kulilia tunavunja ndoa za watu!
 
Back
Top Bottom