Ankoh Mazukuh
Member
- Jan 16, 2023
- 27
- 29
Wanangu wa JF mimi bwana nina jambo langu em naombeni ushauri kidogo.
Mimi bwana nimemaliza chuo mwaka jana mwaka huu mwishoni natimiza miaka 23 naishi na mama yangu peke yake mzee alishafariki miaka mitatu sasa ma bro zangu walishaoa masister nao vile vile.
Sasa bwana changamoto yangu ni moja nikiwa nyumbani nakuwa mvivu sana pia akili haichangamki kama nilivyokuwa chuo. Maana nilovyokuwa chuo nilikuwa napambana maana. Niliamini kwenye kipaji changu sana pia nilikuwa na dhana ya kujiajili so nilivyo kuwa chuo nilipambana mpaka nikafanikiwa kufungua ofisi yangu.
Lakini sasa tangu nimemaliza chuo uchumi uliniyumbia lakini pia nilitamani biashara yangu niihamishie mjini Dodoma ambapo ndio kuna soko kubwa na ndo nyumbani sasa tangu nimerudi naona uchawi uchawi tu sielewi kila siku nina mipango mipya.
Leo nawaza kitu baadae nabadilika. Kitu kibaya mwanzoni sikutaka kufikiria kama nyumbani watanipa mtaji lakini nilivyorudi wakaonyesha kunisaidia alafu baadae wamebadilika so kama vile nimeachwa kwenye mataa.
Sasa ushauri ninao uomba ni huu mimi nilitamani nitoke nyumbani nikapange angalau akili ichangamke kuliko kuamka sehem moja chakula uwakika sijui nini yaani sasa shida mama yangu hataki kusikia kabisa hizo habari tena nilipo jaribu kumwambia kulizuka mambo mengi kiasi kwamba akataka kunitoa kwa laana sasa nikaogopa sana.. Bimkubwa anadai kuwa mimi ni mdogo pia anasema nataka nipange kwa sababu ya wanawake so nikae nyumbani mpaka nitakapo oa.
Pia hawezi kulipa kodi mara mbili yaani imekuwa changamoto nikimwambia najilipia kodi ndo ugomvi zaidi anasema kumbe nina hela ndio zinanipa kiburi ugomvi mwingine anataka awe anajua bank nina kiasi gani na vitu vingine vingi kama hivyo sasa mimi kwangu hii ni changamoto mno.. Kuendelea kukaa nyumbani tu naona kama sikui kiakili.
Yaani tofauti na nilivyokuwa chuo kingine anadai kuwa napenda sana hela. Kwa sababu mze aliniachia nyumba ambayo kwa sasa hivi inaingiza hela na bimdashi aliahidi kunikabidhi nikimailiza chuo sasa nilichokosea ni kugusia iyo mada. Lakini binafsi sijitaji mali za urithi natamani na mimi kuwa na mali zangu kwa amani sasa hapa ni changamoto kwakweli naombeni ushauri wadau.
Mimi bwana nimemaliza chuo mwaka jana mwaka huu mwishoni natimiza miaka 23 naishi na mama yangu peke yake mzee alishafariki miaka mitatu sasa ma bro zangu walishaoa masister nao vile vile.
Sasa bwana changamoto yangu ni moja nikiwa nyumbani nakuwa mvivu sana pia akili haichangamki kama nilivyokuwa chuo. Maana nilovyokuwa chuo nilikuwa napambana maana. Niliamini kwenye kipaji changu sana pia nilikuwa na dhana ya kujiajili so nilivyo kuwa chuo nilipambana mpaka nikafanikiwa kufungua ofisi yangu.
Lakini sasa tangu nimemaliza chuo uchumi uliniyumbia lakini pia nilitamani biashara yangu niihamishie mjini Dodoma ambapo ndio kuna soko kubwa na ndo nyumbani sasa tangu nimerudi naona uchawi uchawi tu sielewi kila siku nina mipango mipya.
Leo nawaza kitu baadae nabadilika. Kitu kibaya mwanzoni sikutaka kufikiria kama nyumbani watanipa mtaji lakini nilivyorudi wakaonyesha kunisaidia alafu baadae wamebadilika so kama vile nimeachwa kwenye mataa.
Sasa ushauri ninao uomba ni huu mimi nilitamani nitoke nyumbani nikapange angalau akili ichangamke kuliko kuamka sehem moja chakula uwakika sijui nini yaani sasa shida mama yangu hataki kusikia kabisa hizo habari tena nilipo jaribu kumwambia kulizuka mambo mengi kiasi kwamba akataka kunitoa kwa laana sasa nikaogopa sana.. Bimkubwa anadai kuwa mimi ni mdogo pia anasema nataka nipange kwa sababu ya wanawake so nikae nyumbani mpaka nitakapo oa.
Pia hawezi kulipa kodi mara mbili yaani imekuwa changamoto nikimwambia najilipia kodi ndo ugomvi zaidi anasema kumbe nina hela ndio zinanipa kiburi ugomvi mwingine anataka awe anajua bank nina kiasi gani na vitu vingine vingi kama hivyo sasa mimi kwangu hii ni changamoto mno.. Kuendelea kukaa nyumbani tu naona kama sikui kiakili.
Yaani tofauti na nilivyokuwa chuo kingine anadai kuwa napenda sana hela. Kwa sababu mze aliniachia nyumba ambayo kwa sasa hivi inaingiza hela na bimdashi aliahidi kunikabidhi nikimailiza chuo sasa nilichokosea ni kugusia iyo mada. Lakini binafsi sijitaji mali za urithi natamani na mimi kuwa na mali zangu kwa amani sasa hapa ni changamoto kwakweli naombeni ushauri wadau.