Nikikutana na Kikwete

Nikikutana na Kikwete

Lukolo

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2009
Posts
5,143
Reaction score
3,210
Mwenzenu mie nina maswali kwa Kikwete. Natamani nimuone Kikwete popote, iwe ni Ikulu au safarini katika kampeni ili nimuulize maswali haya:
  1. Kabla ya kuanguka siku ya tar 21/08/2010 wakati akifungua kampeni alionyesha kushituka sana, akasema "AISEE!!" akatulia kama sekunde arobaini hivi bila kusema neno, akauma meno halafu akaendelea kusema tumefanya mambo mengi huku akielekea chini kama mtu aliyesukumwa kwa nguvu na kitu. Swali ni je Kikwete aliposema Aisee, alikuwa ameona nini? Kama alijua kuna nguvu ambayo ilimzidi,kwanini hakufanya haraka kukimbilia kiti kabla hajaanguka kwa kishindo? Je jambo hili ni la kiafya au lina nguvu za giza?
  2. Jana tar 21 ilikuwa ni mara ya tatu kwa rais kuanguka mbele ya hadhra. Je anajua tatizo linalomkabili? Ikiwa anajitambua kwamba uwezo wake wa kustahimili mikiki mikiki ya kuongoza nchi ni mdogo, haoni kwamba kuna umhimu wa yeye kuridhika na miaka mitano aliyoongoza nchi na hiyo mingine akamwachia mwingine?
Mwisho; namwombea Rais wangu afya njema, ninamwombea kwa mwenyezi Mungu ili maadui zake wote na nguvu za giza zote zinazoyanyemelea maisha ya Rais wetu na nguvu zozote zenye lengo la ama kumdhalilisha Rais wetu kwa kumwangusha mbele za watu na zile zinazokwamisha utendaji mzuri wa Rais katika kuijenga nchi.
 
... Usijitutumue kubakia ikulu kipindi cha pili .... shugulikia afya kwanza...!!!
 
... Usijitutumue kubakia ikulu kipindi cha pili .... shugulikia afya kwanza...!!!

Naliunga mkono wazo hili. Kama kazi za Ikulu ni nyingi kiasi cha kumsababishia uchovu unaomsababishia aanguke akiwa jukwaani, basi ni vema akaachana nayo, ashughulikie kwanza afya yake. Kama ni pesa tayari anayo ya kutosha na hata atakapostaafu ataendelea kutunzwa na serikali. Tayari ameshaingia kwenye historia ya nchi kama mmoja wa Marais waliowahi kuongoza Tanzania sasa anataka nini hasa?
 
Ile "aisee" iliashiria kuna kitu si shwari.....

There you are Nyani Ngabu, na mimi hamu yangu ni kujua kile alichokiona ambacho hakikuwa shwari kwake? Je alikuwa anapambana na nguvu za giza akazidiwa nguvu?
 
There you are Nyani Ngabu, na mimi hamu yangu ni kujua kile alichokiona ambacho hakikuwa shwari kwake? Je alikuwa anapambana na nguvu za giza akazidiwa nguvu?

Nadhani alichokiona au alichokisikia ni hali yake aliyokuwa anaisikia na kujua kwamba mambo si shwari. Mtu ukiwa hujisikii vizuri si mwili wako utakuambia tu....huenda yeye labda alianza kuona kizunguzungu na kuona dalili kuwa mambo hayataenda vizuri na ndipo hapo ile "aisee" ilipotoka kinywani mwake.
 
Du jamaa lazima aliona Kiza mbele, cha kunishangaza zaidi madaktari wake walimruhusu kurudi kukwaani.
whenever their is concution or loss of consious, it take a while kupata fahamu zako zote. wengine inawaaffect siku nzima.
Sasa yeye kurudi jukwaani na kuanza kuongea, wataalamu watakwambia kwamba alikuwa anongea kitu asichokijua.
 
Jibu alikwisha toa hayati Julius K. Nyerere kuwa bado JK hajakomaa na si rahisi kukomaa, kwa nini hilo ndio swali la kumuuliza!!
 
Mwenzenu mie nina maswali kwa Kikwete. Natamani nimuone Kikwete popote, iwe ni Ikulu au safarini katika kampeni ili nimuulize maswali haya:
  1. Kabla ya kuanguka siku ya tar 21/08/2010 wakati akifungua kampeni alionyesha kushituka sana, akasema "AISEE!!" akatulia kama sekunde arobaini hivi bila kusema neno, akauma meno halafu akaendelea kusema tumefanya mambo mengi huku akielekea chini kama mtu aliyesukumwa kwa nguvu na kitu. Swali ni je Kikwete aliposema Aisee, alikuwa ameona nini? Kama alijua kuna nguvu ambayo ilimzidi,kwanini hakufanya haraka kukimbilia kiti kabla hajaanguka kwa kishindo? Je jambo hili ni la kiafya au lina nguvu za giza?
  2. Jana tar 21 ilikuwa ni mara ya tatu kwa rais kuanguka mbele ya hadhra. Je anajua tatizo linalomkabili? Ikiwa anajitambua kwamba uwezo wake wa kustahimili mikiki mikiki ya kuongoza nchi ni mdogo, haoni kwamba kuna umhimu wa yeye kuridhika na miaka mitano aliyoongoza nchi na hiyo mingine akamwachia mwingine?
Mwisho; namwombea Rais wangu afya njema, ninamwombea kwa mwenyezi Mungu ili maadui zake wote na nguvu za giza zote zinazoyanyemelea maisha ya Rais wetu na nguvu zozote zenye lengo la ama kumdhalilisha Rais wetu kwa kumwangusha mbele za watu na zile zinazokwamisha utendaji mzuri wa Rais katika kuijenga nchi.

Aliona paka shume.

 
Mwenzenu mie nina maswali kwa Kikwete. Natamani nimuone Kikwete popote, iwe ni Ikulu au safarini katika kampeni ili nimuulize maswali haya:

  1. Kabla ya kuanguka siku ya tar 21/08/2010 wakati akifungua kampeni alionyesha kushituka sana, akasema "AISEE!!" akatulia kama sekunde arobaini hivi bila kusema neno, akauma meno halafu akaendelea kusema tumefanya mambo mengi huku akielekea chini kama mtu aliyesukumwa kwa nguvu na kitu. Swali ni je Kikwete aliposema Aisee, alikuwa ameona nini? Kama alijua kuna nguvu ambayo ilimzidi,kwanini hakufanya haraka kukimbilia kiti kabla hajaanguka kwa kishindo? Je jambo hili ni la kiafya au lina nguvu za giza?
  2. Jana tar 21 ilikuwa ni mara ya tatu kwa rais kuanguka mbele ya hadhra. Je anajua tatizo linalomkabili? Ikiwa anajitambua kwamba uwezo wake wa kustahimili mikiki mikiki ya kuongoza nchi ni mdogo, haoni kwamba kuna umhimu wa yeye kuridhika na miaka mitano aliyoongoza nchi na hiyo mingine akamwachia mwingine?

Mwisho; namwombea Rais wangu afya njema, ninamwombea kwa mwenyezi Mungu ili maadui zake wote na nguvu za giza zote zinazoyanyemelea maisha ya Rais wetu na nguvu zozote zenye lengo la ama kumdhalilisha Rais wetu kwa kumwangusha mbele za watu na zile zinazokwamisha utendaji mzuri wa Rais katika kuijenga nchi.
Hilo la pili ni gumu sana kwake.
 
Back
Top Bottom