Nikijenga Kigamboni itakuwaje?

Ibrah

JF-Expert Member
Mar 22, 2007
2,729
528
Wadau, bila shaka mwajua mpango wa serikali kujenga mji wa kisasa Kigamboni. Vikao kadhaa vimefnyika baina ya wakazi wa huko na Serikali lakini hakuna mwafaka ingawa serikali imeahidi fidia kubwa. Serikali pia imepiga marufuku wakazi wa huko kujenga nyumba kwa kuwa ni eneo la mradi. Haijulikani fidia yenyewe itatolewa lini na nina eneo langu nataka kujenga na ikumbukwe kuwa hakuna makubaliano rasmi baina ya wakazi na serikali.

Je, nikijenga itakuwaje? Ikiwa serikali itaamua kunibolea naweza kuishtaki?
 
Kama pesa zako si EPA tafuta eneo lingine ujenge...serikali ya kibabe hii ...nawasi wasi usije pata kwikwi ya kilio ukikaidi tetesi hizo!
 
Kama una Vijisenti vidogo vidogo kama alivyonavyo Mh.Chenge jaribu kuibeep serikali, utaona utamu ukoje!!!
 
Serikali imesimamisha kutoa building permit katika eneo la mradi (new kigamboni city) hivyo endapo utaamua kujenga bila permit hutoweza kupata fidia yoyote. Ni vyema kusubiri mpaka hapo utakapojua hatma ya eneo hilo, ijapokuwa kuna siasa nyingi sana na watendaji wa wizara wanapeleka mambo kwa kasi ya konokono.
 
ni vyema kuheshimu kila mamlaka iliyopo kwani mamlaka yote yatoka kwa Mungu..heshimu serekali ili ikuletee maendele!Tumeagizwa tusimamishe ujenzi hivyo inabidi tueshimu serekali yetu kaka...
 
ni vyema kuheshimu kila mamlaka iliyopo kwani mamlaka yote yatoka kwa Mungu..heshimu serekali ili ikuletee maendele!Tumeagizwa tusimamishe ujenzi hivyo inabidi tueshimu serekali yetu kaka...

Nadhani hapa hakuna maendeleo yoyote,zaidi ya mji kuja kukaliwa na wazungu tu.lakin bro nakushauri ucje beep nyuki mwisho utaambulia manundu kwa we ni mzawa lkn ardhi si yako maana awa washikaji ni wababe,upande mwingine nawashukuru marekani kwa kutumia mwanya wa ujinga wetu maana watajenga military base yao hapo na bandari hapo na kuizika bandari ya dsm,je kama mapato hayatatuhusu itakuwaje,nadhani c tutakuwaombaomba ndan ya nchi yetu.
 
Hii kitu mkuu bado haijakaa vizuri kabisa kwa upande wetu sisi wakazi wa Kigamboni,ila watu wanajenga kwani mpango haujakuwa wazi na hao watendaji wenyewe hawako wazi kama inavyo paswa na ilivyo elezwa na wachangiaji hapa.
Ni hivi karibuni tu,waziri mwenye dhamana ya ardhi MH. Mama,Pfs.Tibaijuka kwenye mkutano wa hadhara pale Machava alisema wazi wazi kwamba "MTAHAMA",pamoja na maswali mengi juu ya hilo la kuhama hakujibu swala la msingi, "...ni vipi tutahama..??" ikiwa na maana ya thamani,malipo na wapi tutapelekwa kama fidia inavyo elekeza kwenye mpango kazi wa NEW CITY.Watu walimuuliza maswali mengi lakini hakujiibu kitu zaidi ya MTAHAMA.
Lakini muda unakwenda na hakuna lolote la maana lilokwisha fanyika kwa upande wa serikali/muwekezaji/wawekezaji zaidi ya ile ASSESSMENT iliyofanyika miaka miwili iliyopita yaani 2009 baada ya hapo ni kimya zaidi ya habari iliyotolewa kwenye gazeti la mwana nchi la Aprili na siku zisizo zidi wiki kufatiwa na Mkutano wa Mama Tibaijuka.

Sasa,kama mmiliki na mwananchi/binadamu muda hausimami kwako toka bandiko la MARUFUKU kuisha muda wake na hari za ugumu wa maisha kupanda kwa maana ya kodi za nyumba na vifaa vya ujenzi,......"ushauri wangu"......"kama ulikua una ramani tayari ya ujenzi,basi jenga hata servant quarter/vyumba viwili au vitatu na choo kwa rugha ya Darsalam Banda la uwani kupunguza makali hayo ya maisha kwani ardhi unayo na haina faida kukaa buree wakat hata bank hauwezi kuitumia kukopa (ila kwa mshangao wangu recently ACCESS BANK wanaweza kukukopesha ukiwa na jengo zuri na hati/offer,si jui kwa ma-BANK mengine kama wameshaanza TENA kukopesha).
,shida hizi za ukali wa maisha watendaji wetu wamezifumbia macho,ukiwa na kibdanda chako Kigamboni,kama sio mbali sana hata kwa miguu mjini unafika kupunguza NAURI za daladala na Misongamano ya foleni zinazo zidii mjini (ingawa sasa hata huku pia foleni za magari kuvuka kivuko zimeongezeka,kutokana na uzembe wa waendesha hivyo vivuko,mabaharia na menejimenti kwa ujumla wao) ni bola kuweka jengo la bei rahisi ambalo ikiwa utavunjiwa basi iwe sawa na KODI YA MIAKA MIWILI AU MITATU kwa nyumba ya kupanga mjini!....narudia tena huu ni ushauri wangu
 
Back
Top Bottom