Nikalikuta 'vuvuzela' kanisani

Nikalikuta 'vuvuzela' kanisani

.... hongera zao kwa ubunifu. Ilimradi tu ili noga watu wakafurahia Ibada ya kusifu bial kuvunja miiko ya kanisa

Hapo kuna watu wanatamani wavurumishe bomu humo liwaue wote humo. Hizi dini nyingine... hakika mungu wao ni shetani. Yaani wenzao wakifurahi wao hawapendi.
 
Nimeonja pendo lako,
nimejua u mwema...
Nitakushukuru,nitawainua wote wakusifu wewe.
 
YESU NI MWEMA..

Nimetafakari habari zako nami
nashindwa kuelewa kabisa
Binadamu angenipa neema kesho
angechoka kunipa zaidi
Lakini wewe hauna kikomo, wala mvua
yako haina majira
Bwana, wanyesha mvua, Bwana, kwa
walio jangwani
Bwana, wawasha jua, Bwana, mpaka
baharini
Kweli Bwana wewe ni mwema sana
Nitasimulia miji, Yesu ni mwema, Yesu
ni mwema
Nitahubiri vijijini, Yesu ni mwema Yesu
ni mwema
Nitayafafanua haya –
Watu wote wapate kuyajua—
Nitasimulia nchi –
1. Niliwaza kwa ubinadamu mpaka
mwisho wa kufikiri
Ukataka nijipe moyo, nisihofu
kitu
Kwa kuwa humtupi
anayekutumainia
Ukataka nijipe moyo, nisihofu
kitu, kamwe
2. Uzoefu wa mapito haya
ukaninyima usingizi . . .
Kanuni za dunia zikavunja
matumaini . . .
3. Giza lilipotanda mchana
likanifunika usoni . . .
Nikapiga kelele hofu kuu
ikanisonga . . .
< h i t i m i s h o >
[t|b] Naimba he he, naimba leo
Naimba he he, naimba mimi
Ulijua wazi kwamba mimi
sikuwa nastahili,
Kwa sababu mimi mdhaifu mwili
na roho
Ukaruhusu nifanikiwe juhudi
zangu
Makusudi ili nione ukuu wako
Ndugu wanipende, jamaa
waniheshimu
Marafiki wanijali, wanisaidie
Ndiyo maana leo, mimi
nakurudishia;
[w] Utukufu ni wako milele
Sifa heshima ni vyako daima
Wewe peke yako unastahili
Usifiwe na uhimidiwe!
Nakushukuru Bwana, kwa kuwa
umeniona asante
Nakushukuru Bwana . . .
Nakupa utukufu . . .
Milele na milele . . .
Nakushukuru Bwana . . .

by B.MUKASA
Cc charminglady Kongosho Asprin
 
Last edited by a moderator:
Nimeonja pendo lako,
nimejua u mwema...
Nitakushukuru,nitawainua wote wakusifu wewe.

Composer B.MUKASA

1. Nimeonja pendo lako, nimejua u
mwema
Nitakushukuru nitawainua wote
wakusifu wewe
Nitawaongoza wote waimbe kwa
furaha
Nitakushukuru nitawainua wote
wakusifu wewe
Ukarimu wako ee Bwana, na
huruma yako wewe
Msamaha wako ee Bwana, na
upole wako wewe
Umenitendea wema usiopimika
Nitakushukuru nitawainua wote
wakusifu wewe.
2. Kina mama simameni, piga
vigelegele -
Kina baba nyanyukeni, mkapige
makofi -
3. Watu wote nesanesa, chezeni
kwa furaha -
Inua mikono juu, mshangilieni
Bwana -
4. Watawa washangilie, makasisi
waimbe -
Walei warukeruke, waseme
aleluya -
5. Vitambaa mikononi,
vipeperushwe juu -
Na vichwa viyumbeyumbe, kwa
mwendo wa kuringa -
6. Nitakushukuru mimi, na nyumba
yangu yote -
Nitayatangaza haya, maisha
yangu yote -
 
Hili song huwa nalikubali sana cku hizi hadi maharucn linagongwa,sasa likipigwa najihic kama vile niko meza moja Bwana Yesu
 
Utaskia unaulizwa, vuvuzela imeandiwa wapi kwe biblia itumike, subiri waamke mda wa futari.
 
Yaani mimi nilifikiri umemkuta Nepi Nawuye kanisani. Kumbe ni instrument. Basi sawa.
 
Manjagata, nani kakuomba utoboe namna hii kwa kutaja majina ya watu? Watu walishaelewa.

Nisamehe bure Mkuu! Mavuvuzela ni mengi mno mkuu, hilo nalijua mimi tu kuwa ni livuvuzela! Sikujua kama na wewe unalijua hivyo mkuu!
 
Last edited by a moderator:
YESU NI MWEMA..

Nimetafakari habari zako nami
nashindwa kuelewa kabisa
Binadamu angenipa neema kesho
angechoka kunipa zaidi
Lakini wewe hauna kikomo, wala mvua
yako haina majira
Bwana, wanyesha mvua, Bwana, kwa
walio jangwani
Bwana, wawasha jua, Bwana, mpaka
baharini
Kweli Bwana wewe ni mwema sana
Nitasimulia miji, Yesu ni mwema, Yesu
ni mwema
Nitahubiri vijijini, Yesu ni mwema Yesu
ni mwema
Nitayafafanua haya &#8211;
Watu wote wapate kuyajua-
Nitasimulia nchi &#8211;
1. Niliwaza kwa ubinadamu mpaka
mwisho wa kufikiri
Ukataka nijipe moyo, nisihofu
kitu
Kwa kuwa humtupi
anayekutumainia
Ukataka nijipe moyo, nisihofu
kitu, kamwe
2. Uzoefu wa mapito haya
ukaninyima usingizi . . .
Kanuni za dunia zikavunja
matumaini . . .
3. Giza lilipotanda mchana
likanifunika usoni . . .
Nikapiga kelele hofu kuu
ikanisonga . . .
< h i t i m i s h o >
[t|b] Naimba he he, naimba leo
Naimba he he, naimba mimi
Ulijua wazi kwamba mimi
sikuwa nastahili,
Kwa sababu mimi mdhaifu mwili
na roho
Ukaruhusu nifanikiwe juhudi
zangu
Makusudi ili nione ukuu wako
Ndugu wanipende, jamaa
waniheshimu
Marafiki wanijali, wanisaidie
Ndiyo maana leo, mimi
nakurudishia;
[w] Utukufu ni wako milele
Sifa heshima ni vyako daima
Wewe peke yako unastahili
Usifiwe na uhimidiwe!
Nakushukuru Bwana, kwa kuwa
umeniona asante
Nakushukuru Bwana . . .
Nakupa utukufu . . .
Milele na milele . . .
Nakushukuru Bwana . . .

by B.MUKASA
Cc charminglady Kongosho Asprin
Watu na wakushukuru Eeh Mungu...... By Kashumba.
Nikiziangalia mbingu..... By Kashumba
Inueni vicha vyenu enyi malango By FA Nyundo
Ishara kubwa imeonekana mbinguni.... Byabato


Baaaassss
 
Waumini wa leo ni wavivu katika kumsifu Mungu kwa namna ya muziki ndio maana ndugu yangu uwepo wa 'vuvuzela' umekushangaza.

Nyakati za waumini wa kweli waliomuabudu Yehova walitumia kila kifaa cha muziki kiwezacho kutoa ala maridhawa katika ibada au maadhimisho yao kwa BWANA.

Mathalani:

1 Mambo ya Nyakati 13:8 Wakacheza Daudi na Israeli wote, mbele za Mungu, kwa nguvu zao zote; na kwa nyimbo na kwa vinubi, na kwa vinanda, na kwa matari, na kwa matoazi, na kwa tarumbeta.

Mkuu watu8 nitake radhi. Mimi si kwamba ni muumini wa kubabaisha. Kikubwa hapa ni utaratibu wa vuvuzela katika kanisa katoliki. Itashangaza hapa siku yakianza kutumika magitaa.
 
Last edited by a moderator:
Jumapili iliyopita nilihudhuria misa takatifu katika Kanisa katoliki la Mt.Anoarite,Makuburi Dar es Salaam. Ni misa ya kuanzia saa tano na robo asubuhi. Katika misa hiyo ya kuadhimisha sikukuu ya Watakatifu Petro na Paulo,wanakwaya wa Kwaya ya Mt.Kizito walitumia, pamoja na ngoma na kinanda, vuvuzela kunogesha uimbaji wao. Vuvuzela lilitumika mwanzo hadi mwisho wa misa katika uimbaji.


Kiukweli,sijawahi kushuhudia vuvuzela kanisani (kanisa katoliki) wakati wa misa. Nikiri kuwa vuvuzela lilichagiza vyema uimbaji na kuufanya ujae baraka zaidi. Hongereni wanakwaya ya Mt.Kizito kwa ubunifu huu. Nilibarikiwa sana kwa misa nzima na uimbaji wenu. Vuvuzela liko juu...

Baba Mtakatifu Francisco wakati wa Sala ya Malaika wa Bwana??????????? kwenye Maadhimisho ya Siku kuu ya Watakatifu Petro na Paulo, miamba wa imani anasema, hii pia ni Siku kuu ya Jimbo kuu la Roma ambalo limejengekwa katika ushuhuda wa kifo dini cha Mitume hawa wawili???????
Ndugu zangu kauli hii ya baba mtakatifu haiwezi kukubalika bila kufanyiwa kazi na utafiti wa hali ya juu,anazungumzia Petro tunayemjua aliyekuwa Mwanafunzi wa Yesu au Petro mwingine?na huyu mtume Paulo anayezungumziwa ni huyu tunayemjua au mwingine?
Hivi kanisa la Roma lilianzishwa lini?na nani hasa mwanzilishi?huo uzushi wa kusema ni mtume Petro na Paulo haukubaliki hata kidogo
Mama Maria ameingizwaje hapo?katika kusoma kwangu Biblia sijawahi kuona mahali Yesu ameongea kuhusu Mama Maria ambaye alikuwa Mama yake Yesu,wala Biblia haijaelezea kwa kina historia ya huyu Mama zaidi ya kumshukuru kwa kutuzalia Mwokozi
Eti Kanisa limejengwa kwenye Mathayo 16:18,nami nakuambia wewe ndiye Petro na juu ya mwamba huu nitalijenga Kanisa langu wala milango ya kuzima haitalishinda???????
Yesu aliongea kwa mafumbo kamwe kanisa hai la Mungu haliwezi kujengwa juu ya Binadamu,aliongea parable,
Sijasoma popote pale Yesu aliposema mkitaka maombi yenu yafike Mbinguni mwombeni Mama yangu ayalete???huo ni ujinga ambao hauvumiliki,nataka mjue kwamba ujinga ni dhambi,
Mkitaka kusali semeni hivi,Baba yetu uliye Mbinguni,jina lako litukuzwe,Ufalme wako uje,mapenzi yako yatimizwe hapa Duniani kama huko Mbinguni,utupe leo riziki yetu,utusamehe makosa yetu kama nasi tunavyosamehe waliotukosea,usitutie majaribuni bali utuoke na Yule mwovu,kwa kuwa ufalme ni wako na nguvu na utukufu hata milele Amin!!!!
Je kuna Mama Maria hapo?ndivyo Petro alivyofundishwa ,je mnataka kusema Petro alipotoka na kufundisha mambo tofauti na aliyofundishwa?petro asingeweza kugeuza aliyofundishwa na Yesu na kuchomeka majina na taratibu ambazo hakupokea kutoka kwa master wake
Mtume Paulo tunajua background yake alipokuwa njiani kuelekea Damasks kuwakamata Wakristo walioamini akatokewa na Yesu njiani na kupigwa upofu,kisha akapewa majukumu ya kufanya,katika majukumu sijaona jina la Mama Maria hapo
Ni nini hasa kipo nyuma ya kanisa la Roma?na kwa nini wamebadili Biblia inayosomwa na makanisa yote na kubadili baadhi ya vifungu,
Someni kitabu cha Matendo ya Mitume,soma chote na rudia mara kadhaa utajua jinsi Kanisa lilivyoanzishwa,wakati wa kufata mkumbo umepita ndugu zangu,kaa chini tafakari kama kweli imani unayofata na njia unayofata ya kumwabudu Mungu ni sahihi,hata kama umezaliwa ndani ya kanisa la Roma una haki ya kujiuliza kama kweli upo mahali panapostahili au la!!!!!
 
Mkuu rosemarie,hoja yako hasa ni ipi? Tuachie ukatoliki wetu tafadhali
 
Last edited by a moderator:
Kwaya za Dar hazijui kuimba kabisa, wanazidiwa na za Iringa. Ila kiboko yao MZA, shangwe mwanzo mwisho. Walau Makuburi wanajitahidi sana.
Teh,Na zile wowowoooooh....! za wanakondooo wa kike,bac hatareee
 
Utaskia unaulizwa, vuvuzela imeandiwa wapi kwe biblia itumike, subiri waamke mda wa futari.
Naona hujiamini kama umeenda kupeleka posa kwa mtoto wa kihindi tuwahoji ili iweje kwani ninyi huwa mna kitu mnachofanya ambacho kimeandikwa,nyie huwa c mambo yenu mpendavyo wenyewe,kuoana mashoga ruksa,padri shoga ruksa,kuvisosonora vikondoo vidogo ruksa,sasa tushangae vuvuzela hata mdundiko hatushangai,just keep it on....!
 
Wakatoliki siku hizi nao wanapiga miziki ya kwasa-kwasa kanisani yani ni zamani ndio walikuwa wakiwasema wapentekoste ila saivi wao ndio viranja.
 
Back
Top Bottom