Nifanyeje ili mke wangu ashike mimba haraka

Nifanyeje ili mke wangu ashike mimba haraka

mdizi 2021

Member
Joined
May 4, 2021
Posts
55
Reaction score
53
Habarini ndugu zangu.

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu.mimi mdogo wenu nimeingia kwenye ndoa mwezi wa kwanza mwaka huu,hadi sasa mimi na shemeji yenu tuna miezi 6 ya ndoa yetu .lakini mke wangu mpaka sasa navyoandika uzi huu hana dalili yeyote ya kuwa na mimba inaniuma sana kwa kweli.

Je, nifanyeje ili mke wangu ashike mimba haraka au nitumie dawa gani niongeze vichocheo kwenye SPERMS ziwe imara kutungisha mimba, labda tatizo lipo huko. Niseme tu ukweli sikuwai kulala na mwanamke huko nyuma hata mmoja ila nilikuwa mzee wa CHAPUTA kwa sana, na mke wangu nimemkuta Bikira.

Najua humu wapo watu wajuvi na wazoefu bila kusahau madaktari waliobobea kwenye taaluma ya AFYA. Kwa wiki mimi na mke wangu tunakutana mara 3 kufanya tendo la ndoa.
 
Miez sita michache Sana hyo watu wanakaa Hadi miaka 20 na wanapima wanaambiwa hakuna tatizo lolote mtoto Ni neema kutoka kwa Mungu kuwa na subra kwenye Hilo

Nendeni hospital pata ushaur wa gynerclgst Mwenyez Mungu atakusaidia

Ikishindikana hospital Rudi katika Tiba mbadala Mana ukiwa na majini mahaba mwili huwa wanablock had kizaz
 
Tulia kijana, habari ya mtoto itakuja tu. Mbona bado mapema mno kuwaza habari za watoto?

Fanyeni tendo kama starehe tu, na kusiwe na presha au mawazo juu ya mtoto. Mimi nilipata mtoto baada ya mwaka hivi, wengine miaka hata miwili , punguza hofu, safari ndo imeanza.
 
Mwombe mungu na uache kupania "K" ipo tu siku zote, unalala nayo una amka nayo, usipange muda wa Sex, mda wowote ikidisa hapo hapo mpe show, itakamata tu !

Pia, hakikisha asikose "Morning glory" ile asubuhi mwamshe akakojoe, then piga kimoja cha fasta ndio muamke ,msali , muoge kwenda kazini"
ila ni mapema sana, Bashite alikaa miaka 9 ndio akapata.
 
Habarini ndugu zangu. kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu.mimi mdogo wenu nimeingia kwenye ndoa mwezi wa kwanza mwaka huu,hadi sasa mimi na shemeji yenu tuna miezi 6 ya ndoa yetu...
Pole sana, nakuombea mungu akafanyd wepesi. Lakin Punyeto ni dhambi ni uzinzi kama uzinz mwingine, Rudi kwa imani yako fanya toba juu ya hiyo dhambi. Hilo litakusaidia mkuu

Sent from my SM-G9250 using JamiiForums mobile app
 
Miezi 6 tu mkuu unaanza kulalama, watu wanakaa miaka na miaka bila kupata mtoto na huwa wanapata.

Kuwa na Subira, mtoto utapata, hiyo ni Neema kutoka kwa Muumba. Muda ukifika atakujalia.
Thanks mkuu mungu akubariki kwa ushauri wako
 
Back
Top Bottom